Makapuku Forum

Makapuku Forum

Farhan Jr

Yupo hapo Mkurugenzi wa bodi ya ubashiri Tanzania (The gaming board of Tanzania) kamwe hawezi kushiriki kwenye kitu ambacho sio cha kweli

Yupo hapo mtu kutoka Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ambao wao kisheria wanachukua 25% ya mapato ya Sports Betting, hawezi kushiriki kwenye kitu ambacho sio cha kweli

Guys hii nchi ina mifumo yake, Simba hawezi kuja kutangaza mkataba wa uongo mbele ya serikali, kamwe Simba hawawezi kusema uongo wa aina hiyo ya kuchezea NAMBA ambazo ni mapato

Huu mkataba Simba wameupata sio kwa bahati mbaya ni kutokana na kazi waliyoifanya kwa miaka minne nyuma, nani ambaye haitaki traffic ya Simba mtandaoni? Nani hataki kujihusisha na fan base ya Simba?

Trust me! Simba wanavuna leo walichokipanda miaka minne nyuma, baada ya MO Dewji kuweka pesa iliyozaa mfumo, mfumo uliozaa weledi, weledi ulioleta mafanikio ndicho kinachowalipa sasa

NI BILLION 26.18 NA IMETHIBITISHWA NA MAMLAKA, MIE NANI NIPINGE? TUISHI NAYO HII TAARIFA! GUYS HAKUNA KITU KINAFANYIKA BILA MACHO YA MAMLAKA, HAKUNA

Usikasirike ni mchakato ambao ulichukua muda, watu wakatumia muda na sasa wanavuna matunda ya muda! Beba makombe, nenda Afrika washa moto basi hizi noti zipo tu
Screenshot_20220802-155509_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom