Ngaliba Dume
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,710
- 3,669
Siku chache baada ya Waziri wa Nishati "kumlipua" mmiliki wa St.Mary's Sec. School ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu(CCM) Mch.Rwakatare kuwa ni mwizi sugu wa umeme na uhujumu wa miundo mbinu ya Tanesco kama "Mita" za Luku n.k,hali hiyo imejitokeza tena kwa kada mwingine CCM.
Jana ktk kuongea na vyombo vya Habari,Maafisa wa Tanesco wamemtaja Ndugu Julian Bujugo mmiliki wa Shule za Green Acres kuwa ni miongoni mwa wezi sugu wa umeme na uhujumu wa miundombinu ya Tanesco...na kuwa ndugu Bujugo ameeibia Tanesco umeme kwa kujiunganishia umeme toka mwaka 2005 na hivyo kudaiwa mabilioni ya fedha ktk shule ya Green Acres-Salasala(DSM)
Itakumbukwa kuwa Mh.JULIAN BUJUGO ni diwani wa kata ya Magomeni na anahusika na uuzaji wa eneo la wazi (Open Space) la Magomeni lililo pembeni ya Magomeni kanisani..mpaka sasa ukipita pale Bustan ya Magomeni kuna Bar ya Wazi imefunguliwa ndani ya hiyo Open Space. Ukifuatilia utajua,Viongozi au makada wengi wa CCM wanaomiliki baadhi ya taasisi mbali mbali,wanatumia vyeo vyao na nafasi zao kuiba umeme,na wanatumia network yao kuwatisha watumishi wa TANESCO.
Jana ktk kuongea na vyombo vya Habari,Maafisa wa Tanesco wamemtaja Ndugu Julian Bujugo mmiliki wa Shule za Green Acres kuwa ni miongoni mwa wezi sugu wa umeme na uhujumu wa miundombinu ya Tanesco...na kuwa ndugu Bujugo ameeibia Tanesco umeme kwa kujiunganishia umeme toka mwaka 2005 na hivyo kudaiwa mabilioni ya fedha ktk shule ya Green Acres-Salasala(DSM)
Itakumbukwa kuwa Mh.JULIAN BUJUGO ni diwani wa kata ya Magomeni na anahusika na uuzaji wa eneo la wazi (Open Space) la Magomeni lililo pembeni ya Magomeni kanisani..mpaka sasa ukipita pale Bustan ya Magomeni kuna Bar ya Wazi imefunguliwa ndani ya hiyo Open Space. Ukifuatilia utajua,Viongozi au makada wengi wa CCM wanaomiliki baadhi ya taasisi mbali mbali,wanatumia vyeo vyao na nafasi zao kuiba umeme,na wanatumia network yao kuwatisha watumishi wa TANESCO.