Majuto: Mchepuko anataka kunipeleka kwa Makonda

Majuto: Mchepuko anataka kunipeleka kwa Makonda

mkuu anatikisa kiberiti tu huyo ...250k per month ni pesa mingi sana
 
Hakuna kesi mkuu pale sio mahakamani ni sehem ya maridhiano.
 
Msg za kwenye cm c'yo guarantee/hazipo secured;cm ikipotea na ushahidi unapotea,pia m2 anaweza kuzifuta hata mtoto au akichezea cm anaweza kuzifuta kwa bahati mbaya
Cha kufanya hapo mgungulie account cuz ikitokea ww au yy amepoteza au kuficha deposit in slip,unaenda bank wanaku-printia bank statement
Ishi kama msomi wa karne ya 21,huyo manzi atakujakukushinda kwenye kuongea bila ya ww kuwa na ushahidi!
Akienda kampuni ya mtandao husika anapewa miamara atakayoitaji, na kwa voda huna hata haja ya kwenda unaweza vuta transaction zote wewe mwenyewe
 
Ilikuwa kama utani mwaka 2013 tukiwa kwenye daladala za Kimara - Posta. Nilimtongoza akanitunuku na mimba ya mtoto wa kike ikapatika na akajifungua salama salmini.

Kifupi nimekuwa nikitoa huduma zote kwa huyu mchepuko tokea akiwa mjamzito na nahudumia kwa kutoa kama laki mbili na nusu kila mwezi, lakini haridhiki kabisa anasema fedha haitoshi sababu mtoto anaugua mara kwa mara na mimi nilishamwambia siwezi toa zaidi ya hapo coz hata wife hamjui na nina watoto wengine kwa wife.

Tatizo ni tokea Makonda atangaze kuwa wanawake waliotelekezewa watoto wakatoe taarifa, aisee the whole week am at high risk... nalala kwa shida ni mawazo tu hadi wife kanistukia.. Ni ananitishia kila siku simu haziishi kuwa jumatatu atakuwa wa kwanza kunireport kwa Makonda, na mzaramo huyu kichwa chake antena haipo sawa najua hatanii ataenda tu. Nimejaribu kumtumia rafiki yake amshauri imeshindika.

Jana jioni nimemtumia laki moja, asubuhi hii kanitumia sms... "Unajua kulea wewe? Umenitumia vihela vya mboga hivi huoni wanaume wenzio wanavyotoa? Unajua Mobetto anapewa sh ngapi kwa siku? Kwa taarifa yako hii ni nauli ya tax kesho kwenda kwa Makonda"... Wakuu hapa nakaribia kuwa chizi sometime najikuta naongea alone.
NAOMBENI USHAURI WENU TAFADHALI
By Pius
Anaomba ushauri pius
FB_IMG_1523275461606.jpg
 
Kama ni kweli utakuwa na ushahidi wa hiyo hela uliyotaja utakuwa huna hatia ila kama unajisifia hapa itakula kwako.
 
Aisee... jamaa naona jamaa wanataka kuchukulia matatizo yangu kama burudan .. mimi kama ndio ushauri mzuri nimepokea toka jana na nimefanya maamuzi... cha kusubiri hapa ni mrejesho la huko whatsapp mimi silijui, najua wamecopy hapa
Kuna mtu venchwa ameleta uzi kama huu...
 
Back
Top Bottom