Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,845
Wasalam waleikhum..!
Kidogo tumepumzishwa kwenye zile sinema zetu.... Tumepata msimu mdogo wa mwanadini muimba nyimbo za injili mwanadada na mama wa watoto Rose Muhando.
Hii inaweza kuwa mada ya NNE kumhusu... Japo nyingine zilizotangulia zikimjadili Rose wa sasa kama celeb na kile kinachomtokea...
Kwanza itambulike kuwa hii ni vita ya kiroho, falme za giza dhidi ya falme za nuru, wakuu wa mbingu dhidi ya wakuu wa anga...
Rose ni catalyst tu katika vita kubwa ya kiroho na ya kidunia... Nuru dhidi ya giza... Alikuwa jemadari msimu wa kwanza akapambana vilivyo, akazishinda falme za giza katika maeneo mengi.. Lakini kwakuwa ana mwili wa damu na nyama, alilemewa... Akazidiwa akampa adui nafasi... Sasa anatengenezwa...!
Rose Muhando ni nani?
Kwa wale waliobahatika kusoma habari zake huko nyuma... Aliingia kwenye uimbaji wa nyimbo za injili akitokea kwenye ndoa iliyojaa mateso (kwa mujibu wake) akiwa na karama ya uimbaji na mahitaji ya nyakati kumbeba aliibuka kuwa mmojawapo wa nyimbo za injili mwenye kipaji na mafanikio mengi... Lakini mafanikio yake yalikuwa kwenye hatari kubwa kwakuwa aliyapata kwa kupambana na shetani (kimtazamo)
Kuna wakati tunaweza kusema kwa hakika Rose alikuwa mlokole kamili na nyimbo zake zikiwaokoa na kuwabariki wengi....
Misukosuko ilipoanzia
Zaburi ya 23 kuna mstari unasema... Nijapopita katika bonde la uvuli wa mauti....! Kila mmoja wetu ana mapito yake ... Hata waimbaji wenzake walishapitia anayopitia... Si wa kwanza yeye na hatakuwa wa mwisho... Shida iko hapa, je unapopitia kwenye mapito unasimama upande gani? Wa nuru au giza? Anguko lako ama kusimama tena vitategemea ulikuwa upande gani... I mean upande gani uliupa airtime kubwa....! Ni wazi Rose alipojaribiwa aliingiwa na upofu na kumpa Mungu wake kisogo akaenda kufanya kolabo na upande wa giza... Sasa anasulubiwa.. Msimu huu wa pili anamsaidia adui.. Na huu ndio ushindi uliokuwa unatafutwa na falme za giza
Imekuwaje aibukie Kenya?
Kwanza kiuhalisia Rose ni kweli kabisa anaumwa na hayupo sawa.. Ni kama mwaka sasa tumekuwa hatusikii habari zake nzuri.. Amepitia mapito mengi, amechapwa akachapika.. Anaonekana live ana POP mkononi vidonda na makovu.. Na kwa maneno yake mwenyewe kwa takriban siku 90 alikuwa hajui anatoka wapi anaenda wapi... Amekuwa kama chizi fresh, zinatoka zinarudi... Alifikaje Kenya kwa hali ile? Alipelekwa? Alifikaje kwa yule mtume nabii?
Kisanga kinaanzia hapa!
Dunia ya leo watu hupenda kuyatumia matatizo ya wengine kujinufaisha ama kuwatumia wao wenyewe pia...
Rose Muhando ni jina kubwa Afrika mashariki. Habari zake zikisikika popote ndani ya jumuiya hii si jambo geni
Mtume na nabii kwa kuiona fursa... Anamuahidi kumsaidia Rose kwa masharti hasa la kutaka amuombee mbele ya waumini wake kukiwa na camera zinazochukua video na picha.. Lakini la zaidi anamfundisha cha kuongea..
Nimeangalia kwa makini video ile.. Sijui misa ilianzaje lakini anaonekana mtumishi wa Mungu akimwita Rose aliyechoka na kuanza kumuombea.
Ghafla Rose anaanguka na mapepo yanaaza kuongea kuwa kuna wivu juu ya mafanikio yake, hawataki aimbe, wamechukua magari yake wanataka kumuua nknk... Lakini ni wakati huu mapepo yakiongea Rose ana ufahamu wa kuondoa mkono wa mtumishi mdomoni mwake aweze kuongea vizuri....
Baada ya maombi mafupi mapepo yanatimka na hapo hapo Rose anazinduka na kuanza kuongea yaleyale yaliyokuwa yakiongelewa na mapepo... Halafu anaendelea kuelezea changamoto za familia yake, watoto kukosa ada nk.. Halafu anamalizia kwa kumshukuru Mungu...
Rose, Mungu hadhihakiwi... Mapepo hayatoki kivile na fahamu hazirudi kivile.. Nguvu ya pepo kutoka si ya kitoto (nitaelezea kwenye mada nyingine)
Umetumika vibaya kwenye mapito yako... Angalia wanaokutumia wasikuongoze kwenye anguko kuu
Kidogo tumepumzishwa kwenye zile sinema zetu.... Tumepata msimu mdogo wa mwanadini muimba nyimbo za injili mwanadada na mama wa watoto Rose Muhando.
Hii inaweza kuwa mada ya NNE kumhusu... Japo nyingine zilizotangulia zikimjadili Rose wa sasa kama celeb na kile kinachomtokea...
Kwanza itambulike kuwa hii ni vita ya kiroho, falme za giza dhidi ya falme za nuru, wakuu wa mbingu dhidi ya wakuu wa anga...
Rose ni catalyst tu katika vita kubwa ya kiroho na ya kidunia... Nuru dhidi ya giza... Alikuwa jemadari msimu wa kwanza akapambana vilivyo, akazishinda falme za giza katika maeneo mengi.. Lakini kwakuwa ana mwili wa damu na nyama, alilemewa... Akazidiwa akampa adui nafasi... Sasa anatengenezwa...!
Rose Muhando ni nani?
Kwa wale waliobahatika kusoma habari zake huko nyuma... Aliingia kwenye uimbaji wa nyimbo za injili akitokea kwenye ndoa iliyojaa mateso (kwa mujibu wake) akiwa na karama ya uimbaji na mahitaji ya nyakati kumbeba aliibuka kuwa mmojawapo wa nyimbo za injili mwenye kipaji na mafanikio mengi... Lakini mafanikio yake yalikuwa kwenye hatari kubwa kwakuwa aliyapata kwa kupambana na shetani (kimtazamo)
Kuna wakati tunaweza kusema kwa hakika Rose alikuwa mlokole kamili na nyimbo zake zikiwaokoa na kuwabariki wengi....
Misukosuko ilipoanzia
Zaburi ya 23 kuna mstari unasema... Nijapopita katika bonde la uvuli wa mauti....! Kila mmoja wetu ana mapito yake ... Hata waimbaji wenzake walishapitia anayopitia... Si wa kwanza yeye na hatakuwa wa mwisho... Shida iko hapa, je unapopitia kwenye mapito unasimama upande gani? Wa nuru au giza? Anguko lako ama kusimama tena vitategemea ulikuwa upande gani... I mean upande gani uliupa airtime kubwa....! Ni wazi Rose alipojaribiwa aliingiwa na upofu na kumpa Mungu wake kisogo akaenda kufanya kolabo na upande wa giza... Sasa anasulubiwa.. Msimu huu wa pili anamsaidia adui.. Na huu ndio ushindi uliokuwa unatafutwa na falme za giza
Imekuwaje aibukie Kenya?
Kwanza kiuhalisia Rose ni kweli kabisa anaumwa na hayupo sawa.. Ni kama mwaka sasa tumekuwa hatusikii habari zake nzuri.. Amepitia mapito mengi, amechapwa akachapika.. Anaonekana live ana POP mkononi vidonda na makovu.. Na kwa maneno yake mwenyewe kwa takriban siku 90 alikuwa hajui anatoka wapi anaenda wapi... Amekuwa kama chizi fresh, zinatoka zinarudi... Alifikaje Kenya kwa hali ile? Alipelekwa? Alifikaje kwa yule mtume nabii?
Kisanga kinaanzia hapa!
Dunia ya leo watu hupenda kuyatumia matatizo ya wengine kujinufaisha ama kuwatumia wao wenyewe pia...
Rose Muhando ni jina kubwa Afrika mashariki. Habari zake zikisikika popote ndani ya jumuiya hii si jambo geni
Mtume na nabii kwa kuiona fursa... Anamuahidi kumsaidia Rose kwa masharti hasa la kutaka amuombee mbele ya waumini wake kukiwa na camera zinazochukua video na picha.. Lakini la zaidi anamfundisha cha kuongea..
Nimeangalia kwa makini video ile.. Sijui misa ilianzaje lakini anaonekana mtumishi wa Mungu akimwita Rose aliyechoka na kuanza kumuombea.
Ghafla Rose anaanguka na mapepo yanaaza kuongea kuwa kuna wivu juu ya mafanikio yake, hawataki aimbe, wamechukua magari yake wanataka kumuua nknk... Lakini ni wakati huu mapepo yakiongea Rose ana ufahamu wa kuondoa mkono wa mtumishi mdomoni mwake aweze kuongea vizuri....
Baada ya maombi mafupi mapepo yanatimka na hapo hapo Rose anazinduka na kuanza kuongea yaleyale yaliyokuwa yakiongelewa na mapepo... Halafu anaendelea kuelezea changamoto za familia yake, watoto kukosa ada nk.. Halafu anamalizia kwa kumshukuru Mungu...
Rose, Mungu hadhihakiwi... Mapepo hayatoki kivile na fahamu hazirudi kivile.. Nguvu ya pepo kutoka si ya kitoto (nitaelezea kwenye mada nyingine)
Umetumika vibaya kwenye mapito yako... Angalia wanaokutumia wasikuongoze kwenye anguko kuu