Makapuku Forum

1 Nalimngoja Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu.
Zaburi 40 :1

2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.
Zaburi 40 :2

3 Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumaini Bwana
Zaburi 40 :3

4 Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake, Wala hakuwaelekea wenye kiburi, Wala hao wanaogeukia uongo.
Zaburi 40 :4

5 Ee Bwana, Mungu wangu, umefanya kwa wingi Miujiza yako na mawazo yako kwetu; Hakuna awezaye kufananishwa nawe; Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, Ni mengi sana hayahesabiki.
Zaburi 40 :5

6 Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Zaburi 40 :6

7 Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, (Katika gombo la chuo nimeandikiwa,)
Zaburi 40 :7

8 Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.
Zaburi 40 :8
 
Amen

Ubarikiwe dadake na mimi
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…