2
.Mtume Muhamad;Muhammad (kwa Kiarabu "Mwenye kusifika sana"; jina kamili kwa kirefu ni
محمد بن عبد الله بن عبد ﺍﻟﻤﻄﻠﺐ ﺍﻟﻬﺎﺷﻤﻲ Muhammad bin 'Abd Allāh bin 'Abd al-Muţţalib al-Hāshimī) anaaminika katika dini ya
Uislamu kuwa ni
mtume wa mwisho wa
Mungu (
Allah) kwa
binadamu.
Muhammad aliishi Makka kwa muda wa miaka 53, arubaini (40) katika hiyo akiwa ni mtu wa kawaida kabla ya kupewa utume, na 13 akiwa ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu.
Maisha yake Makka yalikuwa ya taabu tangu utotoni mwake, kwani alizaliwa yatima kisha alipokuwa katika ujana wake alikuwa akifanya kazi ya kuchunga mbuzi na kondoo wa watu wa Makka kwa vijipesa kidogo mpaka alipofika umri wa miaka ishirini na tano akapata kazi ya kumfanyia biashara Khadija, bibi mtukufu wa Kikureshi ambaye baadaye alikuja kuwa mkewe, na kuzaa naye aghlabu ya watoto wake.
Mtume Muhammad, baada ya kupewa amri ya kuguria
Madina, aliondoka na kuhamia mji huo ambao ulimpokea na kumkubali na kumsaidia na kumtukuza na kumlinda na maadui.
Ingawa
Wayahudi wa Madina walikataa kumsadiki kuwa nabii kama wale wa
Biblia, aliendelea kuhubiri huko na tangu mwaka wa kwanza alitunga Hati ya Agano iliyokubaliwa na Wamadina wote: ndiyo asili ya
Umma, jamii ya waumini.
Mtume Muhammad aliishi Madina kwa muda wa miaka 10 mingine akitangaza dini ya Mwenyezi Mungu na huko watu wengi na makabila mbali mbali ya Kiarabu yaliingia dini ya Uislamu kwa makundi makundi.
Mwaka 630 Muhammad akiwa na nguvu za kutosha aliweza kurudi Makka na kuiteka, akairudisha
Kaaba ambayo ndiyo chanzo cha Waislamu wote ulimwenguni kwenda kufanya
Sala na
Hija.