Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo March 23/2025
Screenshot_20250323_070338_Chrome.jpg
 
Huyu ndie Didi Stone Binti Koffi Olomide. Majina yake kamili ni Didi-Stone Naïke Olomidé. Mama yake anaitwa Aliane Olomide. Didi Stone alizaliwa mwaka 1999 huko Neuilly-sur-Seine, Ufaransa.

Koffi Olomide alimpa jina Didi Stone ili kuenzi urafiki wake na tajiri wa Didi Kinuani, mfanyabiashara mkubwa wa vito wa Congo. Didi Stone ni mwanamitindo ambaye ametoka katika majarida kadhaa makubwa ya mitindo duniani ikiwemo The Vogue.

Mama yake Didi Stone ni mke wa tatu wa Koffi Olomide. Mke wa kwanza wa Koffi alikuwa anaitwa Marianne Makosso aliyezaa nae watoto wawili. Mke wake wa pili anaitwa Stephanie Godee aliyezaa nae watoto watatu.

Mke wake wa tatu ni Aliane Olomide, ambaye ndie mama yake Didi Stone. Huyu amezaa nae watoto watatu. Koffi ameishi kwenye ndoa na mama yake Didi Stone kwa muda wa miaka 27.

Walitalakiana mwaka 2022 baada ya kuibuka tetesi kwamba Koffi alikuwa kwenye mahusiano na mwanamke mwingine anayeitwa Cindy.

Talaka hii ilimuingiza Koffi kwenye migogoro na binti yake. Wimbo wa Maman Eyanga wa Koffi Olomide inaaminika ulikuwa ni ujumbe kwa huyu binti yake.

Katika wimbo huo, Cindy anaimba, "Mtoto hapaswi kunena maneno machafu, Angalia usije ukauzwa kwa bei ya uzi wa kushonea kwenye soko Ia dhahabu". Inaaminika Koffi ana mtoto mwingine na Cindy...!
Screenshot_20250323_071927_Instagram.jpg
 
Mwalimu wa kike alikuwa anawabaka wanafunzi wake mpaka akapata mimba, sasa ametupwa jela miaka 25 kwa ubakaji!

Mahakama nchini Marekani imemhukumu Alissa McCommon kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wake wa kiume mwenye umri wa miaka 12.

Mahakama ilielezwa kwamba mwalimu huyu licha ya kwamba alijua wajibu wake kama mwalimu na mlezi lakini alishindwa kusimama wajibu huo na kuwashawishi wanafunzi wake kufanya nae ngono.

Mwanamke huyu alikuwa anawaita wanafunzi nyumbani kwake na kucheza nao magemu lakini baadae aliwashawishi na kufanya nao ngono. Jumla ya wanafunzi 21 wenye umri wa miaka 12 hadi 17 waliripoti kufanya ngono na mwalimu huo ikiwemo ngono asilia na ngono kwa njia ya mdomo.

Mwalimu huyo alipata mimba baada ya kumbaka mwanafunzi wake mwenye umri wa miaka 12. Vipimo vya DNA vimethibitisha kwamba mtoto huyo ndie baba wa mtoto wa mwalimu.

Mama wa mwanafunzi huyo alilia mahakama na kuieleza mahakama kwamba mwalimu huyo alikuwa ameharibu maisha ya mtoto wake kwa kumuingiza katika michezo ya wakubwa kabla ya umri.

Mwalimu Alissa tayari ameisha jifungua na mtoto wake analelewa na bibi ambae ni mama wa mwanafunzi wa aliyekuwa anabakwa na mwalimu.

Mwalimu huyo alikiri mashtaka yote mahakamani, hivyo mahakama imemhukumu kifungo cha miaka 25 jela. Pia mahakama imeamuru leseni yake ya ualimu ifutwe milele. Mwalimu Alissa ni mama mwenye umri wa miaka 39..!
Screenshot_20250323_072239_Instagram.jpg
 
Mganga alisema anataka macho ya mtoto, mama yake akamuuza mtoto wake kwa sangoma..!

Mahakama nchini Afrika Kusini imeelezwa kwamba Kelly Smith mama wa watoto watatu alimuuza mtoto wake kike Joslin Smith
kwa sangoma kwa sababu mtoto huyo alikuwa na macho pamoja na ngozi alivyokuwa anavitaka mganga kienyeji nchini humo.

Mwanamke huyo anashtakiwa na watu wengine wawili akiwemo aliyekuwa mpenzi wake kwa tuhuma za utakaji nyara na ulanguzi wa binadamu.

Polisi wanadai kwamba wakati wa msako wa kumtafuta mtoto wake mwanamke huyo alionekana kutojali na muda mwingi alikuwa akimuwazia tu mpenzi wake.

Mchungaji mmoja aliieleza mahakama kwamba, mwanamke huyo aliwahi kumwambia akipata mteja atauza watoto wake hata kwa Shilingi laki 7 hadi milioni 2.

Jirani wa mwanamke huyo alitoa ushahidi na kueleza kwamba, mwanamke huyo alimfuata na kumwambia amefanya jambo la kipumbavu kwa sababu amemuuza mtoto wake kwa sangoma.

Mtoto huyo alikuwa na macho ya bluu na ngozi ya kuvutia ambayo mganga alikuwa anavitafuta.

Bado mahakama haijaelezwa kwa nini sangoma alikuwa anahitaji macho ya rangi hiyo. Nchini Afrika Kusini waganga wa kienyeji huwa wanaitwa Sangoma.

Polisi nchini humo wanaamini kwamba kama mtoto huyo bado yuko hai basi atakuwa amesafirishwa kwenda mojawapo ya nchi za Afrika Magharibi..
Screenshot_20250323_072454_InstaPro2%20.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom