Makahaba/Matapeli wa mapenzi SGR station Dodoma

and 998 others

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2012
Posts
28,224
Reaction score
39,704
Ndugu zangu tuchukue tahadhari tukitembelea Dodoma hususani wageni wa mji wa Dodoma (demu unamkuta yupo pale pa kusubiria wageni kama TAXI driver vile anasubiria Mgeni, kwa shepu na muonekano lazima ujichanganye. Tukiwa Kwenye gari anadai twende tukalale kwake badala ya hotel.,.).

Nimetapeliwa na demu pale SGR station Dodoma kwa njia ya ajabu Sana kwa ahadi ya mapenzi.

Demu anaonekana anajiweza sana, muonekano na gari analotumia. Ghafla akadai anafanya biashara ya pikipiki anataka tufanye wote. Tukiwa room anaomba nimtumie 3m kutoka benki yangu kwenda akaunti yake ili kumlipa supplier wake wa Dar.

Mpaka muda huu najiuliza nilitoaje Ile pesa huenda anatumia dawa aisee
 
Nimetapeliwa na demu pale SGR station Dodoma kwa njia ya ajabu Sana kwa ("ahadi ya mapenzi.")

Kichwa cha chini kilikuwa kimeshapata moto, ukashindwa kuushirikisha ubongo vizuri, usitafute mchawi nani, ni wewe mwenyewe.
 

Mkuu hapa nimekuelewa yaani yasipomkuta mtu hawezi kuelewa.
 
Kutapeliwa kisa penzi la mtu ambae humjui nalo ni tatizo lingine.

Mwisho wa yote pole, 3 million kwa usawa huu ni nyingi. Huwa nikifika Dodoma ni moja kwa moja hotel ambayo nakuwa nimefanya booking, baada ya hapo ndio meeting na mtu tu ambae nina miadi nae nje ya hapo hapana, hii popote napo enda sio dodoma tu ( nimejiwekea huo utaratibu )
 
Hapana hakuna dawa / uchawi ni wewe mwenyewe na upwiru wako / hii DUNIA SIO ya wanaume dhaifu pole sana sanaa kaka.

Huku pakiwa madawa ya kulevya kwenye chuchu ukajikuta umelala umeibiwa Kila kitu..Mimi ni nadra sana sanaa kumwamini mwanamke stranger.

Tena sisi wapiga pombe Huwa tuna usingizi sana usiku baada ya gemu plus pombe..ila ndio ivyo akili ku mkichwa HATUJAWAI kutapeliwaa..

Kwako min -me
 
Hapo hakuna utapeli bwashee safi sna
 
Hiyo 3m ungeenda Riverside ungefunga na vijiwe vyenyewe vyote na change ingebakiπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Kwa akili hizi ndio unataka kuandamana kupinga uvamizi wa US huko Iran? Wewe mwenyewe unahitaji ukombozi kwanza.
 
Niliwai kuhonga pesa yote ya ada nikajua TU ntaipata haahaa sisi wa government enzi izo ada 75,000 πŸ˜πŸ˜†πŸ˜πŸ˜ƒπŸ˜€

Natania TU mchaga mie nionge pesa ya ADA YA SHUREEEEE haaahaa πŸ˜‚πŸ˜‚
Mimi kwenye maulevi nilisha tunza kwenye live band zaidi ya mil 2 ,ambayo ni pesa ya mtaji wangu ambayo niliweka ni karata yangu ya mwisho ya kutoboa Seran πŸ˜…
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…