Makanisa kuwekewa Ulinzi

Makanisa kuwekewa Ulinzi

Status
Not open for further replies.

Kakende

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2012
Posts
2,741
Reaction score
1,233
Kuna taarifa chini ya kapeti kuwa kuanzia JUMAPILI wiki hii makanisa yote hasa ya Arusha yataanza kulindwa wakati wa ibada kama ilivyo Kenya. Polisi watakuwa na kazi kubwa maana makanisa ni Mengi ARUSHA
 
Hata wakiweka mpaka ulinzi wa farasi hautasaidia labda mbwa wa kutegua mabom
 
Kuna taarifa chini ya kapeti kuwa kuanzia JUMAPILI wiki hii makanisa yote hasa ya Arusha yataanza kulindwa wakati wa ibada kama ilivyo Kenya. Polisi watakuwa na kazi kubwa maana makanisa ni Mengi ARUSHA

Huu ni utumiaji mkubwa wa rasilimali za taifa....najiulizaga sijui watu wanafikiria kwakutumia nini......wakianza kuyalinda makanisa then kesho GULIO likishambuliwa wanatuambia Magulio yote yataanza lindwa na polisi???
 
Huu ni utumiaji mkubwa wa rasilimali za taifa....najiulizaga sijui watu wanafikiria kwakutumia nini......wakianza kuyalinda makanisa then kesho GULIO likishambuliwa wanatuambia Magulio yote yataanza lindwa na polisi???
hivi wewe una akili timamu?
 
hivi wewe una akili timamu?

............mnaosoma vinjwa vya habari mtawajua tu.......nahisi wewe ni moja wao....huna na wala hutakaa uwe na credibility ya ku..question uwezo wa kichwa changu.........kwani likija swala la utashi na kufikiri ni vema ukawa unayatembelea maandishi mara kwa mara.....unaweza ukakomaa kidogo kiakili
 
hivi wewe una akili timamu?

Mbona mimi sioni kosa lake huyo aliyeuliza, ulitakiwa kumuelimisha siyo kumzodoa! Amebainisha kuwa umeandaliwa mkakati wa kulinda makanisa, na je magaidi wakibadili mbinu na kuanza kushambulia magulio, napo tunaweka mkakati mwingine; wakihamia kuteka watu wakiwa makondeni wanalima(kama Kone wa uganda alivyokuwa anafanya); tunakuja na mkakati mwingine. Mikakati viraka haifai, ni muhimu tukawa na mkakati holistic wa ulinzi shirikishi, wananchi, mgambo, sungusungu etc.
 
Mimi nimeshashtukia dili! Nikienda Kanisani nakaa karibu na mlango!
 
tuangalie chanzo cha mataatizo haya ni nini na tutafute ufumbuzi wa kudumu, amani ya kuabudu huku unalindwa na bunduki si amani, amani iwe ya moyoni na si kiwiliwili
 
Serii.imetaka.lile swala lisiusishwe na itikadi za kidini sa kama sio udini kwanini yalindwe Makanisa pekee na sio hadi Misikiti
 
kwanza kabisa dawa ni sheria zilizoko zifanye kazi kwa haki, watu wanapopatikana na hatia adhabu itoke kwa wakati. Mtindo wa siasa kuanzia jan hadi dec ukome. Kila mtu ajue wajibu wake. Jeshi la polisi lipitiwe upya na kuwe na sifa ya ufahamu na uzalendo ni kigezo cha kazi. Mazingira ya polisi yaboreshwe.
 
Kwani Mwanza hakuna polishi

Habari inasema, Makanisa ya Arusha yatawekewa uliniz.

Which is a very reactionary way of dealing with these attacks. Mnasubiri kupigwa, ndo mnaweka ulinzi.

Kama mmeambiwa kwamba ni lazima warudi kupiga hapohapo.

Hatujaambiwa kwamba makanisa ya Mwanza yatawekewa ulinzi.

Ndiyo maana nauliza, wakihamia Mwanza je? Tutakuwa tunaweka ulinzi baada ya kupigwa mabomu tu?

Haya, tutaweka Mwanza, baada ya kupigwa. Wakihamia Mbeya je?

This is a very reactionary approach.
 
Huu ni utumiaji mkubwa wa rasilimali za taifa....najiulizaga sijui watu wanafikiria kwakutumia nini......wakianza kuyalinda makanisa then kesho GULIO likishambuliwa wanatuambia Magulio yote yataanza lindwa na polisi???

Ndo kazi ya jeshi la police....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom