Makapuku Forum

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema amesikitishwa na kitendo cha mahindi ya Uganda kuzuiwa kuingizwa kwenye baadhi ya Nchi za Afrika Mashariki na kusema hiyo sio ishara nzuri kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki huku akisema Uganda haitolipiza kisasi bali itatumia njia nzuri ya mazungumzo ili kulinda Umoja wa Afrika Mashariki.

“Nilisikia kuna baadhi ya Wabunge wanazungumza kuhusu kulipiza kisasi (kwenye ishu ya mahindi ya Uganda kuzuiliwa kwenye baadhi ya Nchi za Afrika Mashariki), siungi mkono visasi, tuwe wavumilivu na tulimalize hili vizuri kwa maslahi mapana ya Jumuiya ya Afrika Mashariki”-MUSEVENI

“Kwakuwa Afrika Mashariki ina Nchi tofauti wale Wazee wa Fursa na Wanyonyaji lazima tu watakuwepo, kuna Wanyonyaji kwenye baadhi ya Nchi wanasema mahindi ya Uganda yatavuruga biashara zao, tunahitaji mazungumzo, muingiliano na ushirikiano sio tu kupiga kelele tupu”- MUSEVENI
 
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema bado hajaruhusu Wataalamu wa Afya wampe chanjo ya Corona na wala Mkewe Janeth Museveni hajachanjwa hiyo chanjo ya Corona kwakuwa anataka chanjo hiyo waanze kupewa Watu ambao wanaugua Corona ambao anaamini wana uhitaji zaidi.

“Sababu nyingine inayonifanya nisikubali kwa sasa kupewa chanjo ya Corona ni kwasababu Mimi ni mwangalifu na nina ulinzi mkubwa kutoka kwenye mfumo wa kiusalama, pia naendelea kuangalia ni chanjo ipi ni nzuri zaidi kuitumia”- MUSEVENI


Hiki chuma kiboko anawatoa chambo wananchi wake
 
Juzi kwenye moja ya Habari kubwa za Kitaifa tulizokua nazo ni kukamilika kwa asilimia 100 kwa Stesheni ya Dar es salaam ya reli ya kisasa (SGR) ambapo sasa baada ya ujenzi kukamilika kwa 100%, samani za kisasa na zimeanza kuwekwa ndani yake kama meza, viti na makochi tayari kabisa kwa kuanza kazi.
 
UNAAMBIWA: Kahawa ambayo inaongoza kwa kuuzwa bei kubwa duniani ni hii iitwayo Black Ivory kutoka Thailand ambayo kikombe kimoja kinauzwa kwa USD 100 (Tsh. laki mbili na elfu 30), kinachoipa upekee zaidi ni kwakuwa inatengenezwa kutoka kwenye maharage ambayo yanapatikana kwenye kinyesi cha tembo, tembo hao hupewa maharage kisha yale ambayo yanatoka yakiwa hayajasigika tumboni huuzwa kwa hadi USD 1100 kwa Kilo (Tsh.Mil 2.5) na kutengeneza kahawa hiyo.
 
UNAAMBIWA: Nchini India kuna Kijiji ambacho kuna Watu wanaishi bila kuweka milango kwenye nyumba zao na hata kwenye maduka, Bank, Shule na biashara nyingine kote hakufungwi na hakuna anayeibiwa, Kijiji kinaitwa Shani Shingnapur na wanaacha bila kufunga kwa kuamini kuwa mungu wanayemuabudu anawalinda na majanga, Je kwa uzoefu wako ni sehemu gani Tanzania kuna usalama kiasi kwamba hakuna haja ya milango?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…