Makamu wa Rais ana kazi gani?

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
Habari zenu wakuu.

Leo nina dukuduku ambalo nataka kulitoa. Sijui kama wenzangu linawatatiza pia. Hivi jamani makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana kazi gani haswa?

Nauliza hivi kutokana na ninayoyaona kwahiyo kama sipo sahihi nitarekebishwa. Kila nikiona kwenye vyombo vya habari namuona makamu wa rais aidha anazindua kitu au ni mgeni rasmi sehemu au anafanya ziara sehemu. Yani amekuwa "mzee wa kukata utepe". Ninachosema ni hivi huyu mtu tunaemuita makamu wa rais tunamlipa na kumhudumia kwa ajili ya kuhudhuria sherehe tu? Kwa nchi masikini kama yetu why do we need a ceremonial leader?

Najua watu wataanza kusema oh ni kwa ajili ya ku-accomodate muungano. Siamini hiyo ni sababu. Kwa maana tunaweza kabisa kufuta nafasi ya makamo wa rais na tukasema rais akitoka upande mmoja wa muungano basi waziri mkuu atoke upande mwingine. Kwanini tupoteze rasilimali za nchi kwa ajili ya kuwa na mtu asiye na shughuli za maana ambazo hata rais na waziri mkuu wanaweza waka gawana na kufanya?

Sina nia ya kumshushia heshima makamu wa raisi wala nafasi ya umakamu wa rais ila ninachosema sasa ifike wakati aidha tumpe makamu wa rais kazi za maana za kufanya au tukifute hiki cheo. Kwa ufahamu wangu, Makamu wa Rais ni msaidizi wa rais kwa maana rais ndiyo anaamua ampe kazi zipi makamu wake. Sasa ni kwamba rais hamuamini makamu wake kumpa kazi zozote za maana?

Jamani hili ndilo dukuduku langu.

========
Jibu lake ni rahisi tu. Hizi ndizo kazi zake kwa mujibu wa kifungu cha 47 katiba ya JMT. Kama kuna kazi nyingine atakuwa anafanya zaidi ya hizi hapa basi hasitahili kulipwa kwani hakuajiriwa kwa zaidi ya hizi hapa.
47.-(1) Kutakuwa na Makamu wa Rais ambaye atakuwa ndiye Msaidizi Mkuu wa Rais kuhusu mambo yote ya Jamhuri ya Muungano kwa jumla, na hususan-
(a) atamsaidia Rais katika kufuatilia utekelezaji wa siku hata siku za Mambo ya Muungano;
(b) atafanya kazi zote atakazoagizwa na Rais;
(c) atafanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje ya nchi.


(2) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 37(5), Makamu wa Rais atapatikana kwa kuchaguliwa katika uchaguzi ule ule kwa pamoja na Rais, baada ya kupendekezwa na chama chake wakati ule ule anapopendekezwa mgombea kiti cha Rais na watapigiwa kura kwa pamoja. Mgombea kiti cha Rais akichaguliwa basi na Mahakmu wa Rais atakuwa amechaguliwa.

(3) Mtu atateuliwa kugombea kiti cha Makamu wa Rais kwa kufuata kanuni kwamba endapo Rais wa Jamhuri ya Muungano atatoka sehemu moja ya Muungano, basi Makamu wa Rais atakuwa ni mtu anayetoka sehemu ya pili ya Muungano.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania


(4) Mtu hatateuliwa kugombea au kushika kiti cha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama-
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa sheria ya Uraia;
(b) ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(d) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi;
(e) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya uchaguzi hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.

(5) Chama chochote hakitazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa mgombea kiti cha Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au kiti cha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.

(6) Makamu wa Rais hatakuwa kwa wakati huo huo Mbunge, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, wala Rais wa Zanzibar.

(7) Endapo mtu ambaye ni Waziri Mkuu, au Rais wa Zanzibar anateuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais ataacha kiti cha Waziri Mkuu, au cha Rais wa Zanzibar, kadri itakavyokuwa.

(8) Makamu wa Rais atatekeleza madaraka yake chini ya uongozi na usimamizi wa Rais, na ataongoza na kuwajibika kwa Rais kuhusu mambo au shughuli zozote atakazokabidhiwa na Rais.
 
Kabla ya kuanza kwa mfumo wa vyama vingi, makamo wa rais alikuwa Rais wa Zanzibar, lakini kwa kuhofia chama kingine kishika madaraka Zanzibar, rais wa Zanzibar ni nobody kwenye set up ya muungano, hivyo sasa Makamo wa rais yupo yupo tuu standby just in case anything happens kwa rais!. Ofisi yake inashughulikia mambo ya mazingira na muungano. Kwa sasa kazi kubwa ya makamo, ni kumwakilisha rais.

P
 
Makamo wa rais yupo yupo tuu standby just in case anything happens kwa rais!. Ila makamo wa rais anapokuwa mchovu mchovu, hilo nalo neno!

Hilo nalo tatizo. If anything happens to the president siyo bora kuachiwa mtu amabe ana experience ya day to day activities za serikali kuliko kumuachia mtu ambae alikua anakaa kaa tu?
 
na msafara wake mzito,pkpk magari km 7 hivi,hii nchi ya ajabu sana kwakweli
 
na msafara wake mzito,pkpk magari km 7 hivi,hii nchi ya ajabu sana kwakweli
Yani acha tu. Unnecessary expenditures everywhere. Nakumbuka wakati Bilal ndiyo kwanza anapata umakamu wa raisi JK alimuambia ikiwezekana aendelee kutoa lecture chuo cha UDOM. Sasa kama makamu wa raisi ana muda wa kufundisha na kusafiri mpaka Dodoma kufanya hivyo ina maana ana a lot of free time.
 
Tuanze na Rais kwanza.. manake bora hata huyo makam wake anakata utepe na kufungua warsha mbali mbali!

Rais yeye kazi yake nini? nchi imegubikwa na matatizo lukuki.. muhimbili watu wanakufa sijasikia lolote la maana zaidi ya ngonjera na siasa za wito!
 
Tuanze na Rais kwanza.. manake bora hata huyo makam wake anakata utepe na kufungua warsha mbali mbali!

Rais yeye kazi yake nini? nchi imegubikwa na matatizo lukuki.. muhimbili watu wanakufa sijasikia lolote la maana zaidi ya ngonjera na siasa za wito!
Tofauti ya raisi na makamu ni kwamba raisi ana nguvu ya katiba kufanya mambo sema mwenywe anashindwa. makamu wa raisi ni hana nguvu yoyote.
 
Ili kuelewa mkorogo huu wa Makamu wa Rais itakupasa urudi miaka ile siasa za vyama vingi ziliporudishwa katika siasa za Tanzania na Muungano.
Mwanzoni, Rais wa Zanzibar alikuwa automatic anakalia kiti hicho ya Makamu wa Rais na alikuwa anawakilisha maslahi ya Zanzibar katika Muungano.

Tulipofuta utaratibu huo wa Zanzibar kuwa Makamo wa Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ndio tumejikuta na Makamu wa Rais ambaye kama ulivyosema katika kutahadharisha "yupo yupo tu ili kuaccomodate Muungano" lakini hawakilishi Zanzibar au maslahi ya Zanzibar katika Muungano.

Jambo baya ambalo linachochea Zanzibar kulalama na kuutupia madongo Muungano ni ile kumfanya Rais wa Zanzibar kuwa ni (Mjumbe )Waziri asiye na wizara maalum katika Baraza la mawaziri wa muungano.

Ukiangalia kwa undani ,tunaweza kusema kuwa Muungano tuliuvunja siku ile tuliyomfanya mwakilishi mkuu wa upande Zanzibar kuwa hana sauti yoyote katika Muungano.

Neno ulilolitumia "ku-accomodate Muungano" lisomeke funika kombe, au kutia changa la macho ili Muungano uzidi kuonekana kuwa ni kichekesho tu. Ni kweli kama ilivyo leo, Nafasi ya Makamu wa Rais ni ukiritimba tu, cheo ambacho kinafuja fedha za walipa kodi.

Inapotokea watu kuanza kuona Serikali ya Muungano haipaswi kuwa na sura ya Kimuungano basi ujue watu wameanza kufuta tongo, watu wameanza kutoka usingizini na kuona mazingaombwe na ombwe la Muungano usio Muungano.

Hiki cheo kuna haja kufutwa ili iwezeshe kuundwa kwa serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar tayari ipo na kuunda serikali ndogo ya Muungano ambayo, Rais wa Tangayika na Rais wa Zanzibar watatawala kama co-presidency ya Muungano na baraza dogo la wizara za muungano.
 
Makamu wa Rais ni Gharama tu kwa walipa kodi kwani nafasi hii ipo only to accommodate siasa za muungano. Miaka ya nyuma, nafasi hii ilikuwa more effective kutokana na kuunganishwa kwake na cheo cha Waziri Mkuu na Rais wa Zanzibar ambapo kulikuwa na makamo wa kwanza na makamo wa pili. Kwahiyo cheo cha makamo wa rais kilionekana kina mashiko lakini kumbe kilikuwa kinabebwa zaidi na kofia za waziri mkuu/rais wa znz.

Nyerere alilshauriwa mfumo huu na tume ya Judge Bomani ambae yeye aliiga mfumo wa mgombea mwenza wa Marekani kama njia ya kuondokana na hofu iwapo CUF ingeshinda Uchaguzi ZnZ, kwani chini ya utaratibu wa zamani, rais wa zanzibar alikuwa automatically makamo wa Rais wa muungano. Vilevile mfumo wetu wa muungano nyerere aliiga ule wa UK (Ireland, Wales, Britain). Kwahiyo, with all due respect to baba wa taifa, kuna mambo mengine hayawezi kuwa effective yakiwa to ni 'copy and paste' from another context.
 
Back
Top Bottom