Makapuku Forum

“Leo ni mara yangu ya kwanza kuwa Mgeni Rasmi kwenye Baraza la Eid hivyo nawashukuru sana kwa nafasi hii, BAKWATA kwenye salamu zenu mumeahidi kunipa ushirikiano Mimi na Serikali, nawashukuru sana”———Rais Samia Suluhu kwenye Baraza la Eid leo

“Nawapongeza Waislamu wote nchini kwa kumaliza salama mfungo wa Ramadhan, nguzo ya nne ya Uislamu, hongereni sana, ni imani yangu kwamba Mungu amezikubali funga zetu na kutusamehe madhambi yetu yote, ucha Mungu usiishie jana baada ya Mwezi kuandama tuuendeleze”———Rais Samia
 
“Watumishi wa Serikali nawasihi wafanye kazi na wajiepushe na rushwa, Wafanyabishara wasikwepe kodi, niwahakikishie Watanzania Serikali itakuwa imara kudumisha amani na usalama , Wananchi mtoe ushirikiano kwa Serikali jukumu la kutunza amani ni letu sote”———Rais Samia kwenye Baraza la Eid
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…