Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

..mgogoro wa Zitto na CDM ni wa muda mrefu sana.

..kuna wakati CDM waliunda kamati ya kujaribu kupata muafaka na Zitto ilimradi aendelee kuwepo CDM.

..mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo alikuwa ni mama mzazi wa Zitto Kabwe.

..sasa mpaka hapo utaona kwamba CDM walimpenda na kumthamini Zitto, tatizo ni kwamba yeye mwenyewe hapendeki na hathaminiki.

..Pamoja na hizi tuhuma za usaliti, Zitto Kabwe anaamini kwamba ana akili kuwazidi viongozi wote wa CDM. Kutokana na imani yake hiyo anaamini kwamba yeye ndiye anayepaswa kuwa Mwenyekiti na Kiongozi mkuu na siyo hao "vilaza."

JokaKuu, hizi ni siasa, uzushi, na propaganda za kisiasa ambazo zipo sikuzote na hazitakwisha.

Tutoke huko, tusonge mbele.Chadema wana safari yao na ACT na Zitto wana safari yao, ni safari mbili tofauti.Historia itakuja kuandika ni nani alikuwa sahihi kati yao, ni mapema sana sasa.

Ata uchaguzi wa rais ungefanyika mwaka 2008 Lowassa asingekuwa tishio kabisa, lakini vip leo?ndio siasa.Yawezekana kabisa msaliti wako wa leo akawa shujaa wako wa kesho.Vuta subira.Muda utaongea.
 
Aisee Zitto ana akili nyingi zingekuwa zinagawiwa ninge muomba ampimie kilo moja Mnyika na Mbowe wagawane!

Kijana yuko makini na ni mzalendo wa kweli...

Taabu kweli wee! Siamini kama huo ndo mwisho wa uwezo wako. Unaamini Zitto ana akili! Mtu ambaye anaamua kwenda kusema kwa rais mambo ya watu wengine bila hata kuulizwa!

Huyu Zitto wako anaweza akafanikiwa kisiasa na akawa tajiri, lakini hyo isiwe ajabu maana hata wajinga hufanikiwa.
 
Zitto kama Sitta


13th December 2010



email.png

Email



printer.png

Print



comment_bubble.png

Comments





headline_bullet.jpg
Sasa aundiwa kamati kama ya mpasuko CCM
headline_bullet.jpg
Yaongozwa na Profesa Baregu, wengine watatu
headline_bullet.jpg
Ni baada ya wabunge wenzake kumtosa



Zitto1(12).jpg

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe


Wingu zito limetanda kuhusu hatma ya kisiasa ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, baada ya kunusurika kufukuzwa katika nafasi yake ya Unaibu Katibu Mkuu wa chama hicho kufuatia wabunge wenzake wa chama hicho kupiga kura ya kutokuwa na imani naye.


Hali hiyo inakuja zikiwa zimepita siku mbili tangu wabunge wa chama hicho wamvue Zitto nafasi ya Naibu Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni kwa tuhuma za kusaliti maamuzi halali ya chama hicho.


Hata hivyo, jaribio hilo la kumwondoa kwenye nafasi hiyo lilishindikana baada ya Kamati Kuu kumwokoa kwa kukataa kura ya kutokuwa na imani naye badala yake kamati hiyo ikaelekeza asikilizwe kwanza kabla ya kuadhibiwa. Habari kutoka ndani ya chama hicho zilisema kuwa wabunge walitaka kumtosa Zitto kutokana na kutofautiana na msimamo wa chama chake wa kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete Novemba 17, mwaka huu.


Kamati Kuu ya (Chadema) imeunda kamati ya jopo la wazee wa chama chini ya Profesa Mwesiga Baregu kumsikiliza Zitto na matatizo yake na viongozi wengine wa chama ili kuleta suluhu ndani ya chama. Jopo hilo lina wajumbe wanne ambao ni Shida Salum, Kitila Mkumbo ambaye ni Katibu, Profesa Baregu na mjumbe mmoja aliyejulikana kwa jina moja Shilungushela.


Akizungumza na NIPASHE jana, Profera Baregu alikiri kuwa ni kweli amepewa jukumu hilo na Kamati Kuu kwa ajili ya kutafuta amani ndani ya chama hicho hasa kumsuluhisha Zitto na wabunge wenzake.
Alisema tayari wameanza kujipanga kwa ajili ya kuwakutanisha wabunge wa chama hicho na Zitto ili kuweka mambo sawa ingawa hakutaja watakutana lini na wapi.


“Sijui tutakutana lini lakini itakuwa hivi karibuni bado tunajipanga tukutane na Zitto tumsikilize matatizo yake na kazi yetu ni kujenga uhusiano mwema ndani ya chama, tunataka amani itawale, ” alisema Profesa Baregu.


Hata hivyo, Profesa Baregu hakuwa tayari kuzungumzia jaribio la kumfukuza Zitto katika wadhifa wake ndani ya chama hicho na kutaka aulizwe Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa. “Hayo ya Kamati Kuu yanamhusu Katibu Mkuu ndiye anayeweza kuyazungumzia,” alisema Profesa Baregu.


Habari hizo zilisema kuwa Kamati Kuu ya chama hicho imemtambua Rais Jakaya Kikwete kama Rais halali na kuagiza wabunge kushiriki shughuli zote za kitaifa.
Alipotafutwa kuthibitisha habari hizo, Dk. Slaa, alisema anatarajia kukutana na waandishi wa habari kwa ajili ya kuelezea yaliyojiri kikao cha Kamati Kuu.


“Kikao chetu kiliisha usiku sana sasa tunaandaa tamko na tutawapa, sijajua kama tutaweza kukutana na ninyi leo au la lakini tutawaarifu,” alisema Dk. Slaa.
Alipotafutwa ili atoe maoni yake, Zitto alisema yeye bado ni mgonjwa na yuko kitandani hivyo hawezi kuzungumza lolote kuhusu masuala hayo ya kisiasa.


"Mimi bado naumwa hivi hapa niko kitandani nyumbani siwezi kuzungumza masuala hayo kwanza sijui chochote kinachoendelea," alisema Zitto.
Sakata la Zitto linafanana na lile la aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambalo lilisababisha kuundwa kwa kamati iliyokuwa ikiongozwa na Rais wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi.


Wajumbe wengine wa kamati hiyo walikuwa ni Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa. Kamati hiyo ya CCM ilionekana kumlenga moja kwa moja Sitta, ambaye baadhi ya wanachama wa chama hicho walikuwa wakimshutumu kuwa ndiye aliyesababisha mpasuko ndani ya chama hicho.


Jina la Sitta liliondolewa na Kamati Kuu kwenye orodha ya wanaowania nafasi ya Spika na badala yake yalipitishwa majina ya wanawake watatu ambao ni Anne Makinda, Anna Abdallah na Kate Kamba na majina yao yalipopelekwa kwenye Kamati ya Wabunge wa CCM, Anne Makinda aliibuka mshindi wa kiti cha Uspika. Sitta kwa sasa ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

NB:

..angalieni juhudi zilizofanywa na CDM kujaribu kumrudisha kundini Zitto.

..mpaka wanamuweka mama yake mzazi, mwalimu wake na mentor wake chuo kikuu, rafiki yake wa karibu Kitila Mkumbo ktk kamati ya usuluhishi, kweli mnataka kusema CDM hawakuwa na nia ya kumshawishi Zitto aendelee kuwa nao?

cc getrusa, Kapwela, Mkandara, Nguruvi3







 
Last edited by a moderator:
Taabu kweli wee! Siamini kama huo ndo mwisho wa uwezo wako. Unaamini Zitto ana akili! Mtu ambaye anaamua kwenda kusema kwa rais mambo ya watu wengine bila hata kuulizwa!

Huyu Zitto wako anaweza akafanikiwa kisiasa na akawa tajiri, lakini hyo isiwe ajabu maana hata wajinga hufanikiwa.

Unaweza ukanitajia walau binadamu mmoja asiye mjinga?binafsi sijawahi kumuona wala kumsikia
 
JokaKuu,
Sijakuelewa maana ya hoja hiyo hapo juu ulikuwa unamaanisha nini au uilitaka kusema nini haswa..

..nilichotaka ni kuonyesha juhudi zilizofanywa na CDM kumrudisha Zitto ktk mstari.

..kuna habari za CDM kuunda kamati ya usuluhishi iliyomhusisha Prof.Baregu, Prof.Kitila Mkumbo, Mzee Shilungushela, na Bi.Shida Salum[r.i.p]--mama mzazi wa Zitto Kabwe.

..Kama CDM walikuwa hawamthamini Zitto Kabwe, basi wasingefanya juhudi zote hizo kutafuta suluhu. Tena ktk kuhakikisha kwamba anatendewa haki wakamteua mama mzazi wa Zitto Kabwe kuwepo ktk kamati ya usuluhishi.

cc Kimweri, Kapwela, Nguruvi3, Alinda, Mchambuzi, getrusa
 
Last edited by a moderator:
..nilichotaka ni kuonyesha juhudi zilizofanywa na CDM kumrudisha Zitto ktk mstari.

..kuna habari za CDM kuunda kamati ya usuluhishi iliyomhusisha Prof.Baregu, Prof.Kitila Mkumbo, Mzee Shilungushela, na Bi.Shida Salum[r.i.p]--mama mzazi wa Zitto Kabwe.

..Kama CDM walikuwa hawamthamini Zitto Kabwe, basi wasingefanya juhudi zote hizo kutafuta suluhu. Tena ktk kuhakikisha kwamba anatendewa haki wakamteua mama mzazi wa Zitto Kabwe kuwepo ktk kamati ya usuluhishi.

cc Kimweri, Kapwela, Nguruvi3, Alinda, Mchambuzi, getrusa
Mkuu haya hayatakiwi kuongelewa! Kinachotakiwa kusemwa na kusika ni ''Zitto kaonewa, kafukuzwa bila sababu''

Mkuu unakumbuka hoja ya ukaguzi wa CAG, aliyeibua ni Zitto. Kumbe wakati huo waraka ulikuwa jikoni!
Haya hayasemwi, ni taboo! tunachotakiwa kuamini ni kufukuzwa kwa ukanda baasi.
 
Unaweza ukanitajia walau binadamu mmoja asiye mjinga?binafsi sijawahi kumuona wala kumsikia

Tunaishi kijiji kimoja? Ninayemfahamu nawe unamfahamu? Una habari kwamba dunia ina zaidi ya watu bilioni 7?

naona unatafuta sababu ya kujiita mjinga kwa hiyo imani yako.
 
Mkuu JokaKuu,
Mie bado ninasubiri vyanzo vya mapato vya ACT wazalendo.. Walituhadi mwenyewe tena kwa mbwembwe kweli kuwa mapato na matumzi yataletwa kila baada ya miezi 3 humu humu Jamii forum..

Cha kusikitisha sasa tunakwenda mwenzi wa 10 hakuna cha mapato na matumizi na tukuulza wanasema tumamuulie Mzee Mtei kule Tengeru..

Yaani huyu kijana ni mjengo hoja kweli kweli, na ni msomi Tanzani nzima hakuna... Ila isije kuwa tumeisha uzwa kwa Andrea Codes (Ujerumani)Maana wanasiasa hawaminiki kama alivyowahi sema wenyewe (Husimwamini wana siasa- by Zitto Kabwe)

Pia tunasubiri kuona mali na madeni ya viongozi wa ACT.. Mwigamba na mama Mwenyekiti Zingatieni katiba ya ACT..
.Aione Mkandara :shocked::shocked: na Kapwela
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JokaKuu,
Mie bado ninasubiri vyanzo vya mapato vya ACT wazalendo.. Walituhadi mwenyewe tena kwa mbwembwe kweli kuwa mapato na matumzi yataletwa kila baada ya miezi 3 humu humu Jamii forum..

Cha kusikitisha sasa tunakwenda mwenzi wa 10 hakuna cha mapato na matumizi na tukuulza wanasema tumamuulie Mzee Mtei kule Tengeru..

Yaani huyu kijana ni mjengo hoja kweli kweli, na ni msomi Tanzani nzima hakuna... Ila isije kuwa tumeisha uzwa kwa Andrea Codes (Ujerumani)Maana wanasiasa hawaminiki kama alivyowahi sema wenyewe (Husimwamini wana siasa- by Zitto Kabwe)

Pia tunasubiri kuona mali na madeni ya viongozi wa ACT.. Mwigamba na mama Mwenyekiti Zingatieni katiba ya ACT..
.Aione Mkandara :shocked::shocked: na Kapwela

Kuna sehemu nimeona na alwatan Nguruvi anaongelea Hummer, nikabaki kushangaa tu?ata huyu?? na hapa tena kichwa ninachokikubali sana Alinda anaongelea hiyo bold tena!!dah..inakuwaje watu ambao kwa fikra zao wanapaswa kuaminika lakini nao wanabeba tu na kukomaa na propaganda?vip sasa masela wa kitaa??kwa hiyo bold unaweza ukafanya watu wayachukulie yote uliyoandika hapo kama ni utani tu.

Kimsingi huu ni uthibitisho kuwa siasa zetu so far zimeshindwa kabisa kuleta tija, kwa siasa hizi hatutaweza kutumia kwazo kupata viongozi bora bali tutaishia tu ile ya "wacha na wengine wale tu", hapa ndipo vyama vilivyopo vilipotufika, uzushi,porojo na propaganda umekuwa ndio msingi wa siasa za Tanzania.

Watanzania wanastahili zaidi ya hivi,wacha tuendelee kutafuta tumaini.Tutafika tu.
 
Tunaishi kijiji kimoja? Ninayemfahamu nawe unamfahamu? Una habari kwamba dunia ina zaidi ya watu bilioni 7?

naona unatafuta sababu ya kujiita mjinga kwa hiyo imani yako.

Ebu angalia kamusi yako maana ya MJINGA, tunajifunza kila siku.
...............................................................................................................................................................................
Nimejikuta nimekumbuka kipande cha hekima za Mwenyekiti wa Kijiji chetu.Japo ni nje ya mada, nisamehe kushare nawe neno la ufahamu


  • Ndugu Zangu,

    KUNA tofauti ya mjinga na mpumbavu. Marehemu Mzee Jongo alipata kutamka; " Kusoma sio kuufuta ujinga, bali ni kuupunguza". Kila mwanadamu ana ujinga wa jambo moja au mia moja. Kuwa na ujinga wa jambo si kosa, hata Profesa anaweza asijue namna ya kuchochea kuni za kuchomea hindi bichi likachomeka. Kijana wa darasa la saba anaweza kuwa hodari wa jambo hilo kumshinda Profesa.

    Lakini upumbavu ni ile hali ya mwanadamu kufanya jambo isivyotakiwa huku akiwa na uelewa wa namna ya kufanya inavyotakiwa. Huo ndio upumbavu. Na ndio maana binadamu kuitwa mpumbavu ni tusi. Kuitwa mjinga si tusi, kila mmoja ana ujinga wake. Kuwa na ujinga wa jambo fulani ni kutoelewa jambo hilo. Ni nani anayeelewa kila jambo?

    Na mwanadamu unafanyaje unapoamka na kukuta dunia unayoishi ardhi yake imeanza kumegeka na kuchotwa na bahari? Kuna niliyemwuliza swali hilo. Naye akanijibu; " Huo ndio utakuwa mwisho wa dunia!" Aliyenijibu alikuwa amechoka kufikiri. Nilidhani amgetamka, kuwa angeanza kujifunza kuogelea. Maana, kwa kuogelea majini angeweza kukutana na kisiwa, au nchi kavu.

    Wanadamu tumejaliwa akili ili tuweze kufikiri. Na kufikiri ndio njia mojawapo ya kuiteka kweli. Kufikiri kunahamisha milima na hata kuiweka kando kuruhusu mwanga upite. Inakuwaje basi mwanadamu anapoacha kufikiri? Na hilo ni Neno La Leo.

    Maggid
    Iringa,
    Jumanne, Machi 22, 2011
    http://mjengwa.blogspot.com



 
Mkuu JokaKuu,
Mie bado ninasubiri vyanzo vya mapato vya ACT wazalendo.. Walituhadi mwenyewe tena kwa mbwembwe kweli kuwa mapato na matumzi yataletwa kila baada ya miezi 3 humu humu Jamii forum..

Cha kusikitisha sasa tunakwenda mwenzi wa 10 hakuna cha mapato na matumizi na tukuulza wanasema tumamuulie Mzee Mtei kule Tengeru..

Yaani huyu kijana ni mjengo hoja kweli kweli, na ni msomi Tanzani nzima hakuna... Ila isije kuwa tumeisha uzwa kwa Andrea Codes (Ujerumani)Maana wanasiasa hawaminiki kama alivyowahi sema wenyewe (Husimwamini wana siasa- by Zitto Kabwe)

Pia tunasubiri kuona mali na madeni ya viongozi wa ACT.. Mwigamba na mama Mwenyekiti Zingatieni katiba ya ACT..
.Aione Mkandara :shocked::shocked: na Kapwela
Mbona vyanzo vipo ofisi kuu mlishaambiwa. hata mimi nikitaka vya Chadema nitaambiwa niende Ufipa au unadhani wanaweza vianika humu?.. Tuwe wakweli jamani hata wewe nikikuuliza vyanzo vyako mwenyewe utaanza hadithi...
 
..nilichotaka ni kuonyesha juhudi zilizofanywa na CDM kumrudisha Zitto ktk mstari.

..kuna habari za CDM kuunda kamati ya usuluhishi iliyomhusisha Prof.Baregu, Prof.Kitila Mkumbo, Mzee Shilungushela, na Bi.Shida Salum[r.i.p]--mama mzazi wa Zitto Kabwe.

..Kama CDM walikuwa hawamthamini Zitto Kabwe, basi wasingefanya juhudi zote hizo kutafuta suluhu. Tena ktk kuhakikisha kwamba anatendewa haki wakamteua mama mzazi wa Zitto Kabwe kuwepo ktk kamati ya usuluhishi.

cc Kimweri, Kapwela, Nguruvi3, Alinda, Mchambuzi, getrusa
Mkuu umeisoma hiyo kwa makini au? maana wanazungumzia wao kutoka Bungeni wakati wa Kuapishwa JK.. come on now! tulipinga wengine humu JF kitendo hicho kwa sababu utaratibu upo na unalazimika kuufuata. Mnapopinga matokeo ya NEC ni hatua ya kwanza, kisha kuna mahakama mna kuachia Mahakama itoe maamuzi, nao wakisha amua mshindi nani basi huna jinsi. JK ni mteuliwa tu huwezi kumgomea yeye kuwa rais badala ya system nzima ilikuwa aibu tupu.

Mara nyingi sana kutomtambua rais ni kutoyatambua matokeo, sasa wanapokwenda Bungeni kama Wabunge walotambua matokeo yao, halafu inapokuja swala la rais unatoka nje. Unafiiri ingekuwaje kama Chadema wangeingia Bungeni CCM waka walk out? kwa sababu hawatambui baadhi ya wabunge wake. Mnaweza sema namtete ZZK lakini kama kweli chama kingeendelea na kutomtambua toka atangazwe na wakaweka mikao mahakamani,watu wakakusanyika kama Misri vile kupinga matokeo ya NEC hapo ningesema kweli Chadema imeiva na inataka mabadiliko. lakini upuuzi ule utanisamehe mkuu hata mimi nisingetoka.

Hii ya Bunge la katiba nisingetoka maana unaawachia nafasi CCM bure kabisa kutengeneza katiba yao kisha unaiita katiba ya Chenge! wewe ulikuwa wapi ilihali umekula hela za wananchi halafu una ujasiri wa kutoka unapopenda kama vile Katiba itatokana na uamuzi wako, tena wmnatumia Uchama kuitana Ntarahamwe yaani Katika ilikuwa ya vyama sio ya wananchi. Sina baya na Chadema lakini wakati mwingine inaonekana kabisa Akili ndogo kuongoza Akili kubwa..
 
Mbona vyanzo vipo ofisi kuu mlishaambiwa. hata mimi nikitaka vya Chadema nitaambiwa niende Ufipa au unadhani wanaweza vianika humu?.. Tuwe wakweli jamani hata wewe nikikuuliza vyanzo vyako mwenyewe utaanza hadithi...

Kwa hiyo ACT wanafanya kama Chadema? Pia ukumbuke Chadema,CCM, Cuf, Nccr na nk. hawakuwahi kutuahidi kuleta vyanzo vya mapato humu Jf.

Swala vyanzo vya mapato walilisema wao tena kwa mbwembwe kweli, Hawakusema huwa anayetaka aende ofisini, walisema kuwa kila baada ya miezi 3 watakuwa wanaleta na kweli miezi 3 ya kwanza walileta uzi huku humu..

Mie huwa nasimamia katika ukweli sipendi siasa za ulaghai ukisema kitu ni lazima ukiteleze au kama unaona hautakiteleza basi kaa kimya... ahadi ni deni Act leteni vyanzo na matumizi ya chama.. tunakwenda mwezi wa 10 sasa...


KItu kingine ninamkumbusha Katibu mkuu, Mama mwenyekiti na viongozi wote wa ACT kwa ujumla watangaze mali zao kama katiba inavyotamka pia wasihau kutuletea humu dani tuone kama alivyofanya kiongozi wao.. ahadi ni deni.
 
Kwa hiyo ACT wanafanya kama Chadema? Pia ukumbuke Chadema,CCM, Cuf, Nccr na nk. hawakuwahi kutuahidi kuleta vyanzo vya mapato humu Jf.

Swala vyanzo vya mapato walilisema wao tena kwa mbwembwe kweli, Hawakusema huwa anayetaka aende ofisini, walisema kuwa kila baada ya miezi 3 watakuwa wanaleta na kweli miezi 3 ya kwanza walileta uzi huku humu..

Mie huwa nasimamia katika ukweli sipendi siasa za ulaghai ukisema kitu ni lazima ukiteleze au kama unaona hautakiteleza basi kaa kimya... ahadi ni deni Act leteni vyanzo na matumizi ya chama.. tunakwenda mwezi wa 10 sasa...


KItu kingine ninamkumbusha Katibu mkuu, Mama mwenyekiti na viongozi wote wa ACT kwa ujumla watangaze mali zao kama katiba inavyotamka pia wasihau kutuletea humu dani tuone kama alivyofanya kiongozi wao.. ahadi ni deni.
Nani aloahidi kuleta vyanzo vya mapato humu JF ebu nikumbushe?
 
  • Thanks
Reactions: kdc
Kuna sehemu nimeona na alwatan Nguruvi anaongelea Hummer, nikabaki kushangaa tu?ata huyu?? na hapa tena kichwa ninachokikubali sana Alinda anaongelea hiyo bold tena!!dah..inakuwaje watu ambao kwa fikra zao wanapaswa kuaminika lakini nao wanabeba tu na kukomaa na propaganda?vip sasa masela wa kitaa??kwa hiyo bold unaweza ukafanya watu wayachukulie yote uliyoandika hapo kama ni utani tu.

Kimsingi huu ni uthibitisho kuwa siasa zetu so far zimeshindwa kabisa kuleta tija, kwa siasa hizi hatutaweza kutumia kwazo kupata viongozi bora bali tutaishia tu ile ya "wacha na wengine wale tu", hapa ndipo vyama vilivyopo vilipotufika, uzushi,porojo na propaganda umekuwa ndio msingi wa siasa za Tanzania.

Watanzania wanastahili zaidi ya hivi,wacha tuendelee kutafuta tumaini.Tutafika tu.


Mkuu Kapwela yaani unasahau mara hii kuwa wewe ndo kinara wa siasa za propaganda (kukumbusha tu Dr. Slaa (Padre) hawezi kuchaguliwa na Cuf...)

Hapo hakuna propaganda kama vyanzo vya mapato havijulikani na wanao vijua hawataki kusema basi kuna kitu ambacho hakiko sawa "somewhere" Maana sioni kwanini kunakuwa na kigugumizi katika hili.

Na ni wajibu wenu/wao (wana ACT) kututoa hizo wasi wasi na njia ya kutoa hizo wasi wasi ni kuleta wafadhali wa hicho chama. Walau kwa hili wawaige wenzao Chadema maana Chadema huwa tunaambiwa au hata kupiga picha kabisa na wafadhili wao.

Pia kutofanya hivyo mnaua/wanaua dhana mzima wa ACT wazalendo. Uwazi.. Maana uwazi ndo huo lini,wapi, na nani alichangia ACT.. tendeni mnachohubiri.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu haya hayatakiwi kuongelewa! Kinachotakiwa kusemwa na kusika ni ''Zitto kaonewa, kafukuzwa bila sababu''

Mkuu unakumbuka hoja ya ukaguzi wa CAG, aliyeibua ni Zitto. Kumbe wakati huo waraka ulikuwa jikoni!
Haya hayasemwi, ni taboo! tunachotakiwa kuamini ni kufukuzwa kwa ukanda baasi.

..nilichotaka ni kuonyesha juhudi zilizofanywa na CDM kumrudisha Zitto ktk mstari.

..kuna habari za CDM kuunda kamati ya usuluhishi iliyomhusisha Prof.Baregu, Prof.Kitila Mkumbo, Mzee Shilungushela, na Bi.Shida Salum[r.i.p]--mama mzazi wa Zitto Kabwe.

..Kama CDM walikuwa hawamthamini Zitto Kabwe, basi wasingefanya juhudi zote hizo kutafuta suluhu. Tena ktk kuhakikisha kwamba anatendewa haki wakamteua mama mzazi wa Zitto Kabwe kuwepo ktk kamati ya usuluhishi.

cc Kimweri, Kapwela, Nguruvi3, Alinda, Mchambuzi, getrusa

JokaKuu, tukianza kurudi huko nyuma hatutafika.Mshukuruni kuwa Zitto amekomaa sasa kisiasa kwa sasa na amekubali kusamehe yaliyopita anaiachia nature ichukue mkonod, maana ukweli utafika tu ata kama utachelewa.Muda utaongea tu na makamanda wa kuchonga watajulikana tu.

Kwa kuwa umeleta habari ya Mama Zitto,Mungu amrehemu; ebu soma maelezo yake juu ya mgogoro wa viongozi wa Chadema na mwanae.Nimeweka tu kwa kumbukumbu ya Mama Zitto kwa sababu ya wewe kumingiza hapo juu,tusijadili haya yaliyopita.Muda wenyewe utatupa majibu, am sure miaka minne ijayo kama tutakuwa hai, kila mmoja naturally atakuwa kaishaujua ukweli.Tuache nature ifanye kazi.
................................................................................................................................................................................
‘Nilikuwa naomba Mungu kila siku ili afukuzwe Chadema' - Mama Zitto

Dar es Salaam.
Siku moja baada ya Kamati Kuu ya Chadema kumvua uongozi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Taifa wa chama hicho, Zitto Kabwe, mama yake mzazi, Shida Salum ametoa ya moyoni akieleza kuwa kilichomkuta mwanaye kimefunika mabaya mengi yaliyopangwa afanyiwe.

"Kwa upande wangu naona kama ni ushindi kwa Zitto kutokana na jinsi ninavyojua hali ilivyo, mambo yalikuwa ni mengi mno na nikwambie tu, Zitto kuvuliwa uongozi kumefunika hayo yaliyokuwa yamekusudiwa kufanywa dhidi yake. Nilikuwa naomba Mungu kila siku ili afukuzwe Chadema," alisema mama huyo wakati akizungumza na gazeti hili nyumbani kwake Tabata, Dar es Salaam.

Shida Salum alisema kuwa Mungu amemnusuru mwanaye na kusisitiza, "Watu walikaa na kutengeneza ripoti ya siri kuhusu Zitto na kuiweka kwenye mtandao kisha kuituma kwa wanachama wa Chadema wanaowafahamu. Mpaka wanafikia hatua hiyo maana yake ni kwamba wamejaribu njia zote za kummaliza, lakini wameshindwa."

Katika ufafanuzi wake wa jana, Shida aliwataka wanachama wa Chadema kuwa watulivu "Siku nyingi walikuwa wanamwinda na hata hilo jambo ambalo Chadema wanasema amefanya, hawana uhakika nalo."


Alisema tangu siku nyingi ndani ya Chadema kulikuwa na mpango wa kumng'oa Zitto, akifafanua kuwa hata katika kikao cha Kamati Kuu iliibuliwa hoja ya ruzuku za vyama, huku wajumbe wakimshutumu Zitto kwamba kwa nafasi yake na Naibu Katibu Mkuu alitakiwa kuitetea Chadema kuhusu ruzuku.

Katika vikao vya Kamati ya PAC, Zitto aliingia katika malumbano na chama chake baada ya kutuhumu vyama vya siasa kuwa hesabu zake hazikaguliwi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), huku akitaka ruzuku kwenye vyama hivyo isimamishwe.

"Zitto alipoingia katika kikao cha Kamati Kuu alishikilia msimamo wake kwamba kama Chadema inachukia ufisadi, nacho lazima kihakikishe kinakaguliwa," alisema na kuongeza;

"Wao wanaona ili waweze kusalimika katika suala hili la ruzuku ni lazima wamfukuze Zitto. Chadema hawako sawa, hesabu zao haziko sawa."

"Zitto anahusishwa na kitu ambacho Chadema hawana uhakika nacho, ukiusoma ule waraka katika aya ya mwisho umeandikwa hivi, ‘Huyu mtu tunayefikiria awe mwenyekiti hajaoa, tumshauri aoe akikataa tutafute mtu mwingine', maana yake ni kwamba waraka huo ulikuwa haujamfikia Zitto, kama ungekuwa umemfikia Zitto watu hao wasingemwomba Zitto agombee uenyekiti.

Alisema wakati Kikao cha Kamati Kuu kikifanyika Zitto alikuwa nje ya nchi na kwamba yeye alimshauri kuhakikisha kuwa anahudhuria kikao hicho.
"Alipotua tu na ndege aliniambia kuwa kuna foleni na alitaka kukodi pikipiki ili awahi kikao, aliniambia lazima aende ili kujua hatima yake"


Aliacha gari lake na kwenda na hata mimi nilimsisitizia kwamba ni lazima aende katika kikao," alisema. Alisema kuwa Zitto alipofika katika kikao hicho aliweza kuzima hoja zote zilizomhusu ikiwamo ya ruzuku za vyama, kwamba baadhi ya wajumbe walipoona amebadili mwelekeo wa kikao, mjumbe mmoja (akamtaja kwa jina) aliibua waraka uliomng'oa Zitto katika wadhifa wake.


"Unajua Kamati Kuu ilijadili zaidi kuhusu ruzuku. Hata ule waraka uliongezwa maneno baada ya baadhi ya wanachama kumpora Mwigamba laptop yake alipokuwa mkoani Arusha katika kikao cha Chadema," alisema.

Huku akiwataja wanachama wa Chadema walioongeza maneno katika waraka huo (wakiwamo wabunge wawili) na viongozi wa ngazi za juu wa Chadema, mama Zitto alisema kilichomkuta mwanaye ni ushindi mkubwa, kwamba alipangiwa kufanyiwa makubwa zaidi ya yaliyomkuta.

"Hakuna amani maana ukisikia kengele inagongwa hapa nyumbani unasema hao ndiyo wamekuja kumuua Zitto nini, hivi sasa mpaka walinzi wanaolinda hapa wakisikia unakuja nyumbani kwa Zitto lazima wakuandike jina na kukufuatilia," alisema mama huyo.



‘Nilikuwa naomba Mungu kila siku ili afukuzwe Chadema’ - Mama Zitto - Kitaifa - mwananchi.co.tz
 
Mkuu Kapwela yaani unasahau mara hii kuwa wewe ndo kinara wa siasa za propaganda (kukumbusha tu Dr. Slaa (Padre) hawezi kuchaguliwa na Cuf...)

Hapo hakuna propaganda kama vyanzo vya mapato havijulikani na wanao vijua hawataki kusema basi kuna kitu ambacho hakiko sawa "somewhere" Maana sioni kwanini kunakuwa na kigugumizi katika hili.

Na ni wajibu wenu/wao (wana ACT) kututoa hizo wasi wasi na njia ya kutoa hizo wasi wasi ni kuleta wafadhali wa hicho chama. Walau kwa hili wawaige wenzao Chadema maana Chadema huwa tunaambiwa au hata kupiga picha kabisa na wafadhili wao.

Pia kutofanya hivyo mnaua/wanaua dhana mzima wa ACT wazalendo. Uwazi.. Maana uwazi ndo huo lini,wapi, na nani alichangia ACT.. tendeni mnachohubiri.

Mosi, mie sina nafasi yoyote ya uongozi kwenye ACT,hivyo siwezi kuiwakilisha ACT kwa lolote hapa.

Pili, tunamchagua kiongozi ambaye tunamjua, kusema Dr Slaa ni padre mstaafu sio kashfa, ni jambo la kujivunia tu na labda ndio limemjenga kuwa alivyo leo.Na kuwa na historia hiyo hakumpunguzii ata kidogo sifa ya kuwa Rais, ata kidogo.Na mie ni Mkristo pia.

Kuhusu udini hiki ndicho nilichosema,na nimekirudia mara nyingi, na mpaka leo bado ndivyo ninavyoiona Tanzania, ndio hali halisi.
...............................................................................................................................................................................

  • Kuna mtihani mwingine muhimu sana utaikabili UKAWA na watapaswa wauvuke.Mahakama ya Kadhi, upande wa CUF na wafuasi wao hili ni jambo muhimu sana lakini upande wa Chadema hili jambo ni nuksi, kuna mtihani mkubwa sana hapo kuziridhisha pande zote.Kila mtu anaweza akawa aliona kuwa bunge lililopita ilipofika hoja ya kadhi hakukuwa na UKAWA, ilikufa kwa muda.Sasa kwenye uchaguzi mkuu wafuasi wa CUF watataka wathibitishiwe hilo kuwa wakitoa kura inawekwa kwenye katiba??na ukiahidi hivyo utawaelezeje wa upande wa pili?

    Kimsingi CUF na Chadema hazipo compatible, kama wakienda pamoja kwenye uchaguzi chama kimojawapo baada ya uchaguzi kitarudi mtaani na kukuta washabiki wake hawapo tena, wamehamia vyama vingine.

    Kikwete aliongea kuhusu suala la udini kwenye uchaguzi uliopita.Nakubaliana 100% na Kikwete udini ulikuwepo sana kwenye uchaguzi ule, uzalendo sio kujifanya kipofu, ni kuyatambua matatizo tulio nayo, kuyakubali na kuyafanyia kazi.Nasikitika tu kuwa pamoja na Kikwete kuyatambua mapema baada ya uchaguzi ule hajafanya lolote kurekebisha hali hiyo na kufuta isijirudie tena hali ile.Anaondoka madarakani akiliacha taifa palepale.Hapa amefeli vibaya.


    Nawatambua watu kadhaa ambao ni wapinzani wa jadi wa CCM lakini ilibidi wampigie kura Mkapa badala ya Prof Lipumba mwaka 2000, na kuna wengine ambao katu hawataweza kumpigia kura Dr Slaa kwa misingi hiyohiyo.Hizi element zipo kwenye jamii japo tunaweza tusipende ata kuziongelea.Tusijifanye hatuzioni.Tuzifanyie kazi​
    ................................................................................................................................................................

TUUNGANE WOTE KUPAMBANA NA HAYA, KUJIFANYA HAYAPO NI KUJIDANGANYA WENYEWE,TULIFANYIE KAZI, TULIPONYE TAIFA
 
Back
Top Bottom