Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

He is talking with both sides of his mouth. He is a big liar.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...awabeza-ukawa-na-kuwaita-wasaka-tonge-17.html

“Ndugu zangu wananchi, nimepigwa mishale ming sana, hata watoto amabo nimewasaidia kupata ubunge leo wanakuja kunitukana , wanasema kuwa ninagawa kura za wapinzani, hivi mtu waliyemwona hafai ana ana nguvu gani ya kugawa za kura za wapinzani?



“sisi ACT wazalendo tumekubali kuungana (kwenye ukawa) wao hawataki hapa nani mbaya? Ng’ombe anaweza kutikisa mkia lakini mkia hauwezi kumtikisa ng’ombe”



ACT wazalendo kukataliwa kwenye ukawa, hakitatetereka na juhudi za kusamabaza uzalendo kwa watanzania. Na sambamba na kujipanga na uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi octobet mwaka huu.



Source Raia mwema
 
Mtu aliyeonekana hafai anaweza vipi kugawa kura za upinzani?? Mkia hauwezi kumtikisa ng’ombe ila ng’ombe anaweza kutikisa mkia hahahahaha., mkuu panic iko wapi hapo?

Hana jipya kabakiza kulalama mitandaoni na kwenye media baada ya fungu LA kwanza toka ccm kukata na zile mil 700 bado kutoka.Inawezekana maccm yameshituka kuwa yanapoteza Pesa bure kwa huyu mchepuko wake, bora kinana arudi mzigoni tu kuliko kuwategemea hao wachumia tumbo
 
Ivi BAVICHA kwa akili zenu mnafikiri cuf na nccr watakubali kuburuzwa kama mlivyo zoea kuwaburuza? Sera ya usaliti hamkuanzia kwa zzk bali kwa hao mlioungana nao leo tena mliwaita wasaliti,mashoga na ccm b. Mnafikiri Lipumba ni mjinga au Mbatia ni mpumbavu zzk ni jembe la kisiasa msithubutu na watu tunavyosema chadema inakufa mwaka huu aturopoki ile dhambi ya kuwashuhudia uongo cuf na nccr mwaka huu ndio watawaonyesha nini maana ya adabu. Na act ni zaidi ya mnavyofikilia jiulizeni mwaka 2010 kalibia asilimia hamsini na kitu hawakupiga kura unajua kwanini? Jiulizeni mbali na kujaa kwenye mikutano ya chadema wananchi kwanini haikushinda uchaguzi? TUKUTANE OCTOBER
 
Mtu hupimwa kwa matendo yake,wote uliowataja hapo juu wamekuwa mwiba mkali kwa serikali ya ccm kabla na baada ya kuteuliwa katika nafasi zao. Hadi leo ni kati ya watu wanaoogopwa na wameifanya serikali kuwa active kwa kiwango kinachoridhisha. Pia wameendelea kupinga matendo maovu na mipango mikubwa ya kitaifa na kimataifa inayotekelezwa na serikali ya ccm pale inapoonekana kuhodhi maslahi mapana ya Kitaifa kama vile issue ya escrow na mchakato wa katiba. Usaliti wa zzk kwa cdm umedhihirishwa kwa shahidi mbalimbali ndo mana tunasema huyu akijiunga ukawa tumeamua kupalilia utawala wa ccm jambo ambalo si baya sana endapo tu tutakuliana iwe hivyo.
 
Kauli za Zitto ni za kinafiki kabisa yeye ndo aliwaambia wafuasi wake wasiishabikie Ukawa au ameshasahau.
 
Watanzania hatuna chuki binafsi na Zito bali tuna chuki kubwa kwa yale aliyotufanyia. Mengi yamesemwa juu yake lakini hajawahi kuyajibu kwa vielelezo. Hajawahi kueleza kwa ukamilifu hela aliyokuwa akiipokea toka CCM (kwa kupitia maofisa wa TISS) ilikuwa ya nini? Hajawaeleza Watanzania ukaribu wake mkubwa na mawasiliano yake na maofisa wa juu wa TISS yamekuwa yanahusu nini hasa. Mawasiliano na maofisa wa TISS yalioneshwa kwa vilelezo, na hasa yalikuwa wakati wa kipindi cha kampeni kuelekea uchaguzi.

Leo anapotaka kushirikiana na UKAWA, Watanzania watakuwa na uhakika gani kuwa nia yake kubwa siyo kutaka kujua mipango na mbinu za UKAWA kwa manufaa ya wale ambao amekuwa akiwatumikia siku zote, CCM?

Unapomtaka Zitto ajibu mashitaka yake kwa vielelezo je, wewe pamoja na mnaomtuhumu mlishawahi kuleta ushahidi tofauti na waraka uliondaliwa na viongozi wa CHADEA? Kama wameweza kumsingizia kuwa alikwenda kumchongea Mengi kwa Raisi watashindwaje kuandika uwongo waliouandika?
 
NCCR walimchukua Kafulila (Msaliti) kutoka CDM (wanafanya nae kazi UKAWA now)...CDM iliwachukua Rwakatare na Safari kutoka CUF (CCM B) wanafanya wote kazi sasa hivi kwenye UKAWA.....Zitto kafukuzwa CDM (USALITI) kahamia ACT (ameonekana akifanya mikutano na Lipumba Mtwara...Huku Kambaya akimtetea). Naamini kabisa hii itakuwa mara ya kwanza kwa CUF kuchukua mwanachama mwenye vinasaba vya CDM (Zitto) indirectly kupitia ACT kwa mwamvuli wa UKAWA. Kwenye siasa hakuna adui wa kudumu (viongozi wanajua...sisi mashabiki tunabaki kupiga domo). Read my signature kabla hujanitusi (Im stand to be corrected though)
 
mtu alliyeonekana hafai na kufukuzwa kwenye chama kwa usaliti atakaribiswa vipi tena kwenye umoja wa wanamageuzi wa ukweli??
Lakini mkuu, kwanini zzk ndio adui yenu number 1 badala ya ccm?? Au na ninyi ni mapandikizi tu kuhadaa watz?? Back to the point,cuf wanamkubali kinoma na wako tayari kushirikiana sasa ninyi mna nini nae?? Au mlitaka akalime?
 
Jiwe lililokataliwa na waashi ndilo litakuwa mzingi imara wa nyumba, mwisho wa kunukuu!
 
Mkuu itakuwaje kama NCCR, NLD na CUF watataka kushirikiana na ACT? Tatizo mnaifanya UKAWA kama CDM na CDM kama UKAWA. Hapo ndipo penye shida kubwa.

Lakini siyo Zitto alipowakataa kwanza mpaka kusema atakayeshirikiana na UKAWA Uanachama wake ACT utafutwa?Je amejirudi lini?Kwanini amekuwa kama kinyonga wa kubadilika badilika?

Kwa uhakika Zitto anafahamu bila UKAWA kura zake hazitatoshelezeka.Cha msingi badala ya kulumbana kwenye makaorido wakutane wajadiliane.

Ila ninachokiona ni UKAWA kutomwamini mwenzao,NA hii inajidhihirisha hata huku JF jinsi wanachama wa ACT walivyoagainst CDM hivyo sidhani kama itakuwa rais,unaless ZItto awape somo Wanachama wake.Ninauhakika akiwaambia hata malumbano ya ACT aginst UKAWA yataisha.

Lakini hii ya hata KENGE akiingia ACT-Wazalendo,lazima awe ametoka CDM,hawezi akawa mwanaCCM au asiye nachama ndiyo ninayoishangaa............

Na kama hawajui hili ndilo linafanya UKAWA wasiiamini ACT-Wazalendo,na pili ndiyo sababu wanitwa CCMB.
 
UKAWA ina safari ndefu ya kuifikisha Tanzania, huu sio wakati wa kurudi nyuma watanzania wanatamani kuona mabadiliko yanayotokana na upinzani na sio kuona ni vpi upinzani unadhibitiwa na kuvurugwa. UKAWA tunatarajia makubwa kutoka kwenu.
 
Back
Top Bottom