Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20211029-185050_Instagram.jpg
 
WOSIA MZITO WA GOMES KWA MKUDE
.
“Mkude namuamini na naamini katika uwezo wake na kipaji, lakini ili uweze kufikia malengo unatakiwa kutumia muda mwingi kufanya mazoezi utafika mbali zaidi ya hapa ulipo sasa, kama amenielewa na kukubaliana na kauli yangu nina imani atakuwa bora na ataisaidia Simba,” anasema Gomes na kuongeza;
.
“Suala la kucheza kwenye kikosi cha Simba bado lipo kwenye mikono yake yeye mwenyewe Mkude.Lwanga (Tadeo), Sadio (Kanoute), Mzamiru (Yassin) na Erasto (Nyoni) wote ni wazuri kwenye kiungo lakini kila moja ana staili yake ya kucheza.”
.
“Kila mchezaji nimewahi kumpa nafasi ya kucheza hii inaonyesha nilikuwa naelewa umuhimu wao kikosini, shida ni kwa Mkude ambaye sijamtumia mara nyingi hivi karibuni kwasababu hajafanya mazoezi na timu muda mrefu,” anasema na kuongeza:
.
“Hakuna mchezaji ambaye hakuwa na namba kwenye kikosi changu, ukiona mchezaji sijamtumia basi kashindwa kunishawishi mazoezini na amekosa moja ya programu zangu kuelekea mchezo husika.”
Screenshot_20211029-185627_Instagram.jpg
 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

Suala la nembo ya Mdhamini ambaye ni NBC dhidi ya Yanga wala sio gumu na kubwa kama watu wanavyolichukulia, ni suala Jepesi sana linaongeleka

Yule Twiga wa NBC ni kweli ana rangi nyekundu ila Wananchi wana utamaduni wao ambao hautaki nyekundu kwenye jezi zao! Sasa Nilitaka kujua hili linaishi vipi??

Nikamtafuta Kaka yangu mmoja yupo kwenye Kampuni ya VODACOM kutaka kujua suala Lao na Yanga waliliendesha vipi na hatimae Wananchi kutumia rangi tofauti??

Kwanza kabisa yeye akaniambia hili suala ni mazungumzo kati ya Mdhamini na timu, hapa TFF na TPLB wao Kazi yao kusimamia kanuni ila wataheshimu makubaliano kati ya timu husika na Kampuni (Mutual agreements)

Hapo tu nikajua hii kumbe ni issue ya NBC na Wananchi kukaa round table kisha TPLB na TFF wao wataheshimu kile walichokubaliana kuhusu rangi, ila mpaka sasa TPLB wanasimama na makubaliano ya kimkataba kati yao na Mdhamini wao NBC

Turudi kwenye hoja ya msingi, Je VODACOM na Yanga walitatua vipi ilihali tunajua Voda wanatumia kidoa chekundu?? Kaka yangu akaanza kunipa Elimu kuhusu hilo

Akasema kuna kitu kinaitwa BRAND GUIDELINES! Hakuna Kampuni yenye rangi moja pekee, mfano Vodacom wana Nyekundu, Nyeusi na Nyeupe! Hizo ndio rangi zao ambazo zinaweza kutumika kwa mazingira tofauti

Akaniambia wala hapakuwa na shida kati ya Yanga na Vodacom kwakuwa GUIDELINES zipo na Yanga kwa tamaduni zao wakasema wataenda na doa jeusi kwenye jezi yao! Na hapo hapo akaniambia hadhani Kama kuna utata wowote kati ya Yanga na NBC, ni suala jepesi la kureview GUIDELINES tu

NBC wanaweza kuwa na rangi zaidi ya moja, watakaa mezani na kureview kwakuwa zipo rangi nyingi ili kuepusha mazingira Kama haya

Nami nikaenda beyond kwa issue kama ya PSG ambao kulinda tu utamaduni wao wa Mashabiki kuchoma moto uwanjani, basi wanalipa faini ya Dola elfu 30 kila msimu, kulinda tu utamaduni wao wa moto! Ina mantiki kibiashara na kiutamaduni

Jambo jepesi tu
Screenshot_20211029-185805_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom