Makapuku Forum

Makapuku Forum

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limesema katika kipindi cha January hadi December, 2022 Jeshi hilo limekabiliana na matukio ya moto 1854 yaliyosababisha vifo vya Watu 32 na majeruhi 66.

“Tulifanikiwa kufanya uokoaji katika maeneo 567 ikiwa ni pamoja na maeneo ya migodu, mashimo ya vyoo, ajali za barabarani, mafuriko, Mito, Mabwawa na Baharini”

“Matukio hayo yalisababisha vifo na majeruhi 1,010, matukio makubwa yaliyovuta hisia kwa wananchi na Taifa kwa ujumla ni pamoja na kuungua kwa soko la Karume na Vetenari yaliyopo Jijini Dar es Salaam, ajali ya Ndege ya Kampuni Ndege la Precision Mkoani Kagera, ajali ya gari la shule ya Msingi ya King David Mkoani Mtwara na kuungua kwa Mlima Kilimanjaro”
Screenshot_20230103_051555_OGInsta%2B.jpg
 
Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa - IMF amesema mwaka huu wa 2023 utakuwa mgumu kwa sehemu kubwa ya uchumi wa ulimwengu kwa sababu madola muhimu yanayochangia katika ukuaji ambayo ni Marekani, Ulaya na China yote yako kwenye msukosuko.

Mkurugenzi Mkuu wa IMF Kristina Georgieva ameiambia televisheni ya CBS ya Marekani kuwa mwaka huu utakuwa mgumu zaidi kuliko uliopita.

Oktoba mwaka 2022, IMF ilipunguza mtazamo wake wa ukuaji uchumi wa ulimwengu katika mwaka wa 2023 ikizingatia kuzorota kwa uchumi kutokana na vita nchini Ukraine pamoja na shinikizo la mfumuko wa bei na viwango vya juu vya riba vilivyowekwa na Benki kuu kama ile ya Marekani kwa lengo la kutuliza shinikizo la mfumko wa bei.
Screenshot_20230103_051833_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt Hussein Ali Mwinyi amefungua Shule ya Ghorofa ya Sekondari Makangale Kisiwani Pemba iliyojengwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa fedha za Covid-19 Kupitia Shirika la fedha Duniani (IMF).

Kuelekea miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar Rais Dkt Hussein Ali Mwinyi anaendelea kuzindua miradi mbalimbali iliyojengwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Screenshot_20230103_051936_OGInsta%2B.jpg
 
Dubai imeondoa ushuru wake wa asilimia 30 kwenye pombe ikiwa ni jitihada za kukuza utalii ambapo pia itaacha kulipisha pesa ya ada kwenye leseni binafsi ya pombe ambayo alitakiwa kuwa nayo yeyote anayetaka kununua pombe, mabadiliko haya yatadumu kwa kipindi cha mwaka mmoja wa majaribio.

"Kwa kuondolewa kwa asilimia 30 ya ushuru wa Manispaa na leseni ya bure ya pombe, kununua vinywaji unavyopenda sasa ni rahisi na kwa bei nafuu kuliko hapo awali" Mmoja wa Wasafirishaji wakuu wa pombe Dubai” —— ameandika kwa furaha kwenye mtandao wake.

Baadhi ya mitandao ya Dubai imeripoti kuwa Dubai imefanya hivi ili kukabiliana na ushindani unaoletwa na Majirani zake ambao wameweka masharti nafuu kwenye sekta za starehe na hoteli na kuwavutia Wakazi wa Dubai kuendesha magari hadi kwenye hizo falme nyingine na kununua pombe kwa wingi.

Inaelezwa kuwa Watu wasio Waislamu nchini Dubai hutakiwa kuwa na angalau umri wa miaka 21 ili kuruhusiwa kunywa pombe na hutakiwa pia kubeba leseni ya pombe iliyotolewa na Polisi.
Screenshot_20230103_052031_OGInsta%2B.jpg
 
Upelelezi wa kesi ya usafirishaji wa dawa za kulevya Kilogramu 34.89 aina ya Heroin inayomkabili aliyekuwa Kocha wa Makipa wa klabu ya Simba, Muharami Sultan na wenzake umekamilika.

Wakili wa Serikali, Carolina Matemu amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Mary Mario kwamba tayari upelelezi wa shauri umekamilika, wamepeleka taarifa Mahakama Kuu hivyo wanasubiri irudi ili waweze kuwasomea maelezo ya mashahidi washitakiwa hao.

Kutokana na hali hiyo, aliiambia Mahakama kwamba ipange tarehe nyingine ya kutajwa kesi hiyo ambapo Hakimu amekubaliana na ombi hilo na kuahirisha kesi hiyo hadi Januari 16, 2023.
Screenshot_20230103_052300_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Urusi Vladimir Putin katika hotuba yake ya kuelekea mwaka mpya amesema nchi yake haitajisalimisha kamwe kwa nchi za Magharibi kutokana na hatua ya nchi hizo ya kuitumia Ukraine kama chombo cha kuisambaratisha Urusi “Tunapigana na Ukraine ili kujilinda”
Screenshot_20230103_052748_OGInsta%2B.jpg
 
Naibu Katibu Mkuu,TAMISEMI anayeshughulikia elimu Dr. Charles Msonde amesema Wanafunzi 1,073,941 waliochaguliwa kidato cha kwanza 2023 wataanza Shule kwa wakati mmoja na hakutokuwa na chaguo la pili (second selection) kutokana na kukamilika kwa madarasa 8,000.
Screenshot_20230103_053715_OGInsta%2B.jpg
 
Halmashauri ya Wilaya ya Same imekamilisha ujenzi wa jengo la huduma za Wagonjwa wa dharura lililojengwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo.

Jengo hilo lililogharimu shilingi Mil.300 limejengwa kwa fedha kutoka Serikali kuu na ni miongoni mwa majengo yanayotoa huduma za Wagonjwa wa dharura 80 yaliyojengwa katika vituo vya kutolea huduma katika maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumzia ukamilishaji wa Jengo hilo Mganga Mkuu wa Wilaya ya Same Dr. Alex Philemon amesema kuanzia mwaka 2023 wananchi wa Same na maeneo ya jirani wataanza kufaidika na huduma za dharura.

Nae Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Same Dkt. Ibrahimu Sembua amesemap Hospitali hapo awali walikua wanatoa huduma za dharura kwenye jengo la Wagonjwa wa nje ambapo huduma hii haikuwa inatolewa kwa mpangilio mzuri lakin kwa upatikanaji wa jengo hilo huduma zitakuwa za uhakika.
Screenshot_20230103_053848_OGInsta%2B.jpg
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa katika kipindi cha nusu ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2022/23 yaani Mwezi Julai 2022 hadi Desemba 2022 imefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Trilioni 12.46 ikiwa ni sawa na asilimia 99 ya lengo la makusanyo ya Shilingi Trilioni 12.48.

“Makusanyo haya ni ongezeko la Shilingi Trilioni 1.35 ikilinganishwa na kiwango cha makusanyo cha Shilingi Trilioni 11.11 kilichokusanywa kwa kipindi kama hiki kwa Mwaka wa Fedha 2021/22, ongezeko hili ni sawa na ukuaji wa makusanyo wa asilimia 12.2”

“Aidha, TRA inapenda kuutaarifu umma kuwa katika kipindi cha Desemba 2022 imefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Trilioni 2.77 kati ya lengo la kukusanya Shilingi Trilioni 2.60, makusanyo ya mwezi Desemba 2022 yana ufanisi wa asilimia 106.5 sawa na ukuaji wa asilimia 10.3 ukilinganisha na makusanyo ya mwezi Desemba 2021”

“Pamoja na makusanyo haya kuvuka lengo la mwezi Desemba 2022, ndicho kiwango cha juu zaidi kukusanywa kwa mwezi tangu kuanzishwa kwa Mamlaka mwaka 1996, tunaendelea kuwashukuru Walipakodi na wadau wetu mbalimbali kwa kujitoa kwenu katika kipindi cha nusu mwaka ambapo mwenendo wa ulipaji kodi kwa hiari na mahusiano baina ya Mamlaka na Walipakodi umeendelea kuimarika kwa kiwango cha kuridhisha”
Screenshot_20230103_054044_OGInsta%2B.jpg
 
Wakati mwili wa Papa Benedict XVI ambaye alifariki dunia Jumamosi Desemba 31, 2022 katika makazi yake huko Vatican akiwa na umri wa miaka 95 imeelezwa, maneno ya mwisho aliyotamka kabla ya kufikwa na mauti ni “Bwana ninakupenda.”

Kabla ya kifo chake, kando kulikuwa na muuguzi ambaye hafahamu lugha ya Kijerumani, katibu wake, Askofu Georg Gänswein alisema. Kwamba “Benedikit XVI kwa sauti ya chini kabisa ambayo ilieleweka alisema kwa Kiitaliano ‘Signore ti amo!’ yaani “Bwana ninakupenda.”

Ofisi ya Papa ya Holy See Press, Benedict XVI ilieleza alifariki katika makazi yake monasteri ya Mater Ecclesiae ambayo aliyachagua kama makazi yake baada ya kujiuzulu mwaka 2013.

Mwili wa kiongozi huyo mstaafu duniani wa kanisa Katoliki ambaye ni raia wa Ujerumani, utazikwa Alhamisi Januari 5, 2023 kwenye makaburi yaliyoko katika kanisa la Mtakatifu Petro, Vatican ikitanguliwa na ibada ya mazishi itakayoongozwa na Papa Francis.
Screenshot_20230103_055517_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa FIFA, Gianni Infantino amesema ataomba kila nchi duniani kuita uwanja mmoja wapo jina la Pele.
Pele alikuwa mwanasoka nguli duniani alifariki Desemba 29 na atazikwa kesho Brazil.

Screenshot_20230103_055738_OGInsta%2B.jpg
 
Papa Francisko amemteua Askofu Mkuu Angelo Accattino Balozi wa Vatican nchini Tanzania. Kabla ya uteuzi huu, Accattino alikuwa ni Balozi wa Vatican nchini Bolivia.

Askofu Mkuu, Accattino alizaliwa Julai 31, 1966, nchini Italia. Juni 25, 1994 akapadrishwa. Alianza utume wake katika masuala ya diplomasia ya Vatican, Julai 1, 1999.

Papa Francisko Septemba 12, 2017 akamteuwa kuwa Balozi wa Vatican nchini Bolivia na kumpandisha hadhi kuwa Askofu Mkuu na kuwekwa wakfu kama Askofu mkuu Novemba 25, 2017.

Screenshot_20230103_060017_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema katika siku 100 zikizopita nchi imefanikiwa kujenga madarasa ya sekondari 8, 000.

Samia amesema hayo leo Januari 2.2022 katika kurasa zake za mitandao ya kijamii huku akisisitiza kuwa hakuna mwanafunzi atakayekosa nafasi ya shule kwa uhaba wa madarasa.

"Katika siku 100 zikizopita nchi yetu imefanikiwa kujenga madarasa ya sekondari 8,000 na thamani zake nchi nzima. Tunaanza kuyatumia juma lijalo. hatua hii ya kihistoria ni ukombozi kwa wanafunzi zaidi ya 400, 000 hakuna mwananfunzi atakayekosa nafasi ya shule kwa uhaba wa madarasa," ameandika Rais Samia.

Screenshot_20230103_060123_OGInsta%2B.jpg
 
Polisi nchini Uganda wamethibitisha kumshikilia muandaaji wa tamasha lililofanyika katika maduka ya Freedom Mall yalipo jiji Kampala, usiku wa mwaka mpya na kusababisha watu 10 kupoteza maisha.

Abbey Musinguzi "Abitex" ni mtayarishaji maarufu wa matamasha ya burudani ambaye anashikiliwa, huku polisi wakiendelea na uchunguzi kuhusu mkanyagano uliotokea katika jengo la maduka la Freedom City na kusababisha vifo hivyo.

Msemaji wa polisi Fred Enanga amethibitisha idadi ya waliofariki ni 10 kati ya watu 500 waliokuwa kwenye ukumbi huo na miongoni mwa waliofariki ni watoto.

Screenshot_20230103_060230_OGInsta%2B.jpg
 
Kwa mujibu wa mtandao wa Marca ni kuwa kwenye mkataba wa Cristiano Ronaldo na Al Nassr kuna kipengele cha kimkataba ambacho kinamruhusu kutoka kwa mkopo kurejea England kukipiga kwenye klabu ya Newcastle endapo watafuzu UEFA Champions League.

Klabu hizo mbili zipo chini ya umiliki mmoja wa Saudi Arabian Public Investment Fund.
Screenshot_20230103_070938_OGInsta%2B.jpg
 
ENZO FERNANDEZ KUTUA DARAJANI
.
Mabosi wa Chelsea wamekamilisha mazungumzo na Benfica juu ya ada ya uhamisho wanatakiwa kulipa ili kuipata huduma ya kiungo wa kimataifa wa Argentina anayeichezea timu hiyo Enzo Fernandez katika dirisha hili.
.
Chelsea imeweka mezani ofa ya pauni 110 milioni kuishawishi Benfica kumwachia mshindi huyo wa tuzo ya Mchezaji Bora kijana michuano ya Kombe la Dunia 2022.

Screenshot_20230103_071109_OGInsta%2B.jpg
 
DILI LA ARSENAL, MUDRYK LIPO HIVI
.
Winga wa Shakhtar Donetsk, Mykhailo Mudryk amekubali kutua Arsenal, Hata hivyo mbali ya kufikiwa kwa makubaliano kati ya wawakilishi wa Mudryk na mabosi wa Arsenal, bado hadi sasa haijajulikana dili hilo litaigharimu Arsenal kiasi gani juu ya ada ya uhamisho wa fundi huyo mwenye umri wa miaka 21.
.
Taarifa kwa mujibu wa Fabrizio zilidai kwamba Arsenal imewasilisha ofa ya Pauni 55 milioni, lakini ilikataliwa. Ikiwa Shakhtar itakubali kufikia muafaka na Arsenal kuna uwezekano dili la fundi huyo likakamilika mapema wiki ijayo.
.
Mudryk ni mmoja kati ya wachezaji tegemeo katika kikosi cha kwanza cha Shakhtar na msimu huu amecheza mechi 24 za michuano yote, amefunga mabao 10 na kutoa asisti nane. Mkataba wake unamalizika 2026.
Screenshot_20230103_071233_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom