Makete kuangukia mikononi mwa CHADEMA

Makete kuangukia mikononi mwa CHADEMA

Singwa

Member
Joined
May 26, 2011
Posts
65
Reaction score
25
Wanajukwaa

Kuna kila dalili za jimbo la Makete mkoani Njombe kuangukia mkononi mwa CHADEMA mwenye uchaguzi utakaofanyika baadaye mwaka huu. Tangu kuanzishwa kwake na Nguli wa majingambo Tuntemeke Sanga jimbo hili kimekuwa likiongozwa na CCM.

Mwaka huu jimbo hili laweza kuwa mikononi mwa CHADEMA baada ya kazi kubwa ya team ya kijana mwenye ushawishi aliyetangaza nia ya kugombea Ubunge, AHADI ASAJILE MTWEVE kufanya ziara ya ujenzi wa chama kijiji kwa kijiji na kujihakikishia ushindi wa kimya kimya.

Mtweve amekuwa gumzo kwenye radio za Makete hasa Kitulo fm na Green fm pamoja na majukwaa ya Whatsapp na Facebook. Pia wananchi wa Makete bila kujali tofauti za vyama wameonyesha kuvutiwa na siasa za kijana huyu baada kuonyesha ujasiri wa kuwatetea wanyonge.

Kila laheri CHADEMA Makete, kila laheri Ahadi Mtweve

😀😀😀😀😀😀
 
Watakuwa wamekosea Sana kumpa huyu kijana,wawaulize wafanyakazi wa tigo branch za Lindi na Mtwara asivyofaa.
 
Kila lakheri CDM ila msipuuze wazo la huyu jamaa niliyenukuu uzi wake hapa chini.Ni muhimu mwananchi wakapata mtetezi makini. Akishindwa si yeye bali ni chama.

Loading October..........


Watakuwa wamekosea Sana kumpa huyu kijana,wawaulize wafanyakazi wa tigo branch za Lindi na Mtwara asivyofaa.
 
Kusema tu kuwa waulize wafanyakazi wa tigo na Mtwara inasaidia nini? Au unachuki binafsi na mtu, yeyote anayekubalika na watu huwa hakosi kutafutiwa zengwe.
 
sasa wewe singwa siumeshaweka post yako hapa acha ajitetee mwenyewe kuhusu ya tgo lindi na mtwara bwana
 
Sina uhakika kama ni mwanachama wa hapa JF, kwa kuwa mimi ndio nimeleta uzi huu hapa, ngoja nichimbue hizi tuhuma za mchumia tumbo, nitakuja na Majibu hapa
 
Watakuwa wamekosea Sana kumpa huyu kijana,wawaulize wafanyakazi wa tigo branch za Lindi na Mtwara asivyofaa.

Nimeongea na wafanyakazi kadhaa wa Tigo branch za Lindi na Mtwara wanasema huyo jamaa alikuwa ni mchapakazi sana, hapendi uvivu, mtetezi wa wateja na asiyependa mizaha kwenye mazingira ya Kazi. Tabia yake hiyo ilimfanya achukiwe na baadhi ya wafanyakazi wenzake.
 
Watakuwa wamekosea Sana kumpa huyu kijana,wawaulize wafanyakazi wa tigo branch za Lindi na Mtwara asivyofaa.

Kwenye siasa hakuna biashara mkuu kaa chonjo waacha chadema speed yao inatisha..zimbombo zibe nkaaafuuu
 
sasa wewe singwa siumeshaweka post yako hapa acha ajitetee mwenyewe kuhusu ya tgo lindi na mtwara bwana

Ajitetee kitu gani?angekuwa amekorofisha angeshitakiwa wacheni siasa za maji taka.
 
Kusema tu kuwa waulize wafanyakazi wa tigo na Mtwara inasaidia nini? Au unachuki binafsi na mtu, yeyote anayekubalika na watu huwa hakosi kutafutiwa zengwe.

Pia mti wenye matunda mazuri ndio upigwao mawe
 
Wanajukwaa

Kuna kila dalili za jimbo la Makete mkoani Njombe kuangukia mkononi mwa CHADEMA mwenye uchaguzi utakaofanyika baadaye mwaka huu. Tangu kuanzishwa kwake na Nguli wa majingambo Tuntemeke Sanga jimbo hili kimekuwa likiongozwa na CCM.

Mwaka huu jimbo hili laweza kuwa mikononi mwa CHADEMA baada ya kazi kubwa ya team ya kijana mwenye ushawishi aliyetangaza nia ya kugombea Ubunge, AHADI ASAJILE MTWEVE kufanya ziara ya ujenzi wa chama kijiji kwa kijiji na kujihakikishia ushindi wa kimya kimya.

