Majukumu yamenielemea

Majukumu yamenielemea

Usiendekeze upumbavu kila binadamu mwenye viungo kamili na akili timamu anatakiwa atafute chake.shida zipo lakini angalia zenye ulazima.you can't please everybody my friend
Ukijifanya mwema sana kwa kila ndugu na jamaa utaishia kuwa masikini. Baadae ni hao hao watakaokucheka na kukusema umeshindwa kujenga nyumba au kununua gari kisa ulikuwa unatumia fedha ovyo.
 
ilo ndio tatizo la kuzaliwa kwenye familia za kimasikini. mimi uwa nakuwa nabadirisha namba mara kwa mara. ndugu wamekuwa hawawezi tena kujituma wakiona ndugu upo na kipato kinono
 
Wewe ndio una suluhisho sahihi. Hapa unaweza shauriwa vibaya ukapata laana kwa kushindwa kusimama katika yale unayopaswa kutenda.

Kuna jamaa alifanikiwa akajenga nyumba kubwa sana mama yake akamuhusia kuishi na nduguze mama alipokufa jamaa akauza ile nyumba na kusambaza ndugu zake ili wajitegemee. Wengi waliangaika sana baada ya kusambazwa ila jamaa naye ali suffer kinoma maana hata ile nyumba aliiuza tena mwishowe wanaye wote walikufa pia sasa kabakia na kijana mmoja naye choka mbaya sana.

Hivyo suala la ndugu ni la kuangalia sana.
Watt walikufa kwasababu gan mkuu?
 
Pole mkuu hizi familia zetu mtihani sana,sema ukipata nafasi angalia namna ya kuwainua kupunguziana mzigo
Sema ndiyo wajitume sasa...
Kama uko na nafasi wasaidie tu ila nao wajisaidie

Ova
 
Habar Zenu

Mwenzunu nimejikuta kwenye wimbi la mawazo Baada ya kuelemewa na majukum. Baada ya Kupata kibarua nimejikuta napokea simu nyingi kuhusu Matatizo ya kifamilia

Nimejitahid sana kutatua Matatizo Kwa kadri ya uwezo wangu lakini mambo yanazidi kuwa magumu.

Ukiachana na kuhudumia familia Yangu lakini shida za Ndugu zimekuwa haziishi

Zinapokaribia tarehe za mwisho wa mwezi najikuta sina raha Kabisa maana napigiwa simu nyingi za shida na kuombwa pesa tu

Naombeni mbinu ya kukabiliana na changamoto hizi
Zima simu kuanzia tarehe 20 afu iwashe kwenye tarehe 5. Ni wakati Kila mtu ajifunze kudeal na shida zake mwenyewe tukutane kwenye shida kubwa kubwa sio mtu kakosa Hela ya k-vant anaanza kusumbua.
 
Hili ni tatizo la overpopulation inayosababisha utegemezi na umaskini mkubwa.
Pole sana mkuu, huna budi kuubeba mzigo wako.
 
Wewe endelea kuendeleza upumbav wa kusikiliza na kusaidia ndugu... Ndugu yako wa kweli ni Watoto wako, Baba, Mama na Uliozaliwa nao tumbo moja. Hao wengine wasaidie pindi wanapotaka kufa tu. Ukiendelea na huo upumbav utakufa masikini na watakucheka...
 
Wewe ndio una suluhisho sahihi. Hapa unaweza shauriwa vibaya ukapata laana kwa kushindwa kusimama katika yale unayopaswa kutenda.

Kuna jamaa alifanikiwa akajenga nyumba kubwa sana mama yake akamuhusia kuishi na nduguze mama alipokufa jamaa akauza ile nyumba na kusambaza ndugu zake ili wajitegemee. Wengi waliangaika sana baada ya kusambazwa ila jamaa naye ali suffer kinoma maana hata ile nyumba aliiuza tena mwishowe wanaye wote walikufa pia sasa kabakia na kijana mmoja naye choka mbaya sana.

Hivyo suala la ndugu ni la kuangalia sana.
Kwaiyo watoto wake wamekufa kwa sababu hakuwasaidia ndugu zake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habar Zenu

Mwenzunu nimejikuta kwenye wimbi la mawazo Baada ya kuelemewa na majukum. Baada ya Kupata kibarua nimejikuta napokea simu nyingi kuhusu Matatizo ya kifamilia

Nimejitahid sana kutatua Matatizo Kwa kadri ya uwezo wangu lakini mambo yanazidi kuwa magumu.

Ukiachana na kuhudumia familia Yangu lakini shida za Ndugu zimekuwa haziishi

Zinapokaribia tarehe za mwisho wa mwezi najikuta sina raha Kabisa maana napigiwa simu nyingi za shida na kuombwa pesa tu

Naombeni mbinu ya kukabiliana na changamoto hizi
Badilisha namba ya simu kwa miaka miwili kwanza.

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
Saidia unapoweza..usisahau nawewe una majukumu na malengo yako binafsi..usijitoe sana
 
Asante Mkuu
Hii kitu changamoto sana na wengi wanakutana nayo
Mimi binafsi nasaidia ila kuna limit
Na msimamo wangu
Mfano kuna dogo moja alikuwa kutwa anataka msaada sawa nkawa namsaidia,ila kuna mchongo nliupata gairo nkamstua nkamchomeka huko
Huko sasa nkamwambia apambane
Akifeli asitegeme mambo ya msaada
Kweli dogo mpaka sasa anakaza

Kuna ndg wengine unawasaidia maana kutwa wanalia shida,lakini utashangaa kutwa kupata mimba na
Kuzaa mimba kuzaa kha!
Aina ya ndg hao nishawakatia line
Unakuta anatmbn hko anapata mimba
Kwenye kuzaa anataka msaada alafu bwana aliyemtia mimba hata hMsumbui,hiyo nishamkataga kofi ndg mmja
Huwa naamini mambo ya kuzaa zaa bila mpangilio ni kujiletea matatizo tu
Zaa hku umejipanga

Ova
 
Pole ndg.Kwa Tanzania yetu hii sio wew peke yako mwenye hyo changamoto.Binafsi Mimi nikama wewe.Nilichofanya nikujitahid kuwasomesha madogo Kwan wakat naanza kibarua hakun aliyekuwa amemaliza walau form 4.Nashukur madogo wa3 saiv wamegraduate chuo japo ajira ndo mziki .
Nakushaur utafute namna yakuwaezesha ili wajitegemee kiuchumi.
 
Usiogope ,ndio uhalisia wa maisha yafamilia za kitanzania zenye background ya kimasikini.

Just priotize misaada, na anza kuongeza uwekezaji na kufukuzia fursa. Pia acha kijihirumia na kutaka upnewe huruma.

Kubali lawama na anza kuufunza moyo wako kufa ganzi coz kinachokutesa ni moyo wako mzuri wa utoaji ulioathiriwa na umaskini wa muda mrefu .

Badiri mtazamo juu ya maisha kisha utambue kua, hata nchi ina rasilimali nyingi ila imeshindwa kuumaliza umasikini sembuse wewe na mshahara wako huo wa laki 7?

Wakikusumbua sana Fanya Kuni PM tuyajenge
 
Watakwambia ndio ukubwa huo, najiuliza kikwete ni mkubwqa mara 2 kwangu nae anakutana na haya yangu, kisha najiuliza tena ningekuwa sina kazi, ni mtoto mdogo wa darasa la 7 wangeniomba msaada jibu hapana.

Nina uwezo nasaidia, sina navunga.. "WEMA USIZIDI UWEZO mkuu"
 
Back
Top Bottom