Makapuku Forum

Farhan Jr

MTIBWA SUGAR, binafsi niseme baada ya miaka mingi ya kuibua ndoto, kufurahia vipaji, kuleta neema kwa familia zisizo na neema, kufuta machozi mkoa wenye vipaji vingi na kuwa mwangaza kwenye giza basi safari hiyo inaelekea kufikia tamati, ijapo bado sitaki kuamini kama tunashuka bado.

Kwetu sisi MOROGORO hii ni zaidi ya klabu, zaidi ya maisha ambapo watoto kutoka Bonde la Mto Kilombero walipata nafasi ya kuamini, Vijana kutoka safu za Milima ya Uluguru na maporomoko ya Udzungwa walipata sababu ya kuamini, kutoka nyika za Gairo mpaka Bonde la mpunga Mlimba na Mizimu ya Kolelo ilibariki mpaka Milima ya Ndororo huko Ulanga.

Muda unakimbia, ndoto zinafifia, nuru inapotea, historia inaenda kufutika? Nyumbani kwa soka la vijana, Mabingwa wa kihistoria wanaenda kupita njia ya Tukuyu Stars? Cosmo na Pamba? Wapi Reli ya Morogoro na Nyota Ndogo, Moro United za Morogoro? Soka la Mkoa wa Morogoro linaenda kuanguka, sifa inaenda kupoteza na nuru kwenye kiza imezima.

UNITED WE STAND, tutasimama wote mpaka mwisho kuimba wimbo wa ushindi, hakuna atakayekimbia kwakuwa hii ni timu yetu, utamaduni wetu na kielelezo chetu cha ubora, tutapigana mpaka nwisho wa pumzi yetu, ikitokea tumeondoka basi tunawaomba sana enzini yale mema yetu na ndoto za Vijana ziendelee, ikitokea tumeondoka naomba niseme its not a Goodbye, its a see you soon

Screenshot_20240430_091145_InstaPro%20.jpg
 
Farhan Jr

Wakati WAKULIMA wenzangu wamenituma niripoti hii habari nikaitwa Muongo tena na Senior Journalists kabisa na wengine wakisema natumika, ila UANDISHI WA HABARI hauna Uchawi, ukipata taarifa ifanyie kazi kisha peleka duniani.

Kuachana kwa General na Simba ilianza viashiria wazi kabisa wakati wa dirisha la dogo la usajili, walipishana kwenye sera wala sio pesa! General alitaka Striker aliyewahi kucheza mpaka EPL kwenye klabu ya Watford hapo zamani, haikuwa issue pesa bali UMRI wa Mchezaji miaka kama 35, Simba walitaka Project mpya na sio kujaziana tena wachezaji wenye umri mkubwa.

Hapo ndipo shughuli ilipoanza, Kocha anataka Wachezaji experienced lakini hawatodumu kwa muda mrefu! Kifupi alitaka CV yake zaidi kuliko maslahi ya timu ya Simba, hapo ndipo nilianza kupata FIRST HAND INFORMATION kuhusu moshi ndani ya Simba, ilikuwa suala la Club policy.

Nilitaka kupost tangu mwezi Desemba lakini baada ya kuwasiliana na Profesa wangu ambaye kwangu ni Role Model akaniambia achana na hii kitu kwasasa, unaweza kuripoti kitu sahihi lakini wakati sio sahihi, SIMBA na YANGA kwenye hii nchi zina nguvu kubwa mno, itulize kalamu subiri timing! Na hii ni kanuni moja wapo kwenye UANDISHI, unapima Impact ya stori yako.

Niliiachia juzi kabla ya fainali ya Muungano kwakuwa nilifahamu anaondoka baada ya hapo and so it happened! Tuliacha kilimo Morogoro ili tuje tuifanye hii kazi kwa weledi halafu tuondoke zetu turudi kwenye kilimo.

Baada ya Benchika kuna Kiongozi mwingine mkubwa ataondoka Simba mwishoni mwa msimu, ni dhahiri Simba wanataka kuanza upya na THE NEW ERA HAS ARRIVED.

Screenshot_20240430_091426_InstaPro%20.jpg
 
Klabu ya Yanga, imefungiwa kusajili mpaka itakapomlipa aliyekuwa mchezaji wake Lazarus Kambole. Uamuzi huo umefanywa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) baada ya mchezaji huyo kushinda kesi ya madai dhidi ya klabu hiyo.
.
Mchezaji huyo raia wa Zambia alifungua kesi FIFA akidai malipo ya malimbikizo ya mishahara na fidia ya kuvunjiwa mkataba. Yanga ilitakiwa iwe imemlipa ndani ya siku 45 tangu uamuzi huo ulipotolewa, lakini haikutekeleza hukumu hiyo.

Wakati FIFA imeifungia klabu hiyo kufanya uhamisho wa wachezaji kimataifa, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) nalo limeifungia kufanya uhamisho wa ndani
Screenshot_20240430_092433_InstaPro%20.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom