Mosi, mie sina nafasi yoyote ya uongozi kwenye ACT,hivyo siwezi kuiwakilisha ACT kwa lolote hapa.
Ni matumaini yangu ya kuwa wenye nafasi wanaingia humu na hayo maswali hayana budi kujibiwa..
Pili, tunamchagua kiongozi ambaye tunamjua, kusema Dr Slaa ni padre mstaafu sio kashfa, ni jambo la kujivunia tu na labda ndio limemjenga kuwa alivyo leo.Na kuwa na historia hiyo hakumpunguzii ata kidogo sifa ya kuwa Rais, ata kidogo.Na mie ni Mkristo pia.
Hakuna niliposema kuwa "Padre ni kashfa.. ila ninaomba ufafanuzi wako kwa hii sentensi yako.. "Dr.Slaa (padre) hatapata kura kutoka chama cha CUF".
Mimi nimekuunganisha dot na kupata maana halisi ya sentensi yako kuwa
Dr. Slaa kwa vile mtakoliki tena aliyekuwa padre hawezi kupigiwa kura na wanachama wa Cuf kwa vile wanachama wote wa Cuf ni waislamu.. Hayo ni mawazo yangu inawezekana kabisa niko "wrong" na wewe ulimaanisha kingine.. hivyo basi naomba uniambie ni nini ulichomaanisha.
Kuhusu udini hiki ndicho nilichosema,na nimekirudia mara nyingi, na mpaka leo bado ndivyo ninavyoiona Tanzania, ndio hali halisi.
Sasa kama unaona Tanzania kuna udini (kitu ambacho mimi sioni) ni kwa nini upigie debe badala ya kuupiga vita kwa nguvu zako zote. Na kuupiga piga ni pamoja na kujiepusha kuandika au kutamka maneno yenye viashiria vya udini..rejea hao juu.
Pili hivi huu udini mnao usema ni udini wa aina gani? au tunahubiriwa udini wa wanasiasa.. Sisi huku mitaani hakuna udini Juzi hapa tumetoka kumzika jirani yetu mwislamu na katika hayo mahudhurio kulikuwa waislamu na wakristo.
Sio hilo tu hapa ninapoongea wiki hijayo kuna harusi ya kiislam mwaliko nimeishaletewa. Katika kukua kwangu sijawahi kubaguliwa sehemu yeyote ile au kuhisi ninagabuliwa kwa ajili ya dini yangu. Sasa basi labda nyie mnao sema kuna udini naomba utwambie jinsi mlivyobaguliwa/kunyanyaswa kwa ajili za dini zenu au hata ndugu jamaa na marafiki zenu.. Naomba msiniambie maswala ya serikali na mahospital au msinipe mambo ya wanasiasa maana hawa watu wanatumia teke hlii kwa ajili ya matumbo yao. (hapa naomba ushuhuda wako wewe kama wewe kwa nini unahisi kuna udini)
...............................................................................................................................................................................
Kuna mtihani mwingine muhimu sana utaikabili UKAWA na watapaswa wauvuke.Mahakama ya Kadhi, upande wa CUF na wafuasi wao hili ni jambo muhimu sana lakini upande wa Chadema hili jambo ni nuksi, kuna mtihani mkubwa sana hapo kuziridhisha pande zote.Kila mtu anaweza akawa aliona kuwa bunge lililopita ilipofika hoja ya kadhi hakukuwa na UKAWA, ilikufa kwa muda.Sasa kwenye uchaguzi mkuu wafuasi wa CUF watataka wathibitishiwe hilo kuwa wakitoa kura inawekwa kwenye katiba??na ukiahidi hivyo utawaelezeje wa upande wa pili?
Swala la mahakama ya kadhi ni swala rahisi sana ila linakuzwa na wanasiasa kwa minajili ya matumbo yao kama nilivyokwisha sema hapo juu..
Mimi kama Alinda sina tatizo na Mahakama ya kadhi na nafikiri ili ni kwa wakristo wengi tu (ok kuna wakristo wengine wanalipinga maana hakuna kitu kinaweza kukubaliwa na watu wote) Ila tatizo linapofika kwa wanasiasa wanaligeuza kuwa mitaji..
Na ninafikiri kama serikali ingekuwa na nia kweli na mahakama ya kadhi basi ingetoa elimu kwa wale watu ambao wana wasi wasi, na baada ya hapo ni kukaa chini pande nne yaani wakristo, waislamu, serikali na wataalum wa aina mbali mbali (km sheria, mausiano,dini na nk.) hawa watu wakikaa chini bila kuingiliwa na wanasiasa ni matumaini yangu wangeleta muhafaka.
Tukumbuke mahakama ya kadhi haizuiriki tena cha muhimu ni kukaa pamoja kama ndugu, kama watanzani na kama wataka kupata muhafaka na mwisho wa siku hakuna lisilowezekana chini ya jua..
Na hiki kitu kwa viongozi wa Ukawa sina shaka nalo watatoka na muhafaka maana waislamu hawako Cuf tu, Waislamu wako Chadema, wako CCM wako CUf, wako Nccr na nk. na mashabiki wa chadema sio wakristo tu au mashabiki wa Cuf sio waislamu tu.
Kikwete aliongea kuhusu suala la udini kwenye uchaguzi uliopita.Nakubaliana 100% na Kikwete udini ulikuwepo sana kwenye uchaguzi ule, uzalendo sio kujifanya kipofu, ni kuyatambua matatizo tulio nayo, kuyakubali na kuyafanyia kazi.Nasikitika tu kuwa pamoja na Kikwete kuyatambua mapema baada ya uchaguzi ule hajafanya lolote kurekebisha hali hiyo na kufuta isijirudie tena hali ile.Anaondoka madarakani akiliacha taifa palepale.Hapa amefeli vibaya.
Ni kweli Kikwete aliliongelea na nilitegemea kuwaona wagombea urais wote kwa pamoja wakikataa kura za ubaguzi iwe ni kwa Dr.Slaa au Mh. Kikwete na nk. "kama unanipigia kura kwa vile mimi Slaa ni mkristo basi wewe kaa nyumbani kura yako sitaki.. kama unanipigia kura kwa vile mimi ni Wiislamu basi kaa nyumbani kura yako sitaki. Ila kwa bahati mbaya sana hiki kitu sikukiona na sio Kikwete tu aliyesema kuhusu udini hata MH. ZItto Kabwe alisema kuwa alipata kura ndogo kwa vile wakristo hawakumpigia kura (kitu kama hicho ila sikumbuki) ila Sikusikia Zitto akikataa kura za waislam wanaotaka kumchagua kwa ajili ya dini yake.. Sasa kama ni kweli mimi sijui, kama ni hisia tu na hapo sijui, kwa bahati mbaya sana mimi kama Alinda mwaka 2005 nilimpigia kura Mh.Kikwete na 2010 nilimpigia kura Slaa kwa vile rais wangu alini-let down kwa swala zima la kushughulikia mafisadi.
Nawatambua watu kadhaa ambao ni wapinzani wa jadi wa CCM lakini ilibidi wampigie kura Mkapa badala ya Prof Lipumba mwaka 2000, na kuna wengine ambao katu hawataweza kumpigia kura Dr Slaa kwa misingi hiyohiyo.Hizi element zipo kwenye jamii japo tunaweza tusipende ata kuziongelea.Tusijifanye hatuzioni.Tuzifanyie kazi
Hilo ni kweli kuna watu wa CCM wanaowapigia kura vyama vya upinzani na kuna wanachama wa vyama vya upinzani wanapigia CCM. HIvyo basi inategemea swala hili unaliangalia kwa jicho lipi ukiliangalia kwa jino la udini utaona kuna udini, lakini inawezekana hao watu waliona hoja za Prof. Lipumba ndo jibu la matatizo yao...au walimuelewa vizuri prof. Lipumba kuliko Mkapa. Ukitumia mfn huo mwaka 2005 (kama sikosei) Mbowe alipata kura chache sana kulinganisha na Prof. Lipumba hivyo basi kama udini ungekuwepo basi walao Mbowe angekuwa mshindi wa pili.. yaani Mh. Kikwete angegawana kura na Pro. Lipumba.
Tukiangalia matokeo ya mwaka 2010 utaona DR. Slaa alipata kura 2ml sasa unataka kusema katika hizo kura 2ml kulikuwa hakuna kura za waislamu? au Mh. Kikwete hakuna kura za wakristo? Kasumba ya watanzania hawajawahi kuchagua mtu kutoka na dini yake labda huku mbeleni..
Tuupinge udini wa nguvu zetu zote, maana watakao kuja kupata shida ni watoto zetu.. na huu ujumbe auone kaka yangu @Mkandara maana naona taratibu anaelekea kwenye janga la dini. Tusiangalie kitu kwa jicho la ubaguzi na kwa ili Mkandara wewe ni mfn mzuri maana unaishi nje ya Tanzania na ninafikiri unafahamu kama mtu ukianza kuangalia kitu kwa jicho la ubaguzi basi inawezeka kabisa paka kakupita na kukuangali na wewe ukasema "huyu paka ameniangalia sana kwa vile mimi ni mkristo, wiislamu, au mwafrika.
................................................................................................................................................................
TUUNGANE WOTE KUPAMBANA NA HAYA, KUJIFANYA HAYAPO NI KUJIDANGANYA WENYEWE,TULIFANYIE KAZI, TULIPONYE TAIFA