Makapuku Forum

USA watu wabaya Sana
 
Daaaaah kweliii hili dili likitiki tutaamini kuna watu wanacheza na faranga....


Mshambuliaji wa Barcelona Neymar, 25, amekubali dau la Paris Saint-Germain, baada ya klabu hiyo ya Ufaransa kuwa tayari kutoa pauni milioni 195. (Esporte)
 
Tottenham watalazimika kumlipa kiungo Moussa Sissoko, 27, ili aondoke, licha ya kutoa pauni milioni 30 kumsajili mwaka jana tu. (Daily Mail)
 
Arsenal watajaribu kutaka kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzima, 29, iwapo Alexis Sanchez, 28, ataondoka Emirates. (Don Balon)
 
Wakala wa Alexis Sanchez amewapa Real Madrid nafasi ya kumsajili mchezaji huyo wa Arsenal, lakini Real wamekataa kumchukua mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona. (OK Diario)
 
Ivan Perisic, 28, amesafiri na klabu yake kwenda China baada ya Manchester United kushindwa kufikia makubaliano ya ada ya uhamisho na Inter Milan. (Telegraph)
 
Manchester United wameacha kumfuatilia kiungo Eric Dier, 23,wa Tottenham baada ya klabu hiyo ya kaskazini mwa London kukataa kumuuza mchezaji huyo. (Mirror)
 
Manchester United wamekuwa na mazungumzo ya awali na Paris Saint-Germain kuhusu kutaka kumsajili Marco Verratti. United wapo tayari kupambana na Barcelona kutaka kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa Italy. (TuttoMercatoWeb)
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…