R-K-O
JF-Expert Member
- Jun 27, 2023
- 482
- 2,138
Kitu kisipowekewa juhudi ya kurekebishwa huwa ni suala muda tu kinabomoka, usipoziba nyufa ukuta utabokoka
Nimewataja wanaume maana wengi wamebarikiwa uwezo mkubwa wa kutafakari, kwa wanawake ni dhaifu sana kwenye imani, ni ngumu kukuta mwanaume atoe hata elf 3 ya maji wanayonadi ni ya miujiza ila wanawake wapo tayari kutoa hata Milioni, Huyo mchungaji wanakonunua maji anajulikana ni mhuni ila bado watanunua, ni rahisi sana kuchezea akili za wanawake (elewa neno akili, usianze kufananisha na zile za kukariri darasani kupata divishen 1).
Nayaongea haya nami nikiwa moja wapo, Kanisani sijaenda mwaka, ila bado kila siku ni lazima nisali na mara kadhaa napitia Biblia huku nikitia juhudu zaidi kuepukana na dhambi, Kwakweli nilichobakiwa nacho ni imani ila kwenda kanisani labda iwe mwaka mpya tu, imeisha hio !
Ukikemea wanakwambia acha kuhukumu wewe sio Mungu dini sio kigezo cha kukupeleka mbinguni muhimu ni imani yako, Nami nawaambia Mungu alishaweka sheria zake wazi za kutupa muongozo, kama tuna imani nae kwanini tukae kimya maovu na dhambi zinapofanywa na wenzetu katika imani moja ?
MAVAZI
Hakuna cha Waroma, Wasabato, Waluteri, walokole, mashahidi wa Jehova yani wooote wameliunga, Tena kuna hao walikuwa ni mwiko kuchonga nywele ila leo hii hadi wachungaji wanachonga.
Hapo zamani kabla ya miaka ya 2000 nakumbuka binti akiingia kanisani kavaa sketi inayovuka magoti kwenda juu, sketi ndefu yenye mpasuko, gauni linalochoresha, suruali, n.k. huyu alitolewa nje kabisa ama kuvalishwa kanga, Leo hii ni jambo la kawaida kabisa wanawake kuingia kanisani na magauni yanayowachoresha makalio na hips, wengine huingia na suruali zinawachoresha hadi mapaja.
Wanawake wamepotoshana kwamba Mungu anaangalia roho haangalii mavazi, Wachungaji nao wapo kimya , Hebu angalia hii picha kweli ni hapahapa Tz mtu katoka kanisani huyu na kanisa limemruhusu aingie,
KUANZISHA MAKANISA YA HOVYO
Kina George Devie wa Arusha wanaweka mashindano ya umisi kwa mabinti waliovaa nusu uchi wanapita mbele sehemu ya kuhubiria ,n.k. Kondoo waliopotea wanaotaka kutafuta njia wanaenda kupotezwa zaidi na wachungaji hawa.
Leo hii hata kina Masanja wana makanisa yao ya kikristo, anahubiri huku kavaa mlegezo anajitetea eti kanisa ni free ufanye chochote,
KUKALIA KIMYA MAMBO YA USHOGA / USAGAJI
Hadi Papa amekuwa ni mtu wa kuwasapoti mashoga na wasagaji, maana hakamei ! Ni kama vile Papa hili suala kalipa baraka zote. Mara utasikia anasema hawana kosa, muwakaribishe makanisani, DUH !! kuna makanisa yanafungisha ndoa za jinsia moja,
Huu usodoma na ugomora tunapoona haukemewi ni sawa na kuuhalalisha, Nao mashoga wamepata jeuri wanatembea vifua mbele siku hizi kwamba hata Papa yupo upande wao,
SHERIA ZA KANISANI KUTOFATWA
Ni kawaida kukuta mvulana kanyoa kiduku tena cha rasta anapewa komnio.
