Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
Rais wa Marekani Joe Biden amewasili Mji Mkuu wa Ukraine, Kyiv kwa ziara yake ya kwanza ya kushtukiza na iliyofanywa kwa usiri mkubwa kwasababu ya tahadhari za kiusalama, hii ni ziara ya kwanza ya Biden nchini Ukraine tangu kuanza kwa vita ya Ukraine na Urusi mwaka mmoja uliopita.
Ziara hiyo ya kushtukiza ameifanya wakati akisafiri kwenda nchi jirani ya Poland kukutana na Rais Andrzej Duda, New York Times wanaripoti kwamba safari hiyo ya siri ya Biden kwenda Ukraine imefanywa kupitia treni kutoka mpaka wa Poland.
Ripoti zinasema Biden aliondoka pia Marekani bila taarifa na hata taarifa zilipovuja kuwa ataenda Ukraine, Maafisa wa Marekani walikanusha.
Kabla ya mkutano na Waandishi wa Habari, Joe Biden amefanya mazungumzo na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na kuwamwagia sifa Ukranie kwa mapigano yao ya kishujaa licha ya ukosefu wa uzoefu wa kijeshi “Tena cha kustaajabisha ni kwamba Watu wa Ukraine ni Raia wa kawaida ambao hawakuwahi kupata mafunzo ya kijeshi lakini jinsi walivyopiga hatua ya kishujaa ni jambo ambalo na Ulimwengu wote unajivunia.
Ziara hiyo ya kushtukiza ameifanya wakati akisafiri kwenda nchi jirani ya Poland kukutana na Rais Andrzej Duda, New York Times wanaripoti kwamba safari hiyo ya siri ya Biden kwenda Ukraine imefanywa kupitia treni kutoka mpaka wa Poland.
Ripoti zinasema Biden aliondoka pia Marekani bila taarifa na hata taarifa zilipovuja kuwa ataenda Ukraine, Maafisa wa Marekani walikanusha.
Kabla ya mkutano na Waandishi wa Habari, Joe Biden amefanya mazungumzo na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na kuwamwagia sifa Ukranie kwa mapigano yao ya kishujaa licha ya ukosefu wa uzoefu wa kijeshi “Tena cha kustaajabisha ni kwamba Watu wa Ukraine ni Raia wa kawaida ambao hawakuwahi kupata mafunzo ya kijeshi lakini jinsi walivyopiga hatua ya kishujaa ni jambo ambalo na Ulimwengu wote unajivunia.