Makao makuu ya wilaya huchaguliwa au kupangwa na nani??

DMussa

JF-Expert Member
Sep 24, 2007
1,310
296
Wana JF mimi natatizwa na suala zima la uteuzi wa makao makuu ya wilaya. Kuna wilaya moja mpya ya Rorya ambayo iko mkoa wa Mara tatizo ni kwamba kuna mabishano na upinzani mkubwa juu ya eneo lipi liwe ndio makao makuu ya hiyo wilaya. Suali langu kubwa hapa ni kwamba nani haswa ndio mhusika mkuu katika kuteua/kuchagua au kuamua eneo kuwa makao makuu ya wilaya? Naomba ufafanuzi katika hili wananchi wenzangu maana huu uteuzi/uchaguzi naskia umeanza kuchukua sura ya RUSHWA......
 
Wana JF mimi natatizwa na suala zima la uteuzi wa makao makuu ya wilaya. Kuna wilaya moja mpya ya Rorya ambayo iko mkoa wa Mara tatizo ni kwamba kuna mabishano na upinzani mkubwa juu ya eneo lipi liwe ndio makao makuu ya hiyo wilaya. Suali langu kubwa hapa ni kwamba nani haswa ndio mhusika mkuu katika kuteua/kuchagua au kuamua eneo kuwa makao makuu ya wilaya? Naomba ufafanuzi katika hili wananchi wenzangu maana huu uteuzi/uchaguzi naskia umeanza kuchukua sura ya RUSHWA......

Wenye dhamana ya kuchagua makao makuu ya wilaya ni wananchi wenye wilaya husika, kupitia kwa wawakilishi wao ambao ni madiwani. Sidhani kama serikali kuu ina maamuzi katika hili. Baraza la madiwani nadhani ndio wanaohusika na kuamua mahali ambapo kutakuwa na makao makuu ya wilaya, kwa kuangalia idadi ya watu katika eneo husika, ukaribu wa kusambaza huduma kwa tarafa na kata zote za wilaya husika (kwamba angalau makao makuu yawe katikati ya wilaya, kama inawezekana). Huwa kunatokea mara nyingi kwamba wanasiasa (hasa wabunge) hutaka kulazimisha makao makuu yawe mahali fulani, kwa matakwa yao, bila kuangalia vigezo vya kuweka makao makuu mahali fulani.
Hili suala la Rorya kule Mara linashabihiana kabisa vurugu zilizotokea mkoani Iringa ambapo kulikuwa na mgawanyiko wa wananchi na viongozi wao kuhusu makao makuu ya wilaya mpya ya Kilolo, ambayo ilimegwa kutoka wilaya ya Iringa Vijijini!
 
Back
Top Bottom