Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20211102-074246_Opera%20Mini.jpg
 
[emoji3578][emoji3578] Kelvin Rabson

Moja ya mchezo bora sana usiku wa leo pale Italy...Atalanta wakionesha uwezo mkubwa sana[emoji91]... lakini alikuwa ni Cristiano alie simamisha furaha yao.

Man United wanakuwa wazi sana bila mpira, kuanzia eneo la kiungo mpaka ulinzi, hawaweki presha kwa mpinzani, hawaweki presha kwenye mpira....yaani mpaka unajiuliza ma boss wa United wanaangalia mpira na wanaona haya matatizo.
.
Atalanta kila wakihamisha mpira kutoka upande mmoja kwenda mwingine inakuwa matatizo kwa United...walitumia mabeki watatu sawa na Man United lakini pressing yao ilikuwa bora sana, hawakuwaruhusu wachezaji wa United kuchezea mpira mda mrefu.
.
Zapata...Ilićić....Paśaliç walifanya mikimbio sahihi na hatari nyuma ya safu ya kiungo ya United...tafuta nafasi, pasi kwa haraka..tanua uwanja zaidi...shinda mipira ya pili [emoji460]baina ya safu ya kiungo na ulinzi ya United kunao nafasi hiyo ndio waliotumia.
.
Man United bado wanao makosa mengi hasa wakati wa kuzuia Maguire asee unadhani amekuja bure...one vs one anapitwa bado anafanya uzembe kwenye kushinda mipira ya pili...hili litazidi kuwagarimu sana United....Baily ametuokoa sana.[emoji119]
.
NOTE:[emoji3578]Cristiano Ronaldo....Mr Uefa Champions League [emoji119] mechi 4 za UEFA zote kafunga....kaisaidia United wasipoteze poimts zote Form is temporary but class is permanent [emoji847]
.
Daah United itatuuwa kwa presha sasa[emoji23]
.
FT: Atalanta 2-2 Man United.
Screenshot_20211103-040920_Instagram.jpg
 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

Kwakuwa Chuo kimefungua na Profesa yupo busy na Module plus orientation! Simu yake Leo haikuwa ndefu sana

Prof anasema kwanza kuhusu penati! Bila ya usaidizi wa VAR ni ngumu kumshutumu Mwamuzi, kibinadamu sio rahisi kuona tukio lile

Prof anasema presha ya kwanza ni kuwa Yanga wanasaka bao, presha ya pili ni kelele za Mashabiki na presha ya tatu ni akili ya mpira ya wachezaji wa Yanga

Prof anasema, wachezaji walianza kushinikiza maamuzi, na mmoja aliudaka kabisa mpira! That’s football Kama tunakumbuka hii ndio mbinu ya Barcelona siku zote, kumpa presha Mwamuzi! Ijapo haikuwa penati

Prof amependa sana namna Charles Mkwasa aliingia kimbinu Leo, namna amecheza na False 9 Pius Buswita ili kuivunja ile press ya Yanga, walipress na walikuwa bora! Mkwasa kafanya homework vyema kuliko Makocha wote mpaka sasa kwenye Ligi

Leo hakuwepo Khalid Aucho, ila alikuwepo Mukoko Tonombe! Hakuna utofauti sana ila tu Mukoko anaenjoy kumaliza box hadi box na faida yake ni kuzikata nyavu! Hata mechi ilipoisha alikaa na Mwalimu wake kuongea

Kuhusu kadi Nyekundu ya Ruvu! Prof anasema Fiston Mayele alikuwa anaelekea langoni, beki wa Ruvu alikuwa anamaliza mstari, last man kacheza faulo ya hatari, ni Clear penalty haina nongwa

Kuna namna ya kumthamini upya Feisal Salum, mkiweza basi mpeni heshma yake Mwigulu Nchemba! Mpeni tu heshma hata Kinafki, aliona miaka minne mbele kwa Yanga ya Leo

Nilikusikia Farhan ukisema kitu kuhusu FORM na CLASS! Upo sahihi lakini kuna muda Kiwango kinapaswa kuzingatiwa! Kwani ulipewa nafasi Clouds kwa kiwango au Daraja? Wangetazama tu Daraja basi Vijana msingepata nafasi

Yanga ni bora sana hivi sasa! PROFESA[emoji1621]
 
Kutoka Bungeni Dodoma leo kwenye kikao cha kwanza cha mkutano wa tano wa Bunge la 12, Naibu Waziri wa Nishati Steven Byabato amejibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa na Wabunge akiwemo Mbunge wa Tabasamu aliyetaka ifanyike namna kumaliza tatizo la Sengerema kukatika umeme mara thelathini au mara 10 kwa siku na kutaka Sengerema iunganishwe kwenye line ya umeme ya Geita ili waepuke kukatikiwa umeme kama ilivyo sasa.
Screenshot_20211103-042236_Instagram.jpg
 
Polisi Tanga wanawashikilia Watu watatu kati ya sita wanaotuhumiwa kufukua kaburi la Mtu mwenye ualbino ambaye alikua Daktari Hospitali ya Rufaa Muhimbili Heri Shehe Kijangwa kisha kuukata mguu wake wa kulia na kuondoka nao kwa imani kwamba kitendo hicho kitawapa utajiri.

RPC Tanga Safia Jongo ameiambia Ayo TV ———> "Tukio limetokea Kijiji cha Tanda, Kata ya Bumbuli Tanga ambapo Marehemu Herry (45) aliyezikwa July 4 2020 kaburi lake lilikutwa limefukuliwa, ikabidi kaburi lifukuliwe lote ili kuona kama mwili upo…. wakakuta upo lakini mguu wa kulia umekatwa, hapo ndio uchunguzi ukaanza mara moja ndipo wakakamatwa Watu hawa, mguu huo umekutwa umefukiwa kwenye shamba la Mtuhumiwa wa tatu"
Screenshot_20211103-042535_Instagram.jpg
 
Serikali imetangaza bei mpya za mafuta ya diesel kuanzia kesho ambapo bei ya diesel imeshuka kwa shilingi 18 katika bandari ya Dar es salaam kutoka 2261 mwezi October na kufikia 2043 mwezi huu huku bei ya mafuta ya pertol ikibaki kama ilivyo, Kaimu Mkurugenzi wa EWURA Godfrey Chibulunje ameeleza zaidi.
Screenshot_20211103-043550_Instagram.jpg
 
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Said Mtanda amekanusha taarifa iliyodai kwamba amewataka Watumishi wa Serikali wasiochanja wajielezee kwanini hawajafanya.

"Taarifa hiyo imepotoshwa na takwimu zilizotolewa hapa sio sahihi naomba ieleweke kuwa Wilaya ya Moshi tumechanja Manispaa Watu 18,000 na Moshi DC Watu 12,000, nilichosisitiza ni Watumishi tunaosimamia zoezi hili kwanza sisi wenyewe kuonesha mfano kwa kuchanja, inafahamika kitaifa kuwa chanjo ni hiari, nimesisitiza ni hiari lakini ina ulazima"
Screenshot_20211103-043752_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom