Makapuku Forum

Nawaombea tu Tff walalamike Fifa yawakute kama ya Chad
 
PICHA: Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, (CAG) Charles Kichere akifuatilia shughuli za Bunge leo Dodoma.

Ripoti Kuu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu Ukaguzi wa Taarifa za Fedha za Serikali Kuu kwa Mwaka wa Fedha ulioishia June 30, 2020 imewasilishwa Bungeni hii leo.
 
Tume ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa Sudan Kusini UNMISS imesema inapanga kupunguza idadi ya wanajeshi wake kwa asilimia saba mwaka huu. Mkuu wa tume hiyo David Shearer amesema uamuzi huo unatokana na kupungua kwa machafuko nchini humo kufuatia kusainiwa kwa mkataba wa amani mnamo mwaka 2018.

Shearer ameongeza kusema hatua hiyo pia inatokena na wanajeshi wa Umoja wa Mataifa kuondoka kwenye kambi ambazo raia walikuwa wameomba ulinzi wakati wa vita vya miaka sita vya wenyewe kwa wenyewe, huku wakikabidhi udhibiti wa kambi hizo kwa serikali ya Juba.
 
Rais Paul Kagame wa Rwanda leo ameipongeza ripoti mpya ya Ufaransa inayoainisha jukumu la Ufaransa katika mauaji ya halaiki ya Rwanda ya mwaka 1994. Akizungumza mbele ya viongozi mashuhuri mjini Kigali, siku ya kwanza ya wiki ya kumbukumbu ya mauaji hayo, Kagame amesema ni jambo zuri kusonga mbele kwa kufahamu kile kilichotokea, ikiwa ni miaka 27 tangu mauaji hayo yaliyoushutua ulimwengu.

Kagame amesisitiza tafsiri ya serikali yake ya matokeo ya uchunguzi wa tume ya Ufaransa kwamba rais wa Ufaransa wakati huo Francois Mitterand alifahamu mauaji ya halaiki ya Watutsi yalikuwa yakipangwa na washirika wake nchini Rwanda, lakini akaendelea kuwaunga mkono kwa sababu aliamini yalikuwa muhimu kwa nafasi ya Ufaransa katika siasa za kikanda.

Hii ni mara ya kwanza Kagame kuizungumzia ripoti ya mauaji ya halaiki ya Ufaransa iliyotolewa mwezi Machi. Watu takriban laki nane waliuliwa na wauaji wa kihutu wakiwemo Watutsi na Wahutu waliojaribu kuwatetea, katika kipindi cha siku 100 za mauaji hayo.
 
“Idadi ya laini za simu imeongezeka kutoka Mil 39 hadi Mil 48.6, idadi ya Watumiaji wa mitandao ya simu imeongezeka kutoka Mil 9 hadi Mil 27 na gharama za kupiga simu za mkononi zimepungua kutoka Tsh. 274 kwa dakika kwa mwaka 2015 hadi Tsh.70 kwa dakika mwaka 2020”———Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba, Bungeni Dodoma leo
 
“Mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka minne ya utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2016/17–2020/21) ni kuzalishwa kwa
ajira 12,773,126, ambapo ajira za moja kwa moja ni 11,891,772 na zisizo za moja kwa moja ni 881,354”———Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba Bungeni Dodoma leo
 
“Shabaha za Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26 ni pamoja na Kuchochea Maendeleo ya Watu; eneo hili linajumuisha utekelezaji wa miradi ambayo inajikita katika kuboresha maisha ya Watu ikiwemo: elimu na mafunzo kwa ujumla; afya na ustawi wa jamii, kinga ya jamii, huduma za maji na usafi wa mazingira, mipango miji, nyumba na maendeleo ya makazi na athari dhidi ya Mabadiliko ya Tabia Nchi”———Waziri wa Fedha na Mipango, Dr. Mwigulu Nchemba Bungeni Dodoma leo
 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo , Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Abbas pamoja na Wakurugenzi wa Wizara wamemkaribisha Naibu Waziri Pauline Gekul baada ya kuwasili Makao Makuu ya Wizara hiyo na kuanza kazi rasmi baada ya Rais Samia Suluhu kumhamishia akitokea Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Gekul baada ya kuwasili alisaini kwenye kitabu cha Wageni katika Ofisi yake pia kutembelea Ofisi ya Waziri na baadae alikutana na Viongozi wa Wizara na kufanya nao mazungumzo ya ndani.View attachment 1746855
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Aprili 8, 2021 ameongoza Mkutano wa Kazi wa Baraza la Mawaziri ambao pia ulihudhuriwa na Makatibu Wakuu, baadhi ya Makamishina na Wakuu wa Taasisi, Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Hazina Dodoma.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…