Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: Kazi Ni Afya

....nilipokuwa mtoto (sheria ya mtoto 2009 inasema yeyote chini ya miaka 18 ni mtoto) nilikuwa nikiona mtu anaongea peke yake akili yangu iliniaminisha mtu yule ni punguani au kichaa na ikifikia wakati nikamuona anacheka basi najua kabisa moja haiingii mbili haikai. Nilikosea sana, maana sasa nimekuwa mtu mzima na nikimuona mtu anaongea peke yake basi najitahidi kumpa nafasi ya kujua kuwa ana uhuru wa kuongea peke yake ila asipige makelele maana yatanidistub nikiwa nawaza yangu.

ukikosa kazi ya kufanya kuna vitu kadhaa vinakuwa vinakupata, magonjwa yasiyokoma, msongo, mfadhaiko na kukosa mapenzi. Ukikosa ajira na kama una akili timamu unaweza kuamua kujiingiza kwenye vitendo ambavyo tu si kwamba vinapingana na sheria bali imani za dini tunazoziamini.

Kwanini ninaandika koramu hii ya kutafasiri unavyoweza, sababu kubwa ni kuwa kila mmoja anatafairi masuala tofauti kwa njia tofauti. Sita ukiigeuza inakuwa tisa na akili ikikupeleka kwenye 69 kitandani basi una uhuru wa kutafasiri hivyo.

sisemi kuwa wenye kazi/ajira hawana msongo, la, namaanisha ukiwa 'bize' msongo ni ngumu kuupata na ukiwa nao tiba yake haichukui muda kusahihisha tatizo.

Lengo langu hapa ni wewe kutafasiri unavyoweza maana kama serikali haiweki misingi sahihi ya kuhakikisha wananchi sisi tunakuwa na kazi za kutushughulisha, itegemee kuingia gharama kubwa za kutibu msongo na mfadhaiko wa wananchi wengi na kupata kundi la wananchi wenye hasira zisizojulikana kutokana na kulose betting na zile fursa wanazofanywa fursa eti kupata pesa za mkato.

a57e09715145cfe2ff8f5b25333c916c.jpg
 
Muziki: Nini Maneno, Burudika

Leo ni Ijumaa, wikend ndo imeanza fyi.
Nikutakie wikend njema, nipo nafanya yangu, nawe fanya yako. shoo imekolea hapa Mwembeni pub yaana DJ na MC wameng'atana wanaupendeza muziki ukiacha hawa wacheza shoo wanaoifanya bia ya moto kuwa ya baridi. Baadaye nitaomba namba ya mmoja ambaye nishaamka kumtuza si zaidi ya mara nne, atakakuwa keshanikariri

 
Muziki: Nini Maneno, Burudika

Leo ni Ijumaa, wikend ndo imeanza fyi.
Nikutakie wikend njema, nipo nafanya yangu, nawe fanya yako. shoo imekolea hapa Mwembeni pub yaana DJ na MC wameng'atana wanaupendeza muziki ukiacha hawa wacheza shoo wanaoifanya bia ya moto kuwa ya baridi. Baadaye nitaomba namba ya mmoja ambaye nishaamka kumtuza si zaidi ya mara nne, atakakuwa keshanikariri


Mambo ya mwambao haya
 
Muziki: Nini Maneno, Burudika

Leo ni Ijumaa, wikend ndo imeanza fyi.
Nikutakie wikend njema, nipo nafanya yangu, nawe fanya yako. shoo imekolea hapa Mwembeni pub yaana DJ na MC wameng'atana wanaupendeza muziki ukiacha hawa wacheza shoo wanaoifanya bia ya moto kuwa ya baridi. Baadaye nitaomba namba ya mmoja ambaye nishaamka kumtuza si zaidi ya mara nne, atakakuwa keshanikariri


asante Obe kwa muziki ubarikiwe usiku mwema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom