Makapuku Forum

Rais Mstaafu wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu zake za rambirambi kwa Mke wa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Mama Dorcas Membe akielezea alivyopokea taarifa za kifo cha Membe kwa mshtuko na huzuni kubwa.

Dr. Kikwete amesema “Nimemfahamu Membe miaka mingi, tumetoka nae mbali na tumesaidiana kwa mengi, Familia zetu, na mapito ya maisha yetu yamehusiana sana, Bernard KamilliusMembe alikuwa ni Mtu wa msaada mkubwa kwangu katika maisha yangu ya kikazi na kisiasa”

“Nilimuamini na kumtumainia katika nafasi zote alizohudumu kwenye Baraza langu la Mawaziri, aliwahi kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Mambo ya Ndani, na Wizara ya Nishati na Madini, aliwahi pia kuwa Waziri wangu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa miaka 9 ambapo alifanya kazi kubwa na zuri ya kuendeleza maslahi ya Tanzania katika medani za Kimataifa”

“Nautambua mchango wake mkubwa alioutoa kwenye Chama Cha Mapinduzi alipokuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Mjumbe wa Kamati Ku na Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa katika Sekretariati ya Halmashauri Kuu ya Taifa, katika nafasi zote hizo, alijitoa kwa moyo wake wote na kuacha alama za Kudumu”

“Nilimfahamu Mheshimiwa Membe kama Mwanadiplomasia Mbobezi, Mwanamikakati makini, Msomi mzuri, Mcha Mungu, Mzalendo,Mchapakazi hodari na Mtu jasiri ambaye hakuogopa kusema na kulisimamia analoliamini.

“Hakika Taifa limepoteza mmoja wa watu wake muhimu, natoa salaam za rambirambi na mkono wa pole kwako Shemeji yangu Dorcas Membe na Watoto wenu Cecilia, Richard na Dennis, pamoja na Wajukuu, Ndugu na Jamaa wa Marehemu Bernard Kamilius Membe, nawapeni pole kwa msiba mkubwa uliowakuta, lakini napenda kuwahakikishiakuwa hamko wapweke, Mimi pamoja na Mke wangu Salma na Wana Familia wetu wote, tuko pamoja nanyi katika majonzi na kuomboleza, tunawaombea kwa Mola awajalie moyo wa subira na ustahamilivu katika kipindi hiki kigumu mnachopitia, tukumbuke daima “Sisi sote ni Waja wake, na kwake tutarejea" Bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe, Tumuombee kwa mola marehemu mpendwa wetu, apumzike kwa amani na Roho yake aiweke Mahala Pema Peponi. Amina”
Screenshot_20230513_065406.jpg
 
Mwanamtandao maarufu Nchini Tanzania William Malecela maarufu kama ‘LeMutuz’ ambaye pia ni Mmiliki wa Online TV ya LeMutuz amefariki dunia leo Jijini Dar es salaam.

Taarifa za kifo cha LeMutuz ambaye ni Mtoto wa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania John Malecela zimethibitishwa na Ofisi yake pamoja na baadhi ya Ndugu zake.

Mmoja wa Ndugu hao ameiambia @AyoTV_ kuwa wanasubiri taarifa rasmi ya familia ili Vyombo vya habari vipewe taarifa kamili juu ya kifo hicho cha Rafiki wa wengi Ndugu LeMutuz.
Screenshot_20230514_145214.jpg
 
MABOSI MAN U WAMEZINGUA
.
Ole Gunner Solskjaer amesema mara ya kwanza alipowaambia mabosi wa Manchester United waende kumnunua straika Erling Haaland alikuwa anapatikana kwa Pauni 4 milioni tu. Solskjaer alimnoa straika huyo wa mabao 51 huko Manchester City, Haaland wakati walipokuwa pamoja kwenye kikosi cha Molde, kabla ya straika huyo kutimkia RB Salzburg na baadaye Borussia Dortmund.
.
Solskjaer alisema: “Niliwapigia simu Man United miezi sita kabla sijaenda kuwa kocha niliwaambia wamchukue huyu straika, lakini hawakunisikiliza. Nili-waambia watoe Pauni 4 milioni wamchukue Haaland, hawakufanya hivyo.”
.
Haaland akaishia kwenye mikono ya Man City, ambao walilipa Pauni 50 milioni kum-mnasa kutoka Borussia Dortmund na Sasa straika huyo anathaminishwa kuwa na thamani ya Pauni 200 milioni.
.
Man United kwa sasa inashida kubwa ya Namba 9 licha ya Marcus Rashford kuwafungia mabao 29 msimu huu, huku mara nyingi akicheza kutokea kwenye wingi ya kushoto. Anthony Martial haeleweki na Wout Weghorst hana jambo.

Screenshot_20230514_145751.jpg
 
SPURS, NAGELSMANN HAKUNA STORI TENA
.
Aliyekuwa Kocha wa Bayern Munich, Julian Nagelsmann ameripotiwa hatazamwi tena kama mtu mwafaka wa kwenda kuchukua mikoba ya kuinoa Tottenham Hotspur msimu ujao. Tangu Spurs imfute kazi Antonio Conte karibu miezi miwili iliyopita, miamba hiyo ya London imekuwa ikisaka kocha mpya kwa ajili ya kuja kufanya kazi kwenye kikosi chao kwa msimu wa 2023-24.
.
Nagelsmann alikuwa akipewa nafasi kama chaguo la kwanza kwenye ukocha wa timu hiyo baada ya kuachishwa kazi huko Bayern Munich, Machi mwaka huu. Ilielezwa kwamba kocha huyo mwenye umri wa miaka 35 alishafanya hadi usaili Spurs.Hata hivyo, ripoti mpya ya Sky Sports News, inadai kwamba Spurs imeachana na Nagelsmann na hakuna mpango huo.
.
Kocha wa Bayer Leverkusen, Xabi Alonso ni kocha mwingine anayepewa nafasi huko Spurs, huku mwingine ni bosi wa Feyenoord, Arne Slot na wa Eintracht Frankfurt, Oliver Glasne.
Screenshot_20230514_145854.jpg
 
Farhan Jr

NDUGU MGENI RASMI wasifu mfupi sana wa huyo Msela aliyesimama hapo juu, ambaye alisajiliwa kipindi ambacho wengi hawakutarajia makubwa kutoka kwake, akawaambia ASILI YA MUDA ni uvumilivu na aliwaambia nipeni nafasi kwakuwa MUDA UNAATHIRI, nipo hapa kwa ajili ya athari chanya.

Anaitwa nani? MUDATHIR YAHYA ABBAS! Anaishi wapi? JANGWANI! Kazi yake nini? Kuufanya mpira wa miguu uwe kazi rahisi sana katikati mwa uwanja! One hell of a brilliant Midfielder.

Ubingwa wa msimu uliopita ulikuwa kwa ajili ya HATERS wa msimu huu ni kwa ajili ya MASHABIKI, enjoy WANANCHI

Screenshot_20230514_150320.jpg
 
Farhan Jr

David Gill alivyoondoka Manchester United mpaka leo wanakosa Mtendaji Mkuu kama yeye na mara nyingi wanakiri kuwa viatu vyake ni vikubwa sana Mtu kuvaa hata Peter Kenyon pia kama tunamkumbuka.

Mariana ameondoka Chelsea na licha ya yote bado timu inastruggle sana, huyu Mama alichukiwa sana na Watu wa dili jumlisha Mawakala waliokuwa wanampiga Roman, lakini aliweka misingi yake! Mpaka leo tunapambana kwakuwa viatu ni vikubwa.

Mkurugenzi kama Fabio Paratici aliondoka Juventus licha ya yote lakini kuna msoto wanapitia, mambo mengi yanaenda mrama kwakuwa injini moja wapo imesepa Turin.

Nyuma ya anguko la Barcelona kuna majina ya Ferran Soriano na Xiki, nyuma ya uimara wa City kuna Ferran na Xiki, ni ukweli usiopingika kwa namna Watendaji hao walikuwa muhimu.

Beppe Marotta yupo zake Inter Milan na Ivan Gazids yupo AC Milan, PSG wana Luis Ocampos! Ni Watendaji wa maana sana wanaopiga mzigo wa maana sana.

Matajiri wanapambana kuwekeza sana Ulaya ila wanapambana sana kuwa na Watendaji wa kuipush vision na mission!

Kwanini nimetumia picha ya Barbra? Ni kwakuwa amevaa jezi ya Argentina ambao walimteua Cesar Luis Menotti ambaye ni Kocha wa zamani wa timu ya taifa na aliwapa ubingwa wa dunia 1978, ndie Mkurugenzi wa timu zao za taifa kuanzia 2019 na alipewa mpango wa miaka 10, akabeba World Cup mwaka wake wa tatu tu.

Navutiwa sana na soka la nje! Wenyewe wapo tayari kuwapoteza Wachezaji ama Makocha ila sio Watendaji wanaobeba vision na siku hizi wanalipwa sana.

Screenshot_20230514_150430.jpg
 
Nabil Maaloul (60) amejiuzulu nafasi yake ya Ukocha Mkuu wa Espérance Tunis mara moja kufuatia kipigo cha aibu cha mabao 3-0 wakiwa nyumbani dhidi ya Alahly mchezo wa mkondo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kocha gani wa Bongo unayemjua alijiuzulu baada ya kushindwa kufikia malengo_________?
Screenshot_20230514_150616.jpg
 
"Ninamuomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na awape subra wafiwa wote [kifo cha Bernard Membe] katika kipindi hiki cha majonzi tunachokipitia." - Rais Samia Suluhu
Screenshot_20230514_150756.jpg
 
"Kifo chake [hayati Bernard Membe] kimeacha pengo kubwa sio tu katika familia yake, bali kwa taifa la Tanzania na mataifa aliyoyafanyia kazi katika kulinda utu na heshima ya mtu." - Rais Samia Suluhu Hassan
Screenshot_20230514_150852.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom