Makapuku Forum

Kwa afya njema ya kinywa chako, unashauriwa kupiga mswaki mara mbili kwa siku. Wakati unafanya hivyo, usiwe na haraka. Chukua muda wa kutosha kusugua meno yako yote kwa ukamilifu huku ukihakikisha kila kinachopaswa kuondolewa kimefikiwa.

Kulingana na umri, mazingira au hali ya afya, unashauriwa kutumia mswaki sahihi utakaokufaa pamoja na dawa ya meno iliyo na madini ya floridi. Mswaki mzuri ni ule ambao visafishio vyake havikuumizi na unaokaa vizuri kinywan

Watoto wapewe mswaki unaofanana na umri wao ili kufanikisha hili. Wale wadogo wasimamiwe ili kuzingatia namna ya upigaji na kuepuka kutomeza dawa ya meno ambayo haipaswi kumezwa.

Kanuni ya tatu ni kujizoeza njia nzuri za kupiga mswaki. Unapaswa kuushika mswaki wako kwa namna ambayo visafishio (brashi) vyake vitalenga kwenye makutano ya meno na ufizi.
 
Unachotakiwa kufanya ni kusafisha meno yako kwa mwendo mfupi wa kwenda mbele na nyuma, juu na chini. Kumbuka kusafisha nje, ndani na sehemu za kutafunia. Halikadhalika usisahau kusafisha ulimi kwa kutumia mswaki wakati ukipiga mswaki.

Ni muhimu kuutunza mswaki katika hali ya usafi kila baada ya kuutumia. Mara zote safisha mswaki wako kwa maji safi umalizapo kuutumia. Unapouhifadhi, usimamishe ili ukauke mpaka utakapoutumia tena.


Kama una miswaki kadhaa na yote unaitunza mahali pamoja, tenganisha huu uliotumia sasa na hiyo mingine ili kuzuia maambukizi ya bakteria. Weka mswaki wako mahali penye hewa ya kutosha vinginevyo huweza kuchochea ukuaji wa bakteria na fangasi kwenye mswaki wako ambao wanaweza kukusababishia maambukizi ya mgonjwa ya kinywa au mwili kwa ujumla.
 
Kanuni ya tano na mwisho kwa leo ni kutambua wakati sahihi wa kubadilisha mswaki wako. Mswaki hupoteza ubora wake kadri uutumiavyo hivyo kustahili kubadilishwa. Kila mtengenezaji anapaswa kuandika mswaki unaoununua unastahili kutumika kwa muda gani…ingawa hufanya hivyo ila wengi hatuzingatii kusoma maelekezo yaliyomo. Lakini ipo kanuni ya jumla. Unatakiwa kuhakikisha unatumia mswaki mpya kila baada ya miezi matatu mpaka minne. Ni vyema kama utafanya hivyo chini ya muda huo au pale utakapoona umeanza kuharibika.
 
Flosi

Flosi ni uzi maalumu uliotengenezwa ili kusafisha katikati ya meno ambamo brashi za mswaki haziwezi kufika na kutekeleza lengo hilo. Hivyo, kuflosi ni kusafisha maeneo yaliyo kati ya jino na jino ambayo hayawezi kufikiwa na mswaki.
 
Kutokana na ugumu wa kupiga mswaki maeneno ya kati jino na jino, inashauriwa kusafisha mara moja kwa siku ili kuimarisha usafi kamili wa kinywa na kujihakikishia siha njema.


Zipo kanuni au taratibu za kuzingatia. Kwanza unashauriwa kukata uzi wa kufanyia flosi wa kutosha. Kwa mtu mzima, inapendekezwa uwe na urefu walau sentimita 45.
 
Kisha zungusha sehemu kubwa ya uzi huo kwenye kidole cha kati cha mkono mmoja na fanya vivyo hivyo kwenye kidole cha kati cha mkono mwingine.


Flosi hufanywa taratibu. Unashauriwa kuelekeza na kuupitisha uzi kati ya meno ukitumia na kusugua. Sugua meno na sio ufizi. Fanya hivyo kutoka jino moja kwenda jingine kwa zamu.
 
Flosi jino moja kwa wakati mmoja. Jiridhishe kwa ukamilifu ulioufanya kwenye jino la kwanza kabla hujahamia la pili. Flosi taratibu kwa kusugua kwenye jino kwa kwenda juu na kushuka chini.


Habari njema ni kwamba hujachelewa kwani ukifanya kazi yako vizuri, haijalishi umeanza lini kupiga mswaki au kuflosi matokeo ni sawasawa. Utakuwa na afya njema na utajiamini popote utakapokuwa.
 
Auntie zako wananisumbua huku,,,kila siku wananiuliza aunt anakuja ln
ntakuja jumapili niwasalimie
watafurahi sana
waulize wanataka zawadi gani niwaletee
Unadhan hata wana mambo mengi,,mmoja hapa anataka popcon mwingine chocolate
Sawa kumbe ntajtahid niwaletee

ABJ twende tukawasalimu akina anti
Tena kama ABJ toka amewaona ni muda mrefu,,,wanamuuliza yule aunt anapenda kuja na ice cream yupo wapi
ngoja nimshawishi nije nae kwa kweli
Ninge kumbe na wewe una watoto wa insta kama tumosa yaani watoto wa kuchorwa
 
Ameeeeeeen
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…