Makamba: Kwanini serikali ya Nyerere haikujenga shule nyingi za sekondari?

ibange

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
1,543
550
Nimekuwa najiuliza sana sipati jibu, kwanini January Makamba aliamua kumuuliza Mzee Butiku swali la kijinga hivyo? Eti kwanini serikali ya awamu ya kwanza haikujenga shule nyingi za sekondari.

Ikumbukwe awamu ya kwanza ilijenga maelfu ya shule za msingi na mtakubaliana nami kuwa majengo na rasilimali zilizoekezwa kwenye shule hizo ni nyingi kuliko vishule vya kata vinavyojengwa. Shuleza msingi za wakati huo zina majengo na miundo mbinu imara sana kuliko shule za kata.

Pili tuwaulize hao akina Makamba, General tyre ipo wapi,tanganyika pakers ipo wapi, viwanda vyetu na mashirika yetu yapo wapi, serikali imeenda wapi hadi kushindwa kupambana na rushwa, uzalendo umeenda wapi? Hivyo serikali ya awamu ya kwanza ndio hasa yenye maswali ya kuwauliza akina makamba na si wao kuuliza maswali ya kijinga.
 
achana na hawa majuha, wakikaa na kikwete wanamdanganya kuwa tangu tupate uhuru hakuna kiongozi kama wewe mzee, umejenga barabra za lami, wamesahau Nyerere alijenga barabara za lami , dsm hadi mbeya km900! reli, mahule, nk. sasa hizo sekondari angejenga nyingi za nini wakati population ilikuwa ndogo sana, wangeenda akina nani kule. pia akumbuke huyo juha kuwa shule za seriakli kama Tosamaganga ilikuwa ina chukua zaidi ya wannafunzi 1000! Nyerere alitembea hadi urusi kutafuta walimu, na leo tuna wahandisi, madaktari kupitia malengo na mipango ya Mwalimu
 
achana na hawa majuha, wakikaa na kikwete wanamdanganya kuwa tangu tupate uhuru hakuna kiongozi kama wewe mzee, umejenga barabra za lami, wamesahau Nyerere alijenga barabara za lami , dsm hadi mbeya km900! reli, mahule, nk. sasa hizo sekondari angejenga nyingi za nini wakati population ilikuwa ndogo sana, wangeenda akina nani kule. pia akumbuke huyo juha kuwa shule za seriakli kama Tosamaganga ilikuwa ina chukua zaidi ya wannafunzi 1000! Nyerere alitembea hadi urusi kutafuta walimu, na leo tuna wahandisi, madaktari kupitia malengo na mipango ya Mwalimu

Tena kipindi hicho hata chembe moja ya dhahabu ilikuewa imechimbwa
 
Nimekuwa najiuliza sana sipati jibu, kwanini January Makamba aliamua kumuuliza Mzee Butiku swali la kijinga hivyo? Eti kwanini serikali ya awamu ya kwanza haikujenga shule nyingi za sekondari. Ikumbukwe awamu ya kwanza ilijenga maelfu ya shule za msingi na mtakubaliana nami kuwa majengo na rasilimali zilizoekezwa kwenye shule hizo ni nyingi kuliko vishule vya kata vinavyojengwa. Shuleza msingi za wakati huo zina majengo na miundo mbinu imara sana kuliko shule za kata.

Pili tuwaulize hao akina makamba, General tyre ipo wapi,tanganyika pakers ipo wapi, viwanda vyetu na mashirika yetu yapo wapi, serikali imeenda wapi hadi kushindwa kupambana na rushwa, uzalendo umeenda wapi? Hivyo serikali ya awamu ya kwanza ndio hasa yenye maswali ya kuwauliza akina makamba na si wao kuuliza maswali ya kijinga

WAKUU!

Heshima kwenu!

Nilisha wahi kusema hapa kwamba " KENGE NI KENGE TU, HAZAI MAMBA". Huyu Januari Makamba mnatarajia kitu gani cha maana kutoka kwake? Hivi yeye tulipokuwa pale Galanos alikuwa anaionaje ile shule? Habu ajaribu kukumbuka jinsi miundo mbinu yake ilivyo bora kulinganisha na hilo swali alilo muuliza nd. Butiku!!! Hivi analinganisha hivi vishule vya YEBOYEBO na mambo aliyo yafanya Mwalimu JK Nyerere?

Hakumbuki kwamba pale Galanos tulikuwa tuna soma wanafunzi wasiozidi 35 kwa kila darasa na kila mmoja akiwa ana dawati bora la kukalia, vitabu vya kiada vya kutosha, maabara za uhakika, kitanda na dodoro na vyombo vya chakula unapewa shuleni. Nauli ya kwenda na kurudi shuleni unapewa na serikali kupitia shulani. Leo hii anakuja na maswali ya kijanga kiasi hiki!!! Hivi ni vigezo vipi vilivyo tumika kuapewa uwaziri? Au ndiyo hivyo, kwa sabababu tuna uongozi wa kiblaa blaa ndiyo basi tena, kila mwenye jina kubwa anafaa kuwa kiongozi!!!

Watanzania tuna wajibu wa kutafakari tena ili tuliokoe taifa hili. Kama tutaendelea kuwa na viongozi wa aina hii, ambao hata akili ya kufikiria na kukumbuka miaka michache iliyopita hali ilikuwa je hawana, tutaangamia.
 
Ni matokeo ya serikali za muundo wa kiukoo, mtoto wa kada maarufu wa ccm Bwana Yufusu makamba.

Yusufu makamba baba wa January atakumbwa si kwa la maana lolote bali kwa kuiangamiza na kuiacha taaban ccm.

January ni kilaza, na kama kawaida ya kilaza yoyote hujidhihilisha kwa kauli na matendo yake. kwa ukilaza huu eti anataka kuwa rais wa Tz, hili ni balaa jengine lakuepuka.
 
Tunapozungumzia elimu tunazungumzia ubora wala si uwingi anachozungumzia yeye ni uwingi lakini ukija kwenye ubora umeshuka chukulia sasa hivi wanafunzi wanaingia sekondari bila kujua kusoma na kuandika unajenga shule wakati hamna walimu mwanafunzi anaanza kidato cha kwanza mpaka anamaliza hajawahi kufundishwa baadhi ya masomo shule hazina viwanja vya wanafunzi kuchezealakini hizo zote ni tambo za kujiona mimi ni bora kuliko yule lakini Butiku akumjibu makamba bali alimjibu mpaka aliyemteua kitendo cha kumwambia rudi kwenye chama ukasome chama kilikuwa kinazungumzia nini kuhusu elimu ni kumwambia mwenyekiti wa chama kuwa amekuwa akikurupuka kuteuaviongozi wa chama ambao hata chama hawakijui
 
Hamkumuelwa huyu dogo. Yeye alikuwa ana mawazo ya namna ya kupata rushwa na kufanya ufisadi. Alikurupika na kujikuta akiropoka. Hata hizo data kazipata wapi? Mbona hakuuliza kwa nini wanafunzi sasa hivi wanafaulu mitihani wakati hawajui kusoma , kuandika na kuhesabu? Ajibu haya ndipo aulize huu ujinga wake.
 
Back
Top Bottom