Makanisa kama Lutheren KKKT wamebadili sheria kuruhusu wanawake hata waliopo kwenye mzunguko wanahubiri
Nimewataja wanaume maana wengi wamebarikiwa uwezo mkubwa wa kutafakari, kwa wanawake ni dhaifu sana kwenye imani, ni ngumu kukuta mwanaume atoe hata elf 3 ya maji wanayonadi ni ya miujiza ila wanawake wapo tayari kutoa hata Milioni, Huyo mchungaji wanakonunua maji anajulikana ni mhuni ila bado watanunua, ni rahisi sana kuchezea akili za wanawake (elewa neno akili, usianze kufananisha na zile za kukariri darasani kupata divishen 1).
Nayaongea haya nami nikiwa moja wapo, Kanisani sijaenda mwaka, ila bado kila siku ni lazima nisali na mara kadhaa napitia Biblia huku nikitia juhudu zaidi kuepukana na dhambi, Kwakweli nilichobakiwa nacho ni imani ila kwenda kanisani labda iwe mwaka mpya tu, imeisha hio !
Ukikemea wanakwambia acha kuhukumu wewe sio Mungu dini sio kigezo cha kukupeleka mbinguni muhimu ni imani yako, Nami nawaambia Mungu alishaweka sheria zake wazi za kutupa muongozo, kama tuna imani nae kwanini tukae kimya maovu na dhambi zinapofanywa na wenzetu katika imani moja ?
MAVAZI
Hakuna cha Waroma, Wasabato, Waluteri, walokole, mashahidi wa Jehova yani wooote wameliunga, Tena kuna hao walikuwa ni mwiko kuchonga nywele ila leo hii hadi wachungaji wanachonga.
Hapo zamani kabla ya miaka ya 2000 nakumbuka binti akiingia kanisani kavaa sketi inayovuka magoti kwenda juu, sketi ndefu yenye mpasuko, gauni linalochoresha, suruali, n.k. huyu alitolewa nje kabisa ama kuvalishwa kanga, Leo hii ni jambo la kawaida kabisa wanawake kuingia kanisani na magauni yanayowachoresha makalio na hips, wengine huingia na suruali zinawachoresha hadi mapaja.
Wanawake wamepotoshana kwamba Mungu anaangalia roho haangalii mavazi, Wachungaji nao wapo kimya , Hebu angalia hii picha kweli ni hapahapa Tz mtu katoka kanisani huyu na kanisa limemruhusu aingie,
KUANZISHA MAKANISA YA HOVYO
Kina George Devie wa Arusha wanaweka mashindano ya umisi kwa mabinti waliovaa nusu uchi wanapita mbele sehemu ya kuhubiria ,n.k. Kondoo waliopotea wanaotaka kutafuta njia wanaenda kupotezwa zaidi na wachungaji hawa.
Leo hii hata kina Masanja wana makanisa yao ya kikristo, anahubiri huku kavaa mlegezo anajitetea eti kanisa ni free ufanye chochote,
KUKALIA KIMYA MAMBO YA USHOGA / USAGAJI
Hadi Papa amekuwa ni mtu wa kuwasapoti mashoga na wasagaji, maana hakamei ! Ni kama vile Papa hili suala kalipa baraka zote. Mara utasikia anasema hawana kosa, muwakaribishe makanisani, DUH !! kuna makanisa yanafungisha ndoa za jinsia moja,
Huu usodoma na ugomora tunapoona haukemewi ni sawa na kuuhalalisha, Nao mashoga wamepata jeuri wanatembea vifua mbele siku hizi kwamba hata Papa yupo upande wao,
SHERIA ZA KANISANI KUTOFATWA
Ni kawaida kukuta mvulana kanyoa kiduku tena cha rasta anapewa komnio.
Makanisa kama Lutheren KKKT wamebadili sheria kuruhusu wanawake hata waliopo kwenye mzunguko wanahubiri