Muendelezo wa nukuu ya suicide note ya kevin Carter. Party 4
Mwaka unaofuatia mwezi april Kevin anashinda tuzo ya Pulitzer Prize kwa picha aliyompiga mtoto aliyedhoofu kusini kwa sudani.
Miezi mitatu baada ya kushidna tuzo, Tar 27 julai 1994, Kevin Carter anaendesha gari hadi kwenye kiwanja cha study center, sehemu ambayo alikuwa anacheza wakati akiwa na mtoto. Baada ya kufika pale anapark gari yake na kufunga mpira kutoka kwenye exhaust ya gari yake na kuingiza ndani ya gari yake na kujifungia. Anavuta hewa ya carbonmonoxide ambayo ni sumu na mwisho anafariki dunia.
Kwa maelezo ya Jaoa silva alivyoojiwa na mwandishi wa kijapani Akio Fujiwara, anasema Kevin alitumia dakika 20 kupiga ile picha, alifanya hivyo kupata picha nzuri lakini pia anaamini Kevei aliataka kumbeba mtoto ila moyo ukasita akiogopa maambuzi ya magonjwa kabla ya kumfukuza kunguru na kumuaacha mtoto bila msaada.
Kevin alishindwa kumsaidia mtoto kwa kuwa alishapewa maelezo ya
kutoshikana au kugusana wa watu ili kuepuka maambukizi ya magonjwa. Kutokutoa msaada kwa mtoto ndio
kulikompa kevin carter msongo wa mawazo.
Baada ya post ya ile picha, na wasomaji kuanza kuulizia kama mtoto alifika kituoni, kevin anajua nini kilitokea sudani, kevin ndio anaejua kama kweli mtoto alipona na kutokumsaidia motto ndio kikawa chanzo chake kupata msongo wa mawazo, ndio kikasababisha kifo chake..
Baada ya maojiano ya silva na fujiwara kuna wanaosema silva hakutaka kuweka kila kitu wazi, Kevin alifariki kwa msongo wa mawazo, msongo ulisababishwa na yeye mwenyewe.
Ile Dhambi ya kutokumsaidia yule mtoto ndio ilikuwa inamtafuta hadi akapata msongo wa mawazo, ukirudi nyuma utakumbuka kevin aliwahi kupigwa jeshini baada ya kumsaida mhudumu wa magahawa, kevin alikuwa anaumia anapoona mtu anaonewa.
Kwa ajili ya ukumbusho wa Kevin Carter kuna wimbo ulitungwa na
Manic street Preachers unaitwa Kevin Carter na Movie inaitwa Bing Bang Club
Huu ndio ulikuwa mwisho wa Kevin Carter.
Wimbo wa Kevin carter



Rest in peace kevin Carter
Pumzika kwa amani Kevin Carter.
**********Mwisho********