Makapuku Forum

Makapuku Forum

LAZIMA HUWA UNAFANYA MOJA YA VITU HIVI UNAPOHISI HAKUNA ANAYEKUONA!

1.Kunusa baadhi ya maeneo ya mwili wako kuona kama yanatoa harufu!, mara nyingine unajikuna kisha unapeleka mkono puani kuona ni harufu gani utaskia.

2. Kuigiza kama unafanyiwa interview. Unajiuliza maswali kadhaa na kujijibu kwa kujiamin huku unatabasamu kana kwamba kuna mtu anakuona.

3. Kutoa uchafu puani kwa kutumia kidole kwa dakika kadhaa, na mtu akitokea ghafla, unajidai unakuna shavu!

4.Kula haraka haraka kwa kificho (tunda, kitafunwa nk) ofisini, nyuma ya mlango nk na kujifuta mdomo ili asigundue mtu!

5. Kutengeneza Sura mbalimbali mbele ya kioo na kuangalia unaonekanaje!
 
6 Kutoa Hewa chafu kwa sauti (Farting Loud). Hii hairuhusiwi kwenye jamii yetu!

7.Kutoa Haja ndogo wakati wa kuoga

8 Kufanya baadhi ya vitu kwa kutumia miguu badala ya mikono! Kufunga mlango au Kuokota vitu kwa kutumia vidole vya mguuni

9. Kula paketi nzima ya chakula Fulani ambayo pengine ungekula kwa siku kadhaa taratibu
 
KILA MTU HUFANYA UJINGA HUU IKIWEMO WEWE HASA UKIWA UMECHOKA! (KUMI)

1.Kuingia kwenye chumba halafu ghafla unasahau uliingia kufanya nini, ukiamua kutoka tu, unakumbuka!

2.Kuangalia saa na baada ya kuondoa macho tu kwenye saa, unasahau ilikuwa saa ngapi! Na inakubidi uangalie tena!

3.Kukubaliana na mtu kwa kutikisa kichwa kumbe hata hujasikia kakuambia nini. Unaombea tu asije akawa amekuuliza swali

4.Unatembea katikati ya watu mara ghafla unagundua umekosea njia, Unajidai umesahau kitu au kuangalia simu yako na kuanza kurudi kwa kasi!


5.Unabishana kichwani kwako mwenyewe mpaka unapata hasira, baadae unagundua ni mawazo tu na kujiona mjinga!
 
6. Betri za rimoti yako zimekwisha unaamua kuminya batani za rimoti kwa nguvu zaidi ukihisi itasaidia!

7.Unaambiwa kitu Fulani ni cha moto, unaamua kugusa na unaungua kweli!

8. Unajikwaa au kujigonga sehemu na unaanza kutukana ukihisi sehemu hiyo inakusikia

9 Kujiangalia kwenye kioo cha jengo na kusahau kuwa kuna watu ndani ya jengo na wanakuagalia


10. Unabisha kwamba hujalala (huko usingizini) na unasikia kila kinachoongelewa, kumbe kila mtu ameshakushtukia!
 
WAZIJUA LUGHA 10 ZENYE WAZUGUMZAJI WENGI ZAIDI DUNIANI?

1.Mandarian (Jamii ya Ki china). Ni lugha mama ya zaidi ya watu milioni 900.

2.Kiingereza. Lugha mama ya watu 335 milioni, na ni lugha ya pili kwa watu milioni 500 duniani kote

3.Kihisponiola.(Spanish) inawazungumzaji milioni 400 duniani kote

4.Kihindi. kinazungumzwa na watu milioni 295 dunia nzima

5.Kiarabu.kinawazungumzaji milioni 280 dunia nzima


6.Kibengali. Ni lugha inayozungumzwa na watu milioni 240 Duniani.

7.Kireno. Wazungumzaji 204 duniani

8.Kirusi. Wazungumzaji 160 milioni.

9.kijapani. Wazungumzaji 127 milioni.


10.Kifaransa.Wazungumzaji 75 milioni. (Lugha mama). Na zaidi ya wazungumzaji milioni mia moja (Lugha ya pili)
 
REKODI KUMI ZA KIJINGA ZAIDI ZILIZOPO KWENYE KITABU CHA REKODI CHA “GUINNESS”

1.Vijiko Vingi zaidi kwenye mwili wa Binadamu.
Disemba 28 mwaka 2013, Etibar Elchiyev aliweka vijiko 53 mwilini mwake akiwa amesimama wima na kuvunja rekodi yake mwenyewe!













2.Mtu aliyeolewa mara nyingi zaidi!
Linda Lou Taylor wa jimbo la Indiana nchini marekani, anashikilia rekodi ya kuolewa mara nyingi zaidi akiwa ameolewa mara 23!. Ana miaka 69 kwa sasa na amekuwa akisisitiza kutaka kuolewa kwani hana mpenzi kwa zaidi ya miaka kumi sasa!









