Majuto: Mchepuko anataka kunipeleka kwa Makonda

Majuto: Mchepuko anataka kunipeleka kwa Makonda

Mzee mbona unafanywa mdogo kama pilitoni AF unakbali kizembe? Halaf kwnza yeye anafanya kazi gani?
Ana saloon ya kike... mkuu mm ni mbabe ila kwa wife salute.. na huyu mchepuko ninachoepusha ni mzozo kwa wife.
 
Achana naye huyo hana la kukushinda tena asipokaa vizuri hiyo hela itapunguzwa
 
Sheria ya nnchi kupitia ustawi wa jamii ni elfu 75 kwa mweziiii. Kwanza laki 2 unampendelea sana mm wife wangu alikimbia akaenda nikamwambia nenda nikaweka mwanasheria sasa anaambulia elfu 75 tu basi.
 
Haya sasa,...gharama zote/Huduma ulizokuwa unampatia mama mtt wako ulikuwa unaziwekea record yoyote ya kuonesha labda malipo yaliyofanyika???
Hapa nina baadhi ya sms za mpesa tu.. kwani huwa sifuti sms
 
Sasa unapompa fedha za matumizi uwe unamuingizia kwenye account,baada ya hapo unaitoa-copy deposit slip...original unampa yeye na nakala unabaki nayo kwa sababu anaweza kukupeleka kwenye vyombo vya dola (police, ustawi wa jamii,kwa Bashite) na akifka huko anakana kuwa hujawahi kumpatia fedha za matumizi,lkn kama utakuwa na nakala ya deposit slip itakulinda

Pia,huyu mwanamke anaweza kuja kumdanganya mtoto kwa kumjaza maneno 'baba yako m2 mbaya sana hawahi kutoa hata mia ya sabuni tangu ulipozaliwa,yeye tangu ujana wake ni m2 wa kuhangaika na wanawake tu"
Ni mpesa tu, account yenyewe hana
 
Sasa kwa Makonda anaenda kushitaki nn pesa haitoshi au katelekezwa???
Mm nina mtoto wa kiume nje ya ndoa na wife anajua maana kanikuta nmeshazaa naye huwa natoa laki kila mwezi na familia yake wananipenda hatari sembuse laki mbili??.
Hofu yako ni mkeo na wala siyo Bashite
 
Sheria ya nnchi kupitia ustawi wa jamii ni elfu 75 kwa mweziiii. Kwanza laki 2 unampendelea sana mm wife wangu alikimbia akaenda nikamwambia nenda nikaweka mwanasheria sasa anaambulia elfu 75 tu basi.
Kweli jamiiforum ni zaidi ya ujuzi, nitazingatia hili
 
Makondaa akianzishaa Kampeni yoyotee juaa Kunaa watu flani wa Upinzani au wanaoipinga na kuikosoa Serikali watafall kwenye huoo mtegoo...!! Huwa hana lengo la kusaidia kweli bali kukomoaa wachache anaowataka... So relax kijanaa..[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Itunze hio mesej ya mwamala wa pesa uliomtumia kama ushahidi wako
Kingine—ameshajuwa werkness yako ndio maana anakuendesha kama gari bovu
Akikwambia ataenda kwa makonda kukuripoti
Mjibu—Mbona umechelewa?changamka sasa hivi uwende
Tatazo anakudesh kidoogo wewe mavi debe
Kila unavozidi kumpliz ndio unazidi kumpa bichwa[emoji1321]
 
Hahahahaha lol! Na hizi stress za huyu mzaramo cheza mbali na kumwambia wife maana unaweza kabisa kuzua balaa jingine. Pole Mkuu ila usiwe na hofu sana.

Wife tena[emoji15] [emoji15]
 
Mkuu unatoa ela nyingi sanaa,
Ila utakua unaogopa wife asijue, lkn kuhusu kuumwa watoto wanatibiwa bure pia mkatie bima NHIF ni sh 50400 tuu kwa mtoto,
Mkuu akikupeleka kwa makonda ndio ukammalize kabisa utawaambia nna uwezo wa laki na hamsin tuu,
Mjomba angu alkua ananyanyaswa na dada kazaa nae watoto wa2, kafilisi duka, mke kakopa kazini kafilisi tena, wameuza kiwanja wamejaza tena duka ikabidi watu wakamtonye mke wa mjomba, akamwambia mjomba kalete hao watoto, kamfata mzazi mwenzie kaomba watoto kapewa alidhani anatania hawezi kuwachukua maana mkewe hajui kumbe ashajua, mke kachukua watoto kapeleka kijijiniiii, ndio ikawa nafuu ya mjomba kunyanyaswa na mchepuko,
Kua makini mkuu atakunyanyasa sana kwa kigezo cha kuficha mkeo asijue.
 
Hapa nina baadhi ya sms za mpesa tu.. kwani huwa sifuti sms
Msg za kwenye cm c'yo guarantee/hazipo secured;cm ikipotea na ushahidi unapotea,pia m2 anaweza kuzifuta hata mtoto au akichezea cm anaweza kuzifuta kwa bahati mbaya
Cha kufanya hapo mgungulie account cuz ikitokea ww au yy amepoteza au kuficha deposit in slip,unaenda bank wanaku-printia bank statement
Ishi kama msomi wa karne ya 21,huyo manzi atakujakukushinda kwenye kuongea bila ya ww kuwa na ushahidi!
 
sasa na wewe ulimpa mimba ya nini na pesa ya kulea mtoto huna laki mbili kweli haitoshi ongeza ongeza kidogo
 
Ilikuwa kama utani mwaka 2013 tukiwa kwenye daladala za Kimara _ Posta. Nilimtongoza akanitunuku na mimba ya mtoto wa kike ikapatika na akajifungua salama salmini.
Kifupi nimekuwa nikitoa huduma zote kwa huyu mchepuko tokea akiwa mjamzito na nahudumia kwa kutoa kama laki mbili na nusu kila mwezi, lakini haridhiki kabisa anasema fedha haitoshi sababu mtoto anaugua mara kwa mara na mimi nilishamwambia siwezi toa zaidi ya hapo coz hata wife hamjui na nina watoto wengine kwa wife.

Tatizo ni tokea Makonda atangaze kuwa wanawake waliotelekezewa watoto wakatoe taarifa, aisee the whole week am at high risk... nalala kwa shida ni mawazo tu hadi wife kanistukia.. Ni ananitishia kila siku simu haziishi kuwa jumatatu atakuwa wa kwanza kunireport kwa Makonda, na mzaramo huyu kichwa chake artena haipo sawa najua hatanii ataenda tu, nimejaribu kumtumia rafiki yake amshauri imeshindika. Jana jioni nimemtumia laki moja, asubuhi hii kanitumia sms... "unajua kulea wewe? Umenitumia vihela vya mboga hivi huoni wanaume wenzio wanavyotoa? Unajua Mobeto anapewa sh ngapi kwa siku? Kwa taarifa yako hii ni nauli ya tax kesho kwenda kwa Makonda"... wakuu hapa nakaribia kuwa chizi sometime najikuta naongea alone... Ushauri tafadhali..
Mwache aende ataumbuka yeye. Mbaya zaidi ushamwonyesha uoga na amepata pa kukukamatia. Huyo anakutishia tu na haingii kwenye kundi la watu wa makonda. Kwanza usikute huyo mtoto sio wako unalelea wengine aisee. Pole sana. Mi ngesha mdelete siku nyingi na aende popote pale maana MTU asiye na shukrani hudhalilika vibaya. Hiyo laki 2 nyingi sana mkuu kwa MTU kama huyo. Ungepunguza weee mpaka iwe zero kama anaendelea na mambo ya ajabu. Akikupeleka we mkane tu Dadeki na hawezi kwenda anakutishia kitoto toto
 
Back
Top Bottom