Hizo states alizoshinda Obama mostly are liberal,progressive and educated na hata Clinton atazibeba kiurahisi tuu,American politics left/right ni muhimu kuliko rangi ya mtuKuna majimbo mengi tu ambayo Obama alishinda ambayo zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wake ni Wazungu.
Sasa kwenye hayo majimbo alishindaje kama Wazungu walio wengi hawakumpigia kura?
Iowa zaidi ya 90% ya watu wake ni Wazungu. Obama alishinda hilo jimbo chaguzi zote mbili.
Wisconsin zaidi ya 85% ya wakazi wake ni Wazungu. Obama alishinda chaguzi zote mbili tena ushindi mzuri tu.
Minnesota na yenyewe zaidi ya 80% ya wakazi wake ni Wazungu. Huko nako Obama alishinda ushindi mnono tu.
Illinois, huko anakotokea Obama zaidi ya 70% ya wakazi wake ni Wazungu. Obama alishinda kwa landslide.
Hiyo ni mifano michache tu ya majimbo yenye Wazungu wengi kuliko minorities wote combined lakini Obama alishinda.
Sasa alishinda shindaje huko bila kupigiwa kura na majority ya Wazungu wa huko?