Makapuku Forum

Makapuku Forum

*MJINI SHULE*

Kuna mdada nilimkopesha pesa kwa ahadi kuwa baada ya wiki moja atanirejeshea pesa zangu.

Baada ya wiki moja nampigia simu hapokei simu zangu, nimempigia zaidi ya mara kumi (10) bila ya mafanikio!

Kila nikimpigia simu hajibu simu zangu, nikahamua kumwandikia message kwa WhatsApp...!

_Hello Mamu, Nakupigia simu sio kukudai pesa zangu, ila nataka kukwambia kuwa hapa Ubungo Plaza kuna wadada wawili walikuwa wanapigana kumgombea Mumeo (Baba Nang'oto). Ilikuwa vuta nikuvute na mumeo alikuwa kasimama tu anawaangalia akitabasamu. Baada ugomvi kwisha akaondoka na mmoja wao na kumwacha yule mwingine akitukana matusi kama hana akili nzuri._

--
Kisha nikaituma ile message

Baada ya dakika kama mbili hivi, akanipigia simu nami wala sikupokea simu yake... Akapiga tena na tena kama mara ishirini hivi wala sikupokea.

*Akatuma message akiniuliza...*

_Hao wanawake unawajuwa, ...mume wangu na huyo mwanamke wameelekea wapi, wewe unawajuwa hao wanawake waliopigana, yaani hapa nimechanganyikiwa kwa kweli...!_

Nikaisoma message yake wala sikuijibu, nikamchunia kimyaaa...!

Akanipigia tena simu mara tano, sikupokea simu zake, kimyaaa...! Akaniandikia message nyingine....

...Nakupigia jamani pokea simu basi nina pesa zako nataka nikupe... Naomba basi tukutane mjini unihadithie vizuri...!


Nami nikamjibu...

_Nitumie hizo pesa kwenye Namba yangu ya Mpesa, ili nipitie sheli kujaza mafuta nije mjini kukupitia nikupeleke mahala walipo...!_


Baada ya dakika 2 message ikaingia, kuangalia balance yangu ya Mpesa, nikakuta kaingiza pesa zangu zote ninazo mdai...!

Nikazima simu nikajilalia zangu kimyaaa.... Kama sio mie!
Hahahaha...Mjini shule ila usije na madaftari.
 
1958 - Michael Jackson anazaliwa.

Alikuwa ni mfalme wa muziki wa pop Duniani.

Ni mmoja wa wanamuziki bora wa wakati wote kuwahi kutokea Ulimwenguni.

Anashikilia rekodi mbalimbali kama vile Albam iliyouza nakala nyingi zaidi duniani ni Albam yake ya Thriller.

Alijibadilisha rangi toka mweusi mpk kuwa mweupe.

Alifariki Dunia mwaka 2009 lakini Jina lake litaishi miaka mingi sana.
1472482709027.jpg
1472482713234.jpg
1472482718287.jpg
1472482723728.jpg
1472482728594.jpg

.......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom