Makapuku Forum

Makapuku Forum

GUANTANAMO:

Gereza Lenye Wafungwa Walioshindikana.

Mwanzoni mwa miaka ya 1960 alikuwepo msanii wa kilatini aliyejulikana kwa jina la Jose Marti.

Umaarufu wake uliongezeka kwenye nchi za kilatini mwaka 1963 baada ya kuachia wimbo wa “Guantanamera” (Hutamkwa Guantanamo kwa Kispanyola) ambao ulikuwa ‘hit’ kipindi hicho kiasi cha kurudiwa na wasanii wengine akiwemo Julio Iglesias (Baba yake Enrique Iglesias).

Guantanamera ni wimbo wa kilatini (kutokea Cuba) wenye maudhui yanayomsifia mwanamke mrembo kutokea katika ardhi ya Guantanamo.

Kwa kipindi hicho inawezekana dhana hii ikawa inaakisi uhalisia wa wanawake waliopo huko lakini hali imebadilika na kuonekana tofauti baada ya kujengwa kwa gereza linalowakutanisha magaidi kutoka kila pembe ya dunia.


Aghalabu umeshawahi kusikia kuna Gereza linaitwa Guantanamo, lakini pia inawezekana ukawa umesikia stori mbalimbali zinazohusu gereza hili nyingine zikiwa ni za kuogopesha.



Screenshot_20180927-082322.jpeg
 
GUANTANAMO

Ni mkoa uliopo katika kisiwa cha Cuba, mkoa huu upo kusini- mashariki. Wamarekani walichukua eneo hili kinguvu mwaka 1903 na kulimiki wao, kwa muda wote huo lilikuwa ni kambi ya kijeshi.

Wanajeshi wa Marekani walikuwa wakitumia eneo hili kujifunza shabaha na kuweka silaha nzito mpaka mwaka 2002 kwenye utawala wa George Bush alipoamua kujenga gereza ambalo linawahifadhi watuhumiwa wenye makossa ya kigaidi kutoka nchi za kiarabu na mashariki ya mbali.


Pamoja na jitihada mbalimbali zilizofanywa na aliekuwa rais wa Cuba Bwana Fidel Castro kuomba Marekani iondoe gereza hilo kwenye eneo lao, Marekani wameamua kutumia mabavu kubaki eneo hilo, lakini pia wanaamini kuwa endapo watuhumiwa wa kigaidi wakatoroka basi nchi ya kwanza kuathirika ni Cuba na si Marekani.

Kila Mwaka Serikali ya Marekani hutoa dola 4000 kwa Cuba kama malipo ya kuwepo eneo hilo lakini Cuba inagoma kuzipokea


Kitu unachopaswa ufahamu ni kwamba, Washukiwa wanaopelekwa Guantanamo ni watuhumiwa tu. Hakuna mahakama yoyote inayosikiliza kesi zao lakini pia muda unaotumika kuwaweka kizuizini watuhumiwa ni siri kati ya jeshi na serikali.

Screenshot_20180927-082304.jpeg
 
GUANTANAMO

Wizara ya ulinzi ndio huratibu shughuli zote za kukamatwa kwa watuhumiwa na ukamataji hufanywa kwa siri pia haikujulikana idadi ya washukiwa ambao wamekamatwa mpaka pale Association Press walipoandika barua ndipo wakajulishwa kuwa jumla ya wafungwa 779 wameshatiwa kizuizini.


Baada ya Shambulio la Septemba 11, utawala wa Marekani iliwaita wapiganaji wa aina hiyo kuwa magaidi hatari Zaidi na hawastahili kuchanganyika na wengine. Januari 20 2002 watuhumiwa 20 kutokea Afghanistan na Pakistan waliwekwa kizuizini, mpaka kufikia 2005 zaidi ya watuhumiwa 700 walikuwa kizuizini kwenye gereza hilo la kijeshi. Siku hadi Siku watuhumiwa huaga dunia na wengine huachiwa huru ambapo sasa wamebaki takriban watuhumiwa 60 katika kituo hicho.

Kituo cha Guantanamo kina jumla ya madaktari na wauguzi 100 na wanajeshi 2,000. Walinzi katika eneo hilo wanasema kuwa wamepewa amri ya kuwafanyia utu wafungwa lakini stori za wafungwa wenyewe ni tofauti na maneno ya walinzi.


Screenshot_20180927-082340.jpeg
 
GUANTANAMO


Kijografia Guantanamo ni eneo ambalo wanajeshi wengi wanalipenda kwani huduma zote za kijamii zipo. Lakini hiyo ipo tofauti kwa wafungwa wanaopelekwa huko, Adhabu, Mateso na Kazi ngumu ni sehemu ya maisha yao.


Mohamedou Ould Slahi ni miongoni mwa washukiwa wa mwanzo kabisa kuingia katika gereza hilo lakini pia ni mfungwa aliyekaa kipindi kirefu kifungoni (kwa miaka 14). Aliingia mwaka 2002 na kuachiwa huru tarehe 17 Sptember 2016. Alikamatwa nchini Mauritania na kisha kupelekwa Jordan na baadae Guantanamo.


Shtaka lililokuwa likimkabili Slahi ni la kujiunga na Kikundi Cha Al Qaeda nchini Pakistani ambapo kati ya mwaka 1991/1992 alisafiri hadi nchini humo na kuwa mwanafunzi wa kikundi cha Al Qaeda. Kupitia Kitabu alichoandika mara baada ya kuachiwa "Prison Diary" Slahi anasema alikuwa akipata mateso takatifu ndani ya gereza.


Nilikuwa nafungwa pingu miguuni na mikononi, nafungwa kitambaa machoni muda wote,nasimama kwa muda mrefu lakini pia nadhalilishwa mbele ya wanawake kwa kuachwa uchi nyakati nyingine nasafirishwa mbali na eneo la gereza na kuamriwa ninywe maji yenye chmvi


Kijana Jihad Diyab nae pia ni miongoni mwa wafungwa walioonja joto ya Gereza hilo ambapo kwa sasa anatembelea magongo kwa maisha yake yote ikiwa ni kitu cha kumkumbusha mateso aliyoyavumilia kwa miaka 12, miezi 8 na siku 7 kama mfungwa katika gereza la Guantanamo Bay, mahali ambapo jeshi la Marekani linawaweka washukiwa wa makosa ya kivita kwa muda usiofahamika na bila kufunguliwa mashtaka.
Screenshot_20180927-083324.jpeg
 
TUOMBE:

Mtakatifu,Mtakatifu,Mtakatifu ..Bwana Mungu wa Majeshi Asante kwa siku hii ya leo.

Tunaomba Toba Baba kwa makosa yote uturehemu Ee Baba.
Tunawasamehe wote waliotukosea.
Tusaidie tuzidi kukupenda,kukuheshimu na kukutumikia.

Asante kwa ajili ya watoto wako wa kike na kiume,Asante kwa ajili ya uponyaji wa Mwili na Roho...Tunalihimidi jina lako Takatifu na Sifa,heshima,Shukurani ni kwako Ee Baba Mungu mkuu
Endelea kutupigania Mfalme wa Amani maana tunakutegemea wewe tu.

Endelea kutuponya,kutufariji,kutubariki katika kila eneo.Hesabu hatua zetu na vinywa vyetu vijazwe sifa zako daima.
Bariki kuingia na kutoka kwetu Damu yako Takatifu Yesu Kristo inene mema.
Roho Mtakatifu kaa nasi tufundishe katika kila hatua

.Asante Baba
Wasaidie watoto na wajukuu walioanza mitihani leo wakumbushe wasaidie wawe washindi.Asante maana utatenda sawa na mapenzi yako naomba nikiamini katika jina la Yesu Kristo Amen.

SIKU NJEMA YA AMANI NA USHINDI DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO ITUFUNIKE
 
Kwangu bila chai asubuh siku inavurugika.
Uwiiii mm mmojawapo wa kudharau kifungua kinywa nikinywa ujue naumwa tena tumbo mm ni juice au soda
Ee hapo anakua keshapata kipozeo kingine
Akibeba mimba ni yake kwahiyo akizaa pia dume haonekani
poa mamie
Numbii mpenzi ebu punguza kidogo si unajua cha uvivu mm naonaje ndefu kama mwanzo
Moja ila kwa kuangalia unaweza dhani anazo mbili
Ana jinsia mbili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom