Makanisa ya kiroho mnatupeleka wapi?

maandiko yameshawasema watu kama nyie,mwenyezi Mungu kupitia manabii na mitume alisema watu wake wanaangamia kwa kukosa maarifa na kutokusoma maandiko,magazeti ya udaku na umbea mnasoma sana ila kuchukua muda kujisomea neno la Mungu hampati huo muda mnasubiri kusomewa na wachungaji feki wenye kuchambua mafungu ktk biblia yenye kuwanaufaisha na kuwasononesha na kuwafurahisha ila ukweli hawausemi na mtaangamia kweli,na mtawanaufaisha kweli nami nasema acha wawapige,acha wawafilisi na hasa wanawake amabao wao wanaenda kusali sbb ya kupata miujiza,muda unapotea wakizinduka hawana kitu,umri umeenda na hakuna walichopata.Mjini shule,vijana wengi wasomi kwa sasa hawana kazi hvy kimbilio ni kufungua makanisa,kutafuta miujiza basi
 
Ndio nitasaidia maskini lakini siyo kipaumbele changu katika kumtolea Mungu,nitatoa kwenye kazi ya Mungu kwa nguvu zangu zote kwanza kisha wengine watafuatia huko,maskini siyo nafasi ya kwanza.
Nani kakudanganya kuwa MUNGU anahitaji pesa ili kazi yake ifanyike? Sadaka zinazotolewa makanisani zinatumika na hao Wachungaji katika kujilimbikizia mali. MUNGU hana shida na pesa wala haitaji pesa ili kazi yake ifanyike. Pesa ni kwa ajili ya matumizi yetu sisi wanadamu. Hata YESU alisema wazi kabisa, "sitaki sadaka nataka rehema". MATHAYO 9:13

Mkuu Conspiracy theorist rudia tena kusoma maandiko vizuri utaona kuwa dini ya kweli ni kuwasaidia maskini na yatima na wajane, soma YAKOBO 1:27 imeandikwa hivi; "dini iliyo safi isiyo na taka mbele za MUNGU BABA ni hii, kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao na kujilinda na dunia pasipo na mawaa".

Pia soma MATHAYO 25:31-40, hapo utaona wale watakaokaribishwa kwenye Ufalme wa MUNGU ni wale ambao walikuwa wakitoa pesa zao au mali zao kwa ajili ya wale wasiojiweza. Usijidanganye kabisa kusema eti maskini siyo kipaumbele, kumbuka maneno ya YESU kuhusu UPENDO, na upendo ni kuwajali wengine kama vile unavyoijali nafsi yako mwenyewe!

Kutoa Sadaka kanisani ni muhimu, lakini muhimu zaidi na zaidi ni kuwa na huruma na upendo wa dhati kwa masikini na wasiojiweza kwa kuwasaidia zaidi. Ni bora mara mia kumpa masikini au yatima chakula na mavazi kuliko kutoa sadaka kanisani.
 
Hapo nilicho gundua wewe unazungumzia majengo mazur na sio kanisa zur

Nnacho faham Mimi kanisa zur Ni lile lenye kumcha Mungu katika misingi ya amli 10 tu nasio habar cha Tass
 
Umenchekesha sana yani umli uwo ujui hata tofauti ya sadaka na mchango Duh
 
Sifa kuu ya muumini siyo kutoa sadaka bali ni kuzishika Amri za MUNGU na imani ya YESU KRISTO. YESU KRISTO alisema hivi; "enendeni mkajifunze maana ya maneno haya, sitaki sadaka nataka rehema".
Ukiwa na Rehema lazima tu Sadaka utatoa Mungu Fundi sana unajua kama watu humu tungekuwa tuna reema wala watu wasingekuwa wanabishana hapa ukiwa na reema utajua tu kwamba Shukrani inaumuim
 
Naona humu jf kila mmoja kwenye promo ya kanisa lake,msikiti e.t.c
 

Sina haja ya kukujibu kwasababu kiwango cha ujinga ulioandika hapo hakina mipaka,hivyo nakupuuza tuu,ndipo heshima unayostahili.
 
Ukitoka hapo unasema kanisa katoliki wezi wakati ukiumwa unaenda kutibiwa kwenye hospital zao
Kwani unatibiwa bure....hata wasingejenga hospital ningeenda kutibiwa Kwa Ummy mwananyamala....
 

Mrs. Official, kwenda kanisani ni utashi na imani yako kwa kadri ya imani yako .Kama imani na utashi haupo, hakuna anayeweza kukupeleka. Kama vile unaweza kwenda mtoni na usioge... Kama huhitaji kuoga hakuna anayeweza kukulazimisha.. Unaweza kwenda kanisani, usikubaliane na lolote na ukawa mpasha josho viti na vumbi, hiyo inaweza kukufaa kabisa .

Na endapo unaona haifai, unaacha kwenda hapo. Kama bado unahitaji kwenda hapo, basi kuna kitu unaona kipo... Huwezi kuwa na keki na kuila papo hapo?
 
Sina haja ya kukujibu kwasababu kiwango cha ujinga ulioandika hapo hakina mipaka,hivyo nakupuuza tuu,ndipo heshima unayostahili.
Nilichokiandika siyo maneno yangu binafsi, nimekitoa kwenye BIBLIA na kama ni ujinga basi kwako wewe inaonekana NENO la MUNGU ni ujinga usiokuwa na mipaka. Wewe ni chumvi iliyoharibika, na chumvi ikiharibika hata ikitiwa nini haiwezi kufaa tena bali kutupwa na kukanyagwa na watu.
 

Ukweli ndio huo,kama hautaki endelea kujidanganya.

Yesu alipokua hapa duniani alifanya vitu vikuu vitano(5).1 alihubiri,2.alifundisha,3.alitoa pepo ,4.aliponya wagonjwa na 5. alifanya miujiza.

Kanisa lolote lisilofanya hayo mambo matano hata kama likiwa kubwa kiasi gani,kanisa hilo limekufa.Na watu wake wanakua wamekufa kiroho.

Mengi ya hayo makanisa uliyoyataja hapo ni mafu.Mengine uliyoandika hapo sina haja ya kujibu coz naona ni ujinga tuu utatoka taratibu taratibu kadiri unavyojitahidi kujua
 
KWANI TUNATIBIWA BURE? KWANI SHULE ZAO TUNASOMA BURE? KWA TAARIFA YAKO VITEGA UCHUMI VYAO TUNAJENGA SISI THEN TUNALIPISHWA SISI TENA KWA BEI KUBWA ZAIDI BILA KUJALI MICHANGO YETU. TUMIA KICHWA CHAKO VZURI KUFIKIRI
Wewe sio mkatoliki ndo maana sitokujibu swali lako
 

Hamna neno la Mungu hapo,umechukua maandiko na kutafsiri kutokana na akili yako isiyo na nuru na kuliita eti NENO la Mungu,kawadanganye wengine huko,nyie ndio manabii wa uwongo.popote pale ukisikia au kusoma kuhusu nabii wa uongo ujue ni wewe,hivyo unabidi utubu ili uweze kuondokana na hizo roho zidanganyazo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…