Makapuku Forum

Mjukuu wa Malkia wa Uingereza William alikutana na rais John Pombe Magufuli wa Tanzania katika Ikulu ya Dar es Salaam ambapo wawili hao walijadili mikakati ya kupambana na biashara haramu ya bidhaa zitokanazo na wanyama wa porini.

Mwanamfalme William anaendesha kampeini ya endwildlifecrime kutokomeza uwindaji haramu wa wanyama pori
 
Mv Nyerere:

Kivuko kilichozama na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 220 katika ziwa Victoria kimepinduliwa.

Shughuli hiyo ya kukinyanyua ilikuwa ikiendeshwa na jeshi ikiongozwa na mkuu wa jeshi Venance Mabeyo
 
Maelfu ya wafuasi wa madhehebu ya Orthodox wamekusanyika katika bustani ya Meskel mjini Addis Ababa Ethiopia kusherehekea siku ambayo msalaba uliotumika kumsulubisha Yesu Kristo ulipopatikana.
 
Mkataba wa ujenzi wa Daraja la Juu la Eng. Patrick Mfugale ulisainiwa Oktoba 15, 2015 nchini Japan.

Jiwe la msingi liliwekwa na Rais Dkt JP Magufuli Aprili 16, 2016.
Lilifunguliwa kwa ajili ya majaribio Septemba 15, 2018 na kuzinduliwa leo.
Ujenzi umegharimu takribani TZS 102bn.
 
Daktari Fredrik Mashili kutoka Muhimbili amesema, watu wengi nchini wanaotumia dawa za kupunguza unene, hutumia dawa za kuwafanya waharishe na hivyo kupoteza maji mengi mwili.

Hivyo, watu hao huwa hawapungui, bali mwili husinyaa kwa kupoteza maji jambo ambalo ni hatari kiafya.

Vibongeeee mpo
 
Rais wa Bolivia, Evo Morales aishambulia Marekani na kusema, haina lengo la kulinda demokrasia kwani imekuwa ikifadhili mapinduzi ya kijeshi, imeitishia ICC, isingejitoa Baraza la Haki za Binadamu, isingejitoa katika makubaliano ya Paris na isingehamishia ubalozi wake Jerusalem.
 
Mabilionea wawili kutoka Tanzania, Aunali na Sajjad Rajabali wamekuwa wawekezaji wenye hisa nyingi zaidi katika kampuni kubwa ya mawasiliano ya Safaricom ya nchini Kenya.

Wawili hao wanamiliki hisa milioni 21.1 zenye thamani ya TZS milioni 521.
 
Baada ya muda wa kawaida wa masomo, shule moja mjini Kigali nchini Rwanda huwatenga wavulana na wasichana ambapo, wasichana hujifunza kuhusu uwekezaji, kujitegemea kifedha, afya ya uzazi na familia, huku wavulana wakijifunza jinsi ya kuripoti ukatili na pia kuwaheshimu wana
 
Waathirika wa mafuriko Kaskazini mwa Ghana wameanza kuumwa tumbo baada ya kudaiwa kutumia mafuta ya kupikia yaliyoisha muda wa matumizi, waliyopewa na Makamu wa Rais, Mahamudu Bawumia.

Mafuta hayo yalitakiwa kumwagwa, lakini baada ya mafuriko, yalipelekwa kwa waathirika hao.
 
Bodaboda ya mfano iliyofungwa tela iliyotengenezwa na Shirika la Mzinga lililopo chini ya JWTZ kufuatia agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola aliyetaka bodaboda kufungwa tela ili kupunguza ajali.

Taasisi za serikali (VETA, SIDO, TBS) zimejidhatiti kutekeleza agizo hilo.

 
Serikali ya Benin imepitisha sheria ambayo inamtaka kila anayetaka kugombea urais nchini humo kulipa TZS bilioni 1 ($450,000).

Vyama vya siasa pia vitatakiwa kulipa kiasi hicho hicho kuweza kushiriki uchaguzi wa wabunge.

Uchaguzi nchini humo unatarajiwa kufanyika mwaka 2020.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…