3.Watu wengi zaidi Kupiga Mswaki kwa wakati mmoja.
Katika mji wa Manila Nchini Philippines, wanafunzi 10,800 walikusanyika pamoja kupiga mswaki na kutema kwenye kikombe kwa wakati mmoja!












4.Mbwa aliyebeba glass na kutembea umbali Mrefu zaidi.
Usishangae! Wanyama nao wamo. Mmbwa mmoja wa Australia anashikilia rekodi ya kutembea hatua kumi mbele na hatua kumi nyuma akiwa na glass ya maji kichwani!










5.Nywele Ndefu zaidi za Masikioni.
Agosti 26 mwaka 2007, Anthony Victor wa Maduri India, aliweka rekodi ya dunia kuwa binadamu mwenye nywele ndefu zaidi za masikioni zikiwa zimefikia nchi 7!
 
6.Kupigwa Teke Sehemu za siri (mwanaume) kwa spidi ya kilometa 40 kwa saa.
Kirby Roy aliweka rekodi hii alipokubali kupigwa teke zito na mwanamieleka Justice Smith kwa kasi ya kilometa 40 kwa saa teke hilo likiwa na nguvu ya kusogeza kilo mia tano!













7. Choo chenye Kasi zaidi Duniani
Unapoteza muda mwingi kukaa chooni? Colin Furze alitengeneza choo cha kukaa chenye uwezo wa kutembea kwa kasi ya kilometa 100 kwa saa chenye uwezo wa kuflashi!







8.Kuongezeka Uzito kwa kasi zaidi.
Rekodi hii imewekwa na Donna Simpson wa New Jersey, USA. Alifikisha kilo 273.5 kutoka kilo tisini tu! Zoezi hilo alilifanya kwa kipindi cha miaka miwili (2) tu! Alikuwa akitumia zaidi ya shilingi milioni moja kwa wiki kwa kula tu!









9.Mayai Mengi zaidi kupasuliwa kwa kichwa kwa wakati mmoja.
Ashrita Furman anashikilia rekodi ya kupasua mayai 80 kwa kichwa kwa wakati mmoja!











10.Chapati Kubwa Zaidi kutengenezwa!

October 8 2010, katika nchi ya Uturuki, wapishi zaidi ya 50 walikusanyika kwa pamoja na kutengeneza chapatti ya mayai yenye uzito wa tani 6 (Uzito wa gari kubwa). Chapatti hiyo ilichanganywa mafuta lita mia nne (400), na Mayai zaidi ya laki moja (100,000)
 
MALEZI HAYA NDIO YAMETENGENEZA VIONGOZI TULIONAO SASA! (UTAWALAUMU?)

Kama umezaliwa kabla ya mwaka 1990 utakubaliana na mimi kwa aina hii ya malezi uliyolelewa nayo!

1.Mzazi ndiye Mungu, yaani hata kama umefundishwa kwamba anga ni la bluu, mzazi akikuambia anga lina rangi ya njano inabidi ukubali!
(matokeo yake viongozi hawakotayari kukosolewa)

2. Nyumbani ni kwa ajili ya yeyote ilimradi tu awe ni ndugu, ndugu yeyote anaweza kuja kukaa kwa muda wowote hata kama alifukuzwa kwao hukuna haja ya kuwa na wasiwasi nae maadam ni ndugu yetu!
(matokeo yake, mgeni toka nje akija, No problem! Ni rafiki zetu sana hawa, mpe ardhi)

3.Mdogo kwenye familia ndiye atakaesingiziwa kafanya uharibifu wowote nyumbani, mpaka atakapokuwa na uwezo wa kujitetea!
(Matokeo yake wenye vyeo wakitaka “kula” wanatumia mgongo wa watu Fulani wa chini ambao hawana sauti)
 
Sababu Zingine

4. Mkubwa kwenye familia ndiye atakaeadhibiwa na kupewa lawama kwa kile mdogo alichofanya mdogo anaachwa.

5. Wazazi watakuita ukiwa nje unacheza, au unasoma ili wakutume uwachukulie kitu kilichopo mita chache kutoka walipokaa.

6. Sahau Suala la kusifiwa, Ukipata B darasani utaambiwa kwani aliyepata A ana vichwa vingapi?

7. Mtoto hafundishwi elimu ya uhusiano anapobalehe. Yeyote anayeonekana nae huitwa rafiki na mzazi hana muda wa kufuatilia. Unachoambiwa ni “Usituletee aibu nyumbani”

8. Mtoto wa kike hafundishwi chochote kuhusu maisha na baba! Mpaka awepo mama au shangazi

9. Kuna Kinywaji Kabatini? Au Kuna kuku anachinjwa? Oooh basi ujue leo kuna mgeni anakuja!


10. Lazima usomee kozi aliyosomea Yule msomi wa kijijini kwenu. Hii ni amri imetoka kwa baba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom