Makapuku Forum

Makapuku Forum

Gabriel Jesus na maisha mapya jijini London, Uingereza

Ana kibarua cha kufikia na kuzidi kile walichofanya Aubemayang na Lacca kipindi chao, ana kazi ya ziada Jesus

Ataweza kufikia matarajio? Hakuwa na presha kubwa pale City, sasa hivi ana kibarua cha kuibeba Arsenal mgongoni
Screenshot_20220707-045115_OGInsta%2B.jpg
 
Harry Maguire amerejea mazoezini kwa ajili ya kujiandaa na msimu, kila kitu kipo sawa
Screenshot_20220707-045201_OGInsta%2B.jpg
 
Neymar Jr hana uhakika kama atasalia PSG, Cristiano bado anapambana kuondoka United

Miaka kadhaa nyuma walikuwa kwenye ubora wa hali ya juu sana na sasa wanamalizia burudani yao

Tunakubaliana kuwa haikuwa sahihi Jr kwenda PSG na Ronaldo kurejea United?
Screenshot_20220707-045252_OGInsta%2B.jpg
 
Moja kati ya wachezaji ambao wanatazamwa kama kioo cha mitindo, Hector Bellerin amerejea Arsenal na amevaa kitambaa chake cha Unahodha

Msimu uliopita alikuwa kwa mkopo Real Betis ya Hispania
Screenshot_20220707-045842_OGInsta%2B.jpg
 
Mwenyekiti Todd Boehly amesema wazi kuwa hatosajili mchezaji yoyote ambaye hayupo kwenye mipango ya Kocha Thomas Tuchel, ili kuunga mkono project yake anayoijenga
Screenshot_20220707-050118_OGInsta%2B.jpg
 
Majeraha yamemuweka nje Hassan Dilunga, lakini ni moja kati ya ingizo bora kwa Simba kutoka Mtibwa, tangu amejiunga nao hajawaangusha

Akirejea vyema kutoka kwenye majeraha naamini bado ni msaada mkubwa sana kwao, namtazama kama Mchezaji wa viwanja vyote
Screenshot_20220707-050245_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji599]Taarifa zinasema kuwa Wakala wa Cristiano Ronaldo, Jorge Mendes yupo nchini Hispania akijaribu kufanya mazungumzo na Barcelona ili nyota huyo ahamie kwenye klabu hiyo
Screenshot_20220707-050436_OGInsta%2B.jpg
 
Makamu wa Rais ndio Mwenyekiti wa mipango na fedha wa klabu, nitaweka mazingira wezeshi ya kupata fedha za kujenga uwanja.

Kupitia uwanja tutajenga uchumi imara wa klabu kupitia viingilio vya milangoni [gate collections]

Wanayanga tunajua wanachokipenda, ushindi uwanjani na kutwaa mataji tutaendelea kutengeneza timu za kushinda mataji.

Tutakapoimarisha timu za vijana tutapunguza gharama za usajili kwa wachezaji kutoka maeneo mengine. Timu hizi zikiwa imara tutapata wachezaji wazuri wa kuichezea Yanga senior team lakini tutapata fursa ya kuwauza kwenye vilabu vingine na Ulaya.

Timu ya wanawake isipofanya vizuri wala kushinda ubingwa msimu ujao niulizwe mimi.

- Arafat Ally Haji, Mgombea nafasi ya Makamu wa Rais Yanga.
Screenshot_20220707-050744_OGInsta%2B.jpg
 
VIPAUMBELE VYA ENG. HERSI SAID @Caamil_88 endapo atachaguliwa kuwa RAIS WA YANGA.

1. Miundombinu
- kujenga uwanja wenye uwezo wa kubeba watu 20,000 kwenye eneo la Kaunda.

2. Mabadiliko kutoka mfumo wa zamani wa uendeshaji kwenda mfumo wa kisasa wa uendeshaji

3. Kuimarisha uchumi wa klabu
  • Kuanzisha miradi
  • Kuvutia wadhamini
  • Kuvutia wawekezaji

4. Mataji
- Kuendelea kushinda mataji ambayo tumeanza kushinda msimu huu baada ya kuyapoteza kwa muda mrefu.

5. Kuimarisha timu zetu [U17, U20, Yanga Princess na Yanga SC]
- Timu za vijana zitakuwa zinasaidia kupeleka wachezaji kwenye timu ya wakubwa, kuimarisha timu ya Wanawake iwe ya ushindani na kushinda mataji

6. Ushirikiano kati ya klabu na mashabiki, washikadau n.k
Screenshot_20220707-050835_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

Huyu ni Kiungo Said Khamis Ndemla, naomba niwape kisa kimoja kuhusu Kiungo huyu na Mtibwa Sugar

Ndemla yupo Manungu kwa mkopo akitokea Simba ambapo anamalizia mkataba wake sasa na tayari amejiunga na Singida Big Stars

Ikumbukwe Ndemla alipata kadi nyekundu dhidi ya Simba na alikosa mechi mbili, dhidi ya Namungo na Yanga, lakini ngoja niwape kisa kimoja

Baada ya mechi Ndemla aliwasha gari yake binafsi na kuanza safari ya kuelekea Manungu akitokea nyumbani kwake Kigamboni, licha ya kuwa hayupo sehemu ya mchezo dhidi ya Namungo aliwaambia anaenda kuwasupport wenzake, IMAGINE

Kutokana na umbali mrefu aliingia Manungu usiku sana na kweli siku ya mechi alikuwepo uwanjani na aliwapa support wenzake japo Mtibwa alifungwa, akarejea tena Dar Es Salaam kwa usafiri wake binafsi, IMAGINE

Siku ya mechi ya Yanga alifika tena uwanjani kuwapa support wenzake na Mtibwa alipoteza tena ile mechi, rasmi Mtibwa ikaenda Playoffs dhidi ya Prisons! Timu ikitakiwa kusafiri usiku ule kuelekea Mbeya

Kumbuka Ndemla hapo amemaliza adhabu ya mechi mbili lakini hata mkataba wake wa mkopo pale Mtibwa sasa unamruhusu kutoitumikia tena timu akihitaji au akiwaambia tu kuwa hayupo tayari au angeongopa anaumwa, ila kwake ilikuwa tofauti

Alipiga simu kwa Mkewe alete baadhi ya nguo zake na viatu vyake kwenye hotel ya timu pale Kijichi na kumwambia anaelekea Mbeya na timu, wanaenda kupambana pamoja na Ndugu ili timu isalie, hakutaka kukimbia vita na kuwaacha Ndugu zake, IMAGINE! Saa tatu usiku timu iliondoka Dar kuelekea Mbeya, Ndemla akiwemo pia

Kwenye mechi ambayo Ndemla alipiga mpira mkubwa sana akihusika kwenye mabao takribani mawili na timu ilikuwa na balance sana, alitutumikia kwa wema sana Wana Morogoro

Nilimuuliza Ndemla kwanini una moyo kama huu? Kwanza ni heshima yake kwa Mtibwa, wachezaji wenzake na CEO @swabr04 ambaye anaishi nao kwa wema sana, CEO hana baya na mtu, hivyo anajiona ni sehemu ya familia na ana deni la kuibakiza timu

@mtibwaofficial inakuheshimu, MOROGORO inasema Asante, MANUNGU itakuaga kwa heshima kwenye mchezo wako wa mwisho kwenye jezi yetu pale Manungu dhidi ya Prisons
Screenshot_20220707-051043_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom