Makapuku Forum

Wanamitindo wenye ulemavu wa ngozi wameshiriki katika shindano la kuiwakilisha Kenya katika mashindano makubwa ya Afrika mashariki ya kumtafuta Mr & Miss Albino.

Mashindano haya yamenuiliwa ubadili mtazamo wa jamii dhidi ya walemavu hawa.
 
Wanajeshi wakiwa wamemkamata Mbunge Alfred Yekatom maafuru Rambo kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR),

aliyefyatua risasi hewani akiwa ndani ya ukumbi wa bunge baada ya kuibuka kwa mvutano. Wabunge walikuwa wakivutana wakati wakijiandaa kupiga kura kuchagua spika wa Bunge.
 
Gari la kubeba watalii linalotumia nishati ya umeme wa jua (e-car) limezinduliwa rasmi katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Gari hilo linalomilikiwa na Mount Kilimanjaro Safari Club (MKSC) halipigi kelele hivyo kutosumbua wanyama, pia ni rafiki kwa mazingira kwani halitoa moshi.
 
Kampuni ya IPP imetangaza kuanza ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza simu (smartphone) zitakazokaa na chaji kwa wiki moja na pia zitafaa kuchajiwa kwa umeme wa jua.

Uwekezaji huo unakadiriwa kugharimu TZS 11bn, na uzalishaji utaanza ndani ya miezi 3 ijayo, ambapo utatoa ajira 2,000.

 
Meya wa Manispaa ya Iringa (CHADEMA), Alex Kimbe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi kujitafakari kwa kuomba radhi, ili kurejesha imani yake kwa watumishi wa mkoa huo. Amesema, kama Waziri (Selemani Jafo) ameomba radhi kwa niaba yake, na yeye ni lazima aombe radhi.
 
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza Novemba 15, 2018 kuwa ndio mwisho wa kupokea maombi ya uanachama wa CCM na kupewa dhamana ya uwakilishi kwa Wabunge na Madiwani kutoka vyama vingine.
 
Opportunities ndio hizi vijna tuzichangamkieni.
 
Wewe peke ndio ulikuwa haujui,,wenzio mbona tunafahamu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…