Nimekuwa najiuliza sana sipati jibu, kwanini January Makamba aliamua kumuuliza Mzee Butiku swali la kijinga hivyo? Eti kwanini serikali ya awamu ya kwanza haikujenga shule nyingi za sekondari.
Ikumbukwe awamu ya kwanza ilijenga maelfu ya shule za msingi na mtakubaliana nami kuwa majengo na rasilimali zilizoekezwa kwenye shule hizo ni nyingi kuliko vishule vya kata vinavyojengwa. Shuleza msingi za wakati huo zina majengo na miundo mbinu imara sana kuliko shule za kata.
Pili tuwaulize hao akina Makamba, General tyre ipo wapi,tanganyika pakers ipo wapi, viwanda vyetu na mashirika yetu yapo wapi, serikali imeenda wapi hadi kushindwa kupambana na rushwa, uzalendo umeenda wapi? Hivyo serikali ya awamu ya kwanza ndio hasa yenye maswali ya kuwauliza akina makamba na si wao kuuliza maswali ya kijinga.
Ikumbukwe awamu ya kwanza ilijenga maelfu ya shule za msingi na mtakubaliana nami kuwa majengo na rasilimali zilizoekezwa kwenye shule hizo ni nyingi kuliko vishule vya kata vinavyojengwa. Shuleza msingi za wakati huo zina majengo na miundo mbinu imara sana kuliko shule za kata.
Pili tuwaulize hao akina Makamba, General tyre ipo wapi,tanganyika pakers ipo wapi, viwanda vyetu na mashirika yetu yapo wapi, serikali imeenda wapi hadi kushindwa kupambana na rushwa, uzalendo umeenda wapi? Hivyo serikali ya awamu ya kwanza ndio hasa yenye maswali ya kuwauliza akina makamba na si wao kuuliza maswali ya kijinga.