Mtweve amekuwa gumzo kwenye radio za Makete hasa Kitulo fm na Green fm pamoja na majukwaa ya Whatsapp na Facebook. Pia wananchi wa Makete bila kujali tofauti za vyama wameonyesha kuvutiwa na siasa za kijana huyu baada kuonyesha ujasiri wa kuwatetea wanyonge.

Kila laheri CHADEMA Makete, kila laheri Ahadi Mtweve

😀😀😀😀😀😀

Mwambieni asonge mbele hasiogope hao wanafiki wenye siasa za maji taka..songa kijana songa cdm kwa watanzania.
 
Updates za tuhuma za mchumia tumbo kwa bwana Ahadi Mtweve ni hivi...

Ni kweli bwana Mtweve amefanya kazi tigo Mtwara na Lindi kwa miaka tofauti. Alianza kazi Mtwara mwaka 2012 na kufanya kazi kama Customer Service Executive na baadaye akawa promoted kuwa Branch Supervisor na kuja Lindi mwaka 2014 mwanzoni baada ya tigo kufungua branch yao pale, Mwezi desember 2014 ali-resign kwa lengo la kwenda huko jimboni kwake Makete kujipanga na huo ubunge wake.

Source: Wafanyakazi wenzake Lindi na Mtwara na yeye mwenyewe.
 
Updates za tuhuma za mchumia tumbo kwa bwana Ahadi Mtweve ni hivi...

Ni kweli bwana Mtweve amefanya kazi tigo Mtwara na Lindi kwa miaka tofauti. Alianza kazi Mtwara mwaka 2012 na kufanya kazi kama Customer Service Executive na baadaye akawa promoted kuwa Branch Supervisor na kuja Lindi mwaka 2014 mwanzoni baada ya tigo kufungua branch yao pale, Mwezi desember 2014 ali-resign kwa lengo la kwenda huko jimboni kwake Makete kujipanga na huo ubunge wake.

Source: Wafanyakazi wenzake Lindi na Mtwara na yeye mwenyewe.

Habari hizi si za kweli nadhani mreta mada ameamua kumpigia debe Ahadi Mtweve. Hakuna chombo cha habari kinachomzungumzia hata kimoja na wala si facebook wala WhatsApp wanaomwongelea.

Mimi binafsi ni mwenyeji wa Wilaya ya Makete na vile vile nipo kwenye mitandao karibu yote ya watu wenye asili ya Wilaya ya Makete. Sijamsikia zaidi ya Group ya WhatsApp ya Makete Platform na Makete Yetu Forum ambako alitoa CV yake nusunusu. Walipomwambia aeleze sehemu alizowahi kufanyakazi; hakuwa tayari kuwambia watu waliyomwuliza. Hili limewatia shaka watu wengi kuwa huenda hakuondoka vizuri alivyokuwa tigo na voda.

Wilaya ya Makete haiwezi kumpa mtu wa kujifunzia kuitawala. Wanachotakiwa ni kuanza na Udiwani ili wakomae kwanza kabla ya kukurupukia Ubunge. Vijana wote waliyotia nia kugombea Ubunge Wilaya ya Makete bado hawana sifa za kuwa Wabunge. Wengi wao wanasukumwa na njaa na uchu wa kuwa wabunge. Ubunge sio makalio kwamba kila mtu atakuwa nayo.

Wilaya ya Makete tupo makini sana hivyo hatuwezi kuruhusu watu wasiokuwa na sifa kutuongoza eti tu wanataka kuwa wabunge.

Mleta mada naomba uangalie vizuri taarifa zako. Usije na wewe ukawa unasukumwa na njaa ili ushibishe tumbo lako.
 
WASIFU WA MTANGAZA NIA

MAELEZO BINAFSI

Jina: Ahadi Asajile Mtweve
Kuzaliwa: 29/09/1981
Mahali Pa Kuzaliwa: Mahanji - Matamba, Makete
Hali ya Ndoa: Nimeoa na nina watoto wawili
Kujiunga na Chama: 11/4/2007
Simu ya mkononi: 0764660220, 0715365850
Email: amtweveone@gmail.com

ELIMU/TAALUMA

Shahada: Mawasiliano ya Umma (Mahusiano) 2008, SAUT - Mwanza
Shahada: Sheria (LLB) Kuanza mapema mwezi October 2015, OUT - Dar es Salaam

A' Level: History, Geography & Language (HGL), 2002 - 2004, Mwakaleli High School - Mbeya

O'Level: F III - IV 2000 -2001, Wanging'ombe Sec School - Njombe, 1998 - 1999 F I - II, Itamba Sec School - Makete

Primary: 1989 - 1991, D I & II, Ngoje S/M, 1992 - 1995, D III - VII, Mahanji S/M

UONGOZI NDANI YA CHAMA

Mgombea: Baraza kuu Taifa (Vijana) 2011, Kura hazikutosha

Katibu Mwenezi (W): 2009, CHADEMA Makete

Katibu mwenezi Tawi: CHADEMA SAUT - Mwanza, 2007/08

MIKOA NILIYOTEMBELEA TANZANIA

Nimetembea mikoa yote Tanzania bara isipokuwa mkoa wa TANGA

NCHI NILIZOTEMBELEA
Ni Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Mozambique, Zanzibar na Malawi

UJUZI NA UWEZO

- Kufanya harambee za kutafuta pesa kwa ajili ya miradi ya jamii (Fundrising)
- Kuishi popote na kushirikiana na watu wote pasipo kujali elimu au mazingira wanayoishi
- Kuandika miradi ya maendeleo na kuwapelekea wananchi (Project writeup)
Creativity and Researches for community problems solving
- Kusikiliza na kuchambua kwa kina maudhui ya ujumbe (3D communication analysis)

NINAAMINI
Ukweli humuweka mtu huru na atakuwa huru kweli kweli. Nitakuwa tayari kuusema ukweli mahali popote nitakapohitajika kuusema hata kama itanipasa kuhatarisha maisha yangu kwa ajili ya kusema ukweli.

Huyo ndio mimi kwa wasionifahamu.
 
Nimeamua kuiweka CV yake ili na huyo mleta mada asome aone alichokisema kama kinafanana na ukweli ulivyo
 
Habari hizi si za kweli nadhani mreta mada ameamua kumpigia debe Ahadi Mtweve. Hakuna chombo cha habari kinachomzungumzia hata kimoja na wala si facebook wala WhatsApp wanaomwongelea.

Mimi binafsi ni mwenyeji wa Wilaya ya Makete na vile vile nipo kwenye mitandao karibu yote ya watu wenye asili ya Wilaya ya Makete. Sijamsikia zaidi ya Group ya WhatsApp ya Makete Platform na Makete Yetu Forum ambako alitoa CV yake nusunusu. Walipomwambia aeleze sehemu alizowahi kufanyakazi; hakuwa tayari kuwambia watu waliyomwuliza. Hili limewatia shaka watu wengi kuwa huenda hakuondoka vizuri alivyokuwa tigo na voda.

Wilaya ya Makete haiwezi kumpa mtu wa kujifunzia kuitawala. Wanachotakiwa ni kuanza na Udiwani ili wakomae kwanza kabla ya kukurupukia Ubunge. Vijana wote waliyotia nia kugombea Ubunge Wilaya ya Makete bado hawana sifa za kuwa Wabunge. Wengi wao wanasukumwa na njaa na uchu wa kuwa wabunge. Ubunge sio makalio kwamba kila mtu atakuwa nayo.

Wilaya ya Makete tupo makini sana hivyo hatuwezi kuruhusu watu wasiokuwa na sifa kutuongoza eti tu wanataka kuwa wabunge.

Mleta mada naomba uangalie vizuri taarifa zako. Usije na wewe ukawa unasukumwa na njaa ili ushibishe tumbo lako.

Ubunge sio utawala ni uwakilishi
 
updates za tuhuma za mchumia tumbo kwa bwana ahadi mtweve ni hivi...

Ni kweli bwana mtweve amefanya kazi tigo mtwara na lindi kwa miaka tofauti. Alianza kazi mtwara mwaka 2012 na kufanya kazi kama customer service executive na baadaye akawa promoted kuwa branch supervisor na kuja lindi mwaka 2014 mwanzoni baada ya tigo kufungua branch yao pale, mwezi desember 2014 ali-resign kwa lengo la kwenda huko jimboni kwake makete kujipanga na huo ubunge wake.

Source: Wafanyakazi wenzake lindi na mtwara na yeye mwenyewe.

sawa mtweve,,,muda uliotumia kureplay inaonyesha,we ndo mtweve
 
Makete anayekubalika ni Jackson Mbogella Mpiganaji Aliyejitolea Maisha Yake Kuwatetea Wanyonge wa Makete kwa Kupambana na Ufisadi Uliokuwa Umetamalaki Wilayani hapa kwenye taasisi za kanisa KKKT na Halmashauri ambapo mapambano hayo yalipelekea watu kufukuzwa kazi.

Jackson Mbogella ndiye chaguo la Wananchi wengi hapa Makete na wameapa iwapo ukawa watamsimamisha mgombea mwingine basi kura zao zitarudi ccm.

Jackson Taifa Mbogella anamtaji wa wapigakura kutoka vyama vyote hii inatokana na msimamo wake aliyouonesha wa kuupinga ufisadi kutoka rohoni na wanyonge wa Makete bado wanakumbukumbu za namna Jackson alivyowapigania haki zao
 
Back
Top Bottom