Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,903
- 30,243
MAJINA YA MITAA YAHIFADHI HISTORIA
Ndugu zanguni hivi sasa kuna mradi wa Anuani za Makazi (Post Code).
Naamini sote tunashausikia kwa kuwa serikali imeutangaza.
Mradi huu ulitakiwa uchukue miaka 5 lakini Rais Mama Samia ameamua huu mradi uwe "Operation Anuani za Makazi" na ukamilike kwa miezi 5 yaani January hadi May 2022.
Katika mradi huu kupitia serikali za mitaa wakazi wa wana fursa ya kubadili jina la mtaa kwa sababu maalum.
Mathalan Mtaa wa Tandamti ni mtaa akiishi marehemu Mzee Mshume Kiyate ambae mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika hakuna asiyeufahamu.
Hii ni fursa nzuri ya kubadili jina la Mtaa wa Tandamti kuwa Mtaa wa Mshume Kiyate.
Muhimu tuwafahamishe na wengine ili ikiwa ipo haja na wao wabadili majina ya mitaa yao kwa kuenzi historia ya Dar es Salaam na wazee wetu waliofanya makubwa katika mji huu.
Halikadhalika tuwazindue na wenzetu walioko mikoani wabadilo mitaa kuipa majina ya wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika.
Tanga: Rashid Heri, Sheikh Abdallah Rashid Sembe na wengineo.
Moshi: Mama bint Mwalimu, Amina Kinabo, Halima Selengia, Yusuf Olotu na wengineo.
Tabora: Bilal Rehani Waikela, Zarula bint Abdulrahman, Nyange bint Chande na wengineo.
Dodoma: Omari Suleiman, Haruna Taratibu, Alexander Kanyamala na wengineo.
Lindi: Yusuf Chembera, Salum Mpunga, Suleiman Masudi Mnonji na wengineo.
Mikindani: Msham Awadh, Ahmed Adam na wengineo.
Kilwa: Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar, Mwinyi Mcheni Omar na wengineo.
Hawa wazalendo wako wengi nchini kote ni jukumu la wakazi wa sehemu zote wawatambue hawa mashujaa waliopigania uhuru wa Tanganyika.
PICHA: Nyumba ya Ahmed Adam ndiyo nyumba aliyolala Mwalimu Nyerere safari yake ya kwanza Mikindani mwaka wa 1956.
Mwalimu Nyerere Kilwa alikuwa akilala nyumba ya Mwinyi Mcheni Omar na alikuwa akipakiwa kwenye pikipiki ya Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar kuzunguka vijijini kuitangaza TANU.
Ofisi ya kwanza ya TANU Southern Province ilikuwa nyumbani kwa Suleiman Masudi Mnonji, Makonde Street.
Ndugu zanguni hivi sasa kuna mradi wa Anuani za Makazi (Post Code).
Naamini sote tunashausikia kwa kuwa serikali imeutangaza.
Mradi huu ulitakiwa uchukue miaka 5 lakini Rais Mama Samia ameamua huu mradi uwe "Operation Anuani za Makazi" na ukamilike kwa miezi 5 yaani January hadi May 2022.
Katika mradi huu kupitia serikali za mitaa wakazi wa wana fursa ya kubadili jina la mtaa kwa sababu maalum.
Mathalan Mtaa wa Tandamti ni mtaa akiishi marehemu Mzee Mshume Kiyate ambae mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika hakuna asiyeufahamu.
Hii ni fursa nzuri ya kubadili jina la Mtaa wa Tandamti kuwa Mtaa wa Mshume Kiyate.
Muhimu tuwafahamishe na wengine ili ikiwa ipo haja na wao wabadili majina ya mitaa yao kwa kuenzi historia ya Dar es Salaam na wazee wetu waliofanya makubwa katika mji huu.
Halikadhalika tuwazindue na wenzetu walioko mikoani wabadilo mitaa kuipa majina ya wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika.
Tanga: Rashid Heri, Sheikh Abdallah Rashid Sembe na wengineo.
Moshi: Mama bint Mwalimu, Amina Kinabo, Halima Selengia, Yusuf Olotu na wengineo.
Tabora: Bilal Rehani Waikela, Zarula bint Abdulrahman, Nyange bint Chande na wengineo.
Dodoma: Omari Suleiman, Haruna Taratibu, Alexander Kanyamala na wengineo.
Lindi: Yusuf Chembera, Salum Mpunga, Suleiman Masudi Mnonji na wengineo.
Mikindani: Msham Awadh, Ahmed Adam na wengineo.
Kilwa: Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar, Mwinyi Mcheni Omar na wengineo.
Hawa wazalendo wako wengi nchini kote ni jukumu la wakazi wa sehemu zote wawatambue hawa mashujaa waliopigania uhuru wa Tanganyika.
PICHA: Nyumba ya Ahmed Adam ndiyo nyumba aliyolala Mwalimu Nyerere safari yake ya kwanza Mikindani mwaka wa 1956.
Mwalimu Nyerere Kilwa alikuwa akilala nyumba ya Mwinyi Mcheni Omar na alikuwa akipakiwa kwenye pikipiki ya Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar kuzunguka vijijini kuitangaza TANU.
Ofisi ya kwanza ya TANU Southern Province ilikuwa nyumbani kwa Suleiman Masudi Mnonji, Makonde Street.