Makapuku Forum

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kesho Ijumaa May 7, 2021 anatarajia kuzungumza na Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam katika mkutano utakaofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam na kuhusisha Wazee takribani 900.
 
Huko Handeni Tanga sasa hivi kuna misiba mitatu ambapo vifo vya Watu wote hao watatu vimetokana na Tembo ambao walivamia makazi ya Watu na kuwashambulia, ni majonzi yaliyoambatana na hofu kwani Watu wanaogopa hata kutembea.

Hii imefanya Mkuu wa Wilaya ya Handeni, pia Mbunge wa Handeni Reuben Kagilwa na Viongozi wa Vijiji kupaza sauti zao kuomba msaada wa Askari wa Wanyama pori kuweka kambi Handeni ili kusaidia kuepusha vifo vingine visitokee.

Viongozi hawa wa Handeni amewataka Wananchi kutokukimbilia kupiga picha za selfie na Tembo hao wanapowaona kwani tabia hiyo imeripotiwa "Wananchi wengine wanakimbilia kupiga selfie na Tembo naomba wasifanye hivyo, tena wajiweke mbali kabisa... bado Tembo hawa hawajaondoka kwenye hizi kata na Watu wanashindwa kufanya kazi"
 
Kuanzia May 1 2021 kumekua na mjadala mrefu unaohusisha pande mbili ambazo ni upande wa Wasanii na upande wa BASATA (Baraza la Sanaa Tanzania) ni mjadala baada ya BASATA kuanza kuitumia sheria ya kupitia nyimbo zote mpya za Wasanii kabla hazijapelekwa kwenye Radio au TV, Watu mbalimbali wametoa maoni yao na haya ni maoni ya Mwimbaji T.I.D

T.I.D ameandika ———> “hapa kuna tatizo, kila Mtu ana chuki yake na BASATA kwa kuwa hawafanyi kazi yao... kwa kifupi hawasaidii chochote sisi ambao ndio tumeufikisha huu mziki hapa na kwa ujumla sanaa nzima ya Bongofleva, kwenye miziki ambayo kimaadili haitakiwi kupromote uchafu kui-edit naona hapo wameanza kufanya kazi labda hawajatoa ufafanuzi wa jinsi gani wataweza kumudu kwa ukubwa"

"Wakilinyoosha hilo naona sasa ndo wakati wa kuyazungumzia mengine apart from that Wasanii mlikuwa wapi siku zote wengine tunapiga kelele kila kukicha hadi tunajiita BASATA tunataka kuchukua maamuzi mikononi? kwenye hili humu naona kuna utashi sababu nani kasema hivi mnafata mkumbo wakati wenye mashairi yenye MATUSI wenyewe hawajaongea chochote, BASATA fanya kazi umeanza vizuri" ——— TID
 
Hizi ni picha mbalimbali zikiwaonesha Wazee wa Mkoa wa Dar es salaam takribani 900 wakiwa tayari wamewasili kwenye ukumbi wa Mlimani City kwa ajili ya Mkutano wa pamoja wa Wazee hao na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…