Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

Hata ukimuuliza Chenge atajibu sera ya CCM ni ujamaa. Wenye akili ndogo wanadhani nchi hii ina tatizo la sera tu.
Chenge ni mjamaa kama MM wenu, Lowasa ni mjamaa kama MM wenu, Rugemalila ni mjamaa kama MM wenu
View attachment 245912 View attachment 245913

Kusema tu sera yangu ni ujamaa haijawahi kuwa tatizo kwa akina Chenge kama ambavyo sio tatizo kwa MM.

Kwahiyo unakiri kuwa hujui sera za chama chako na huihitaji kujua??

Ndicho nilichomwambia jamaa yangu hapa chini, wanachama wengi wa vyama vya siasa ata hawajui vyama hivyo vinasimamia nini, wanachojua ni majina ya watu na matukio, basi.

Kwa wale waliosomea mambo ya project management kuna kitu kinaitwa RAID. Pamoja na mambo mengine, project yoyote inakubidi kuidentify risk zinazoweza kuadhiri project yenyewe kuisha on time and within the budget. Kati ya risk kubwa nayoiona ndani ya ACT "WAZALENDO" ni kumtegemea ZZK kama kiongozi pekee mwenye mvuto na anayeweza kusikilizwa na kueleweka machoni mwa watanzania! Binafsi simuoni kiongozi yoyote ndani ya chama hichi anayeweza kusimama mwenyewe bila msaada au support. Hii ni risk kubwa kwa chama cha kisiasa kuwekeza kwa binadamu badala kutegemea sera na itikadi ya chama! Siombi jambo baya limtokee kwa ZZK, ZZK ni binadamu leo yupo kesho ametangulia mbele ya HAKI.

Nafikiri unaweza kuona hapo juu.Ni mfano halisi wa wanachama na ata viongozi wa vyama vingine hapa nchini.Sikuhizi siasa zimekuwa ni kama mipasho, mkutano mzima wa siasa ata uwe ni masaa mawili, huwezi kusikia suala la sera wala nini, ni majina ya watu na matukio mwanzo mwisho.

Ndio maana kwenye hili ACT wapo mbele ya vyama vingine vya upinzani.Kwenye mikutano ya ACT asilimia walau 50 za hotuba zao ni sera na aina ya nchi wanayotaka kuijenga.Lakini ukienda mikutano ya Chadema kwa mfano asilimia 99.9% za hotuba zao ni majina ya watu na matukio.
 
“Mwanzo walipotufukuza walituambia tukatafute vyama vingine hilo likafanyika, tulipopata vyama vya kufanyia siasa wakasema vipo kwa ajili ya kugawa upinzani, tukasema tupo tayari kuunganisha Nguvu ya pamoja kwa ajili kuiondoa CCM wenzetu pia hili hawalitaki sasa ni wajibu wenu kutambua watu gani hawataki kuiondoa CCM.

Wananchi watambue tuna nia ya dhati lakini wenzetu wanaweka ugomvi binafsi mbele ya maslahi ya Taifa. Sisi ACT wazalendo bado tupo taayari kushirikiana kwa mujibu wa misingi. Shabaha yetu ni moja tu kubomoa mfumo wa uchumi wa kinyonyaji na kifisadi ili kujenga uchumi shirikishi wa wananchi”

By Zitto kabwe kupitia Twiter

I wish you knew how much you are known.
 
Mkuu wangu, sijui kama hujaona kuwa hizo mbili zinagongana.Zitto hakutaka kuondoka Chadema, alifukuzwa.Option ya kubaki hakuwa nayo.

Sasa yeye ni mwanasiasa, na kwa umri wake hawezi kustaafu leo, hivyo hakuwa na namna zaidi ya kutafuta uwanja wa kuendeleza harakati zake za kisiasa

Sasa kwa kuwa kuna hili suala la kugawanya kura, ndio maana Zitto akasema kama hizo kura zipo (maana wengine wana shaka ata juu ya hili maana wanaona hana impact kisiasa), kama zipo, basi kwa ajili ya CCM kuondoka madarakani yupo tayari kuepusha hilo kwa kushirikiana na UKAWA kwenye uchaguzi huu ili kutogawanya kura.

Sasa Kwa kutangaza hivyo, yeye kajisafisha juu ya suala la kugawa kura.Ni hilo tu.

Maana zaidi ya hapo sioni Zitto afanye nini zaidi ili kuepusha kugawanya kura?au mnataka Zitto atangaze kuwa anavunja chama na astaafu siasa?maana sioni tumlaumu kwa lipi zaidi ya hapo.

Kwa Chadema kama hawahitaji umoja na Zitto, waende kwenye uchaguzi kwa nguvu na wafute hiyo impact ya Zitto, wakishindwa basi hilo litakuwa sio kosa la Zitto bali itakuwa ni kosa la kufanya maamuzi kwa jazba bila kuangalia mbali.
Kapwela,

..Zitto alifukuzwa kwa usaliti na mwenendo wake wa kudharau viongozi wake ktk chama.

..kama angekuwa na nia ya dhati ndani ya moyo wake kubaki CDM basi asingejihusisha na mambo hayo.

..kwa mtizamo wangu, it is too early kwa UKAWA na ACT kuanzisha mahusiano ya aina yoyote ile wakati huu.
 
Last edited by a moderator:
Kapwela,

..Zitto alifukuzwa kwa usaliti na mwenendo wake wa kudharau viongozi wake ktk chama.

..kama angekuwa na nia ya dhati ndani ya moyo wake kubaki CDM basi asingejihusisha na mambo hayo.

..kwa mtizamo wangu, it is too early kwa UKAWA na ACT kuanzisha mahusiano ya aina yoyote ile wakati huu.

Hilo la usaliti ni relative term, maana ata Nelson Mandela nae alikuwa kwenye list ya magaidi hatari duniani kwa mujibu wa USA, ata Martin Luther King alikuwa mtu anayehatarisha amani kabla hajawa shujaa.So sio ajabu, kila mtu anaweza akawa na definition tofauti tofauti ya vitu.

Kwenye issue ya kufukuzwa, ni kweli kafukuzwa, sasa what next??ni kweli ushirikiano ni mapema sana hivyo Zitto akae mbali kabisa na Chadema kwenye uchaguzi huu, sio kwa sababu Zitto hataki lakini kwa sababu Chadema hawataki.

Sasa utamlaumu vip Zitto kwa kura (kama zitakuwepo) ambazo Chadema watazikosa kwa kitendo cha Zitto kwenda kwenye uchaguzi kivyake?ndio maana nilikuuliza sasa unataka ACT na Zitto waachane na siasa kwa sababu Chadema itapunguza kura??hutamtendea haki kumlaumu kwa hilo.

Ndugu yangu, mwaka 1992 tulipata ruksa ya kuwa na vyama vingi, na singi wa siasa hiyo ni ushindani wa vyama ili wananchi wachague aliye bora miongoni mwao, ebu tuache vyama vyote viingie vishindane, ndio maana ya mfumo huu.Na itapendeza zaidi ACT ikipata mgombea urais mwenye nguvu, tupate mpambano mzuri mwezi wa 10.Ili tuendapo kwenye uchaguzi isiwe wawili tu wanashindana bali ata mshindi wa pili tusiwe na uhakika ni nani.
 
Hilo la usaliti ni related term, maana ata Nelson Mandela alikuwa nae alikuwa kwenye list ya magaidi hatari duniani kwa mujibu wa USA, ata Martin Luther King alikuwa mtu anayehatarisha amani kabla hajawa shujaa.So sio ajabu, kila mtu anaweza akawa na definition tofauti tofauti ya vitu.

Kwenye issue ya kufukuzwa, ni kweli kafukuzwa, sasa what next??ni kweli ushirikiano ni mapema sana hivyo Zitto akae mbali kabisa na Chadema kwenye uchaguzi huu, sio kwa sababu Zitto hataki lakini kwa sababu Chadema hawataki.

Sasa utamlaumu vip Zitto kwa kura (kama zitakuwepo) ambazo Chadema watazikosa kwa kitendo cha Zitto kwenda kwenye uchaguzi kivyake?ndio maana nilikuuliza sasa unataka ACT na Zitto waachane na siasa kwa sababu Chadema itapunguza kura??hutamtendea haki kumlaumu kwa hilo.

Ndugu yangu, mwaka 1992 tulipata ruksa ya kuwa na vyama vingi, na singi wa siasa hiyo ni ushindani wa vyama ili wananchi wachague aliye bora miongoni mwao, ebu tuache vyama vyote viingie vishindane, ndio maana ya mfumo huu.Na itapendeza zaidi ACT ikipata mgombea urais mwenye nguvu, tupate mpambano mzuri mwezi wa 10.Ili tuendapo kwenye uchaguzi isiwe wawili tu wanashindana bali ata mshindi wa pili tusiwe na uhakika ni nani.

..wakulaumiwa ni Zitto kwa tabia zake za usaliti na kutokuheshimu viongozi wake.

..Mandela aliwaheshimu sana wenzake, haswa Mzee Oliver Tambo. kwa hiyo ni makosa kumtaja ktk sentensi moja na Zitto Kabwe aliyepatikana na hatia ya kukisaliti chama chake.
 
..wakulaumiwa ni Zitto kwa tabia zake za usaliti na kutokuheshimu viongozi wake.

..Mandela aliwaheshimu sana wenzake, haswa Mzee Oliver Tambo. kwa hiyo ni makosa kumtaja ktk sentensi moja na Zitto Kabwe aliyepatikana na hatia ya kukisaliti chama chake.

Jibu langu bado ni lile lile, usaliti ni relative term, inategemea na mtazamo binafsi wa mtu.Hivyo upo entitled kwa definition yako.

Ndio maana wakati kwa definition zetu Nelson Mandela alikuwa shujaa lakini kwa definition za USA,Nelson Mandela huyohuyo kwa matendo yaleyale alikuwa gaidi hatari sana, kundi moja na Osama Bin Laden.

Wakati sie tunasema Mandela kaenda jela kwa kutetea haki za wanyonge wengine wakasema kiongozi wa kundi la magaidi wa ANC ameswekwa ndani.Ndio ilivyo siku zote.Lazima kuwe na fikra tofauti vinginevyo dunia itakuwa inaboa sana.

Na msingi ni kuwa mwenye nguvu(power) yupo right wakati wote, hana kosa, lakini aliyeshindwa ndiye mkosefu na asiyefaa.Hii ni principle ya kawaida kwenye kisiasa na utawala, kwa Tanzania kwa mfano Kambona angefanikiwa kumpindua Nyerere basi Kambona angekuwa hero na Nyerere angekuwa Msaliti wa Uhuru, Mapinduzi ya Zanzibar yasingefanikiwa akina Shmate wangekuwa mashujaa na Karume na wenzake wangebaki kwenye historia kama maharamia wasiofaa kwenye jamii lakini sababu walifanikiwa kibao kimewageukia wenzao.Ipo hivyo wakati wote.

Lakini msingi wa jumla, hakuna definition ambayo ni universal, definition yoyote inaishia tu kwa mtu au kundi fulani, nje ya hapo inakuwa invalid.
 
Kwahiyo unakiri kuwa hujui sera za chama chako na huihitaji kujua??

Ndicho nilichomwambia jamaa yangu hapa chini, wanachama wengi wa vyama vya siasa ata hawajui vyama hivyo vinasimamia nini, wanachojua ni majina ya watu na matukio, basi.



Nafikiri unaweza kuona hapo juu.Ni mfano halisi wa wanachama na ata viongozi wa vyama vingine hapa nchini.Sikuhizi siasa zimekuwa ni kama mipasho, mkutano mzima wa siasa ata uwe ni masaa mawili, huwezi kusikia suala la sera wala nini, ni majina ya watu na matukio mwanzo mwisho.

Ndio maana kwenye hili ACT wapo mbele ya vyama vingine vya upinzani.Kwenye mikutano ya ACT asilimia walau 50 za hotuba zao ni sera na aina ya nchi wanayotaka kuijenga.Lakini ukienda mikutano ya Chadema kwa mfano asilimia 99.9% za hotuba zao ni majina ya watu na matukio.

"...nitakuwa wa mwisho kutoka CHADEMA" - Nani alitoa kauli hiyo, na kwa nini alikuwa anajiapiza kwa chama ambacho hakina sera? au ndo mmegundua baada ya Msaliti Mkuu kutoka?
 
Jibu langu bado ni lile lile, usaliti ni relative term, inategemea na mtazamo binafsi wa mtu.Hivyo upo entitled kwa definition yako.

Ndio wakati kwa definition zetu Nelson Mandela alikuwa shujaa lakini kwa definition za USA,Nelson Mandela huyohuyo kwa matendo yaleyale alikuwa gaidi hatari sana, kundi moja na Osama Bin Laden.

Ila msingi mwingine ni kuwa hakuna definition ambayo ni universal, bali inaishia tu kwa mtu au kundi fulani, nje ya hapo inakuwa invalid.


..mimi sikumbuki kusikia au kusoma Nelson Mandela akituhumiwa kwa makosa ya usaliti kwa chama chake cha ANC.

..pia sikuwahi kusikia au kusoma Nelson Mandela akiwajihusisha na mwenendo wa kuigawa ANC, na kuwadharau viongozi wake.

..mimi nazungumzia usaliti wa Zitto, pamoja na ukosefu wake wa heshima kwa viongozi wake. hakuna mahali nimezungumzia ugaidi. nakuomba urudi kwenye mada iliyopo mbele yetu.
 
ndo mtaji wao, wafanye nini sasa maana front line kuna Lema, Sugu na mchungaji.. hiyo ndo think tank team ya ndugu zetu, mbowe anaikubali hatari.

Siwapendi watu wanaopoteza muda wao mwingi kujadiri watu binafsi badala ya kujadiri matukio. Hukumu ni Oktoba hapo ndipo kwenye mbichi na mbivu, lakini mara Lema, Sugu, Zitto ya kazi gani. Tuzungumzie mambo yanayoendelea huko mikoani, hayo ndiyo yatakayosaidia kushinda uchaguzi mkuu. Wasi wasi na uzoefu wangu hawa ambao hawaridhiki mpaka wawataje watu binafsi kwa majina wala si wapiga kura bali ni wapiga gumzo.
 
"...nitakuwa wa mwisho kutoka CHADEMA" - Nani alitoa kauli hiyo, na kwa nini alikuwa anajiapiza kwa chama ambacho hakina sera? au ndo mmegundua baada ya Msaliti Mkuu kutoka?

Ata kauli hiyo hukuiona ndugu?alisema "nitakuwa wa mwisho kutoka chadema KWA HIARI YANGU", nadhan unaelewa maana ya hiari yangu, ZITTO ALIFUKUZWA CHADEMA nje ya hiari yake.

Ni wapi Zitto kasema Chadema haina sera?hakuna chama kisicho na misingi na sera zake.Na hapa hatujaongela popote juu ya vyama kutokuwa na sera.Think bro

Naamini hilo swali lako hapo chini uliisha jisomea na kujua kuwa ni wewe hukuwa na taarifa, kwa kuwa sasa unajua nenda uwaelekeze na wengine.Ni vizuri kuwa aware na siasa zinavyokwenda.

We unaishi wapi? mbona yalishawahi kuwa front page Mwa.n.a..ha..lis.i mkuu? tatizo Msaliti Mkuu (MM) hajawahi kujibu ili majibu yake pia yawekwe front page
 
..mimi sikumbuki kusikia au kusoma Nelson Mandela akituhumiwa kwa makosa ya usaliti kwa chama chake cha ANC.

..pia sikuwahi kusikia au kusoma Nelson Mandela akiwajihusisha na mwenendo wa kuigawa ANC, na kuwadharau viongozi wake.

..mimi nazungumzia usaliti wa Zitto, pamoja na ukosefu wake wa heshima kwa viongozi wake. hakuna mahali nimezungumzia ugaidi. nakuomba urudi kwenye mada iliyopo mbele yetu.

Joka kuu, nimekupa mifano hapa muhimu sana ambayo unaweza kui-apply popote.

Tuje South Africa, nimekwambia principle muhimu ya power, Aliyeshinda ndiye hutengeneza historia, sasa Mandela amekuwa mshindi ndani ya ANC atakuwaje tena msaliti??

Mwaka 1959, chama cha ANC kiligawanyika, kundi moja likiongozwa na Prof Sobukwe likaanzisha chama cha PAC, wao walikuwa wanaona ANC ni rahini sana kwa wazungu, wao walitaka Afrika kusini isiyo na wazungu.Kilipata nguvu sana na kama unakumbuka mauaji wa wanafunzi South Africa miaka ya 60s, amabyo yamewekwa kama kumbukumbu ya mtoto wa Afrika sio ANC waliohusika na maandamano yale,ni PAC.

Sasa PAC wangefanikiwa kuja kuibuka kidedea na kuchukua utawala South Afrika, Mandela asingekuwa shujaa alivyo leo badala yake shuja angekuwa Prof Sobukwe, lakini leo hakuna mtu anamjua Sobukwe.ANAYESHINDA NDIYE ANAYETENGENEZA HISTORIA.http://www.southafrica.info/about/history/robert-sobukwe-overview.htm#.VTkEhSFViko

Kingine, je unaamini kuwa Mandela alikuwa gaidi?sasa kwanini taifa kubwa kama Marekani liseme Mandelea gaidi kama sio gaidi?kwa mtazamo wako maana yake anachosema Mkubwa ni sahihi, lakini kwa mfano wa Mandela hapa unaona kumbe ata mkubwa anaweza kuwa wrong,japo kwa wakati wake/kwenye kundi lake definition anayoitaka mkubwa itakubaliwa.

Jibu langu bado ni lile lile, usaliti ni relative term, inategemea na mtazamo binafsi wa mtu.Hivyo upo entitled kwa definition yako.

Ndio maana wakati kwa definition zetu Nelson Mandela alikuwa shujaa lakini kwa definition za USA,Nelson Mandela huyohuyo kwa matendo yaleyale alikuwa gaidi hatari sana, kundi moja na Osama Bin Laden.

Wakati sie tunasema Mandela kaenda jela kwa kutetea haki za wanyonge wengine wakasema kiongozi wa kundi la magaidi wa ANC ameswekwa ndani.Ndio ilivyo siku zote.Lazima kuwe na fikra tofauti vinginevyo dunia itakuwa inaboa sana.

Na msingi ni kuwa mwenye nguvu(power) yupo right wakati wote, hana kosa, lakini aliyeshindwa ndiye mkosefu na asiyefaa.Hii ni principle ya kawaida kwenye kisiasa na utawala, kwa Tanzania kwa mfano Kambona angefanikiwa kumpindua Nyerere basi Kambona angekuwa hero na Nyerere angekuwa Msaliti wa Uhuru, Mapinduzi ya Zanzibar yasingefanikiwa akina Shmate wangekuwa mashujaa na Karume na wenzake wangebaki kwenye historia kama maharamia wasiofaa kwenye jamii lakini sababu walifanikiwa kibao kimewageukia wenzao.Ipo hivyo wakati wote.

Lakini msingi wa jumla, hakuna definition ambayo ni universal, definition yoyote inaishia tu kwa mtu au kundi fulani, nje ya hapo inakuwa invalid.
 
Unaweza kuthibitisha bila shaka ni vipi CCM wanamuandalia mikutano yake??!au unameza na kukalilishwa tu.. umri wako unafananaje?! ZITTO kasema mna chuki Binafsi je hili si la kweli?! Alipokua chadema mlimuona mzigo hata kwenye Machungu yake haumkushtuka nani kati yenu Bavicha alieshiriki hata msiba.!? Halafu mnajifanya watanzania?!wa wapi ..... watz tuna utu.. upendo... na ushirikiano.. katika matatizo na furaha..!!mnataka tushabikie chama kisichojua Utu wala Fadhira..? Kwenu nyinyi mwanachama akifa mko radhi aliwe na mbwa barabarani na sio kuzikwa.. is it how the politics is..?? No sioni ajabu kwanini Shonza na wenziwe waliondoka chadema.. Mna Roho Mbaya na Wabinafsi.. akija mtu kujibu ajibu na hili la Msiba pia.
Kama umezungumzia shonza sina comment!! kama unawaunga mkono sina comment. Msiba ulikuwepo wewe? Acha majungu nani hukumuona! The political issue of content is ZZK is a deadly traitor!! He has not being able to dispute this!! All the evidences are crystal clear!!
 
Kapwela,

..unarudi kule kule.

..mgogoro kati ya ANC na PAC haukuhusisha masuala ya usaliti.
 
Last edited by a moderator:
Noel2014 tafadhali sana! Wakati CHADEMA wamemtimua Zitto Kabwe mlikuja na hoja kuwa ndani ya CDM hakuna demokrasia eti kwanini wamemtimua huyo Ayatola wenu, sasa kwa muktadha huohuo naomba unijibu kwanini CCM wamemtimua HASSAN NASSORO MOYO uanachama kule ZNZ!? Hiyo ndiyo demokrasia au kunya anye kuku akinya bata anaambiwa kaharisha!?
 
Kapwela,

..Zitto alifukuzwa kwa usaliti na mwenendo wake wa kudharau viongozi wake ktk chama.

..kama angekuwa na nia ya dhati ndani ya moyo wake kubaki CDM basi asingejihusisha na mambo hayo.

..kwa mtizamo wangu, it is too early kwa UKAWA na ACT kuanzisha mahusiano ya aina yoyote ile wakati huu.

Ninashangaa!! Alikuwa na nia ya dhati?! Mwanasheria mkuu wa chama alitangaza kuwa zitto kafukuzwa Chadema. Na si hivyo tu.. kwa mujibu wa maelezo ya zitto alikuwa sudani kusini.. kikazi akaja ili ajitetee kwenye kikao cha kamati kuu ya chama akaambiwa kikao kilisha fanya maamuzi.. je hayo hayakumbukwi nanyi watu wa chadema?! Mtu gani anahukumiwa bila kusikilizwa?! Leo mmemfukuza wenyewe mnamwita msaliti.. how?!
 
Last edited by a moderator:
Kapwela,

..unarudi kule kule.

..mgogoro kati ya ANC na PAC haukuhusisha masuala ya usaliti.

Naona tunarudi palepale

Jibu langu bado ni lile lile, usaliti ni relative term, inategemea na mtazamo binafsi wa mtu.Hivyo upo entitled kwa definition yako.

Na msingi ni kuwa mwenye nguvu(power) yupo right wakati wote, hana kosa, lakini aliyeshindwa ndiye mkosefu na asiyefaa.Hii ni principle ya kawaida kwenye kisiasa na utawala, kwa Tanzania kwa mfano Kambona angefanikiwa kumpindua Nyerere basi Kambona angekuwa hero na Nyerere angekuwa Msaliti wa Uhuru, Mapinduzi ya Zanzibar yasingefanikiwa akina Shamte wangekuwa mashujaa na Karume na wenzake wangebaki kwenye historia kama maharamia wasiofaa kwenye jamii lakini sababu walifanikiwa kibao kimewageukia wenzao.Ipo hivyo wakati wote.

Lakini msingi wa jumla, hakuna definition ambayo ni universal, definition yoyote inaishia tu kwa mtu au kundi fulani, nje ya hapo inakuwa invalid.
 
Ninashangaa!! Alikuwa na nia ya dhati?! Mwanasheria mkuu wa chama alitangaza kuwa zitto kafukuzwa Chadema. Na si hivyo tu.. kwa mujibu wa maelezo ya zitto alikuwa sudani kusini.. kikazi akaja ili ajitetee kwenye kikao cha kamati kuu ya chama akaambiwa kikao kilisha fanya maamuzi.. je hayo hayakumbukwi nanyi watu wa chadema?! Mtu gani anahukumiwa bila kusikilizwa?! Leo mmemfukuza wenyewe mnamwita msaliti.. how?!

..mgogoro wa Zitto na CDM ni wa muda mrefu sana.

..kuna wakati CDM waliunda kamati ya kujaribu kupata muafaka na Zitto ilimradi aendelee kuwepo CDM.

..mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo alikuwa ni mama mzazi wa Zitto Kabwe.

..sasa mpaka hapo utaona kwamba CDM walimpenda na kumthamini Zitto, tatizo ni kwamba yeye mwenyewe hapendeki na hathaminiki.

..Pamoja na hizi tuhuma za usaliti, Zitto Kabwe anaamini kwamba ana akili kuwazidi viongozi wote wa CDM. Kutokana na imani yake hiyo anaamini kwamba yeye ndiye anayepaswa kuwa Mwenyekiti na Kiongozi mkuu na siyo hao "vilaza."
 
.

..mimi nazungumzia usaliti wa Zitto, pamoja na ukosefu wake wa heshima kwa viongozi wake.

JokaKuu, unaweza kuona hapa jinsi "usaliti" ilivyo relative term, definition yako haiwezi kuwa sawa na ya getrusa.

Ninashangaa!! Leo mmemfukuza wenyewe mnamwita msaliti.. how?!

Na ndio maana nikakwambia definition hiyo haiwezi kuwa sawa kwa kila mtu.

J
Lakini msingi wa jumla, hakuna definition ambayo ni universal, definition yoyote inaishia tu kwa mtu au kundi fulani, nje ya hapo inakuwa invalid.

Na ndio uzuri wa demokrasia, tuwape wanachi machaguzi zaidi, mwisho wa siku historia zao zitakapoandikwa atakayeshinda miongoni mwao atakumbukwa kama shujaa na atakayeshindwa miongoni mwao ataandikwa kama msaliti/dhaifu/mbinafsi/asiye na maono ya kisiasa n.k

Hivyo wacha Chadema na ACT waende wote kwenye uchaguzi, Chadema watasema Zitto msaliti na ACT watasema Zitto Shujaa na Mzalendo, mwisho wa siku wananchi watachagua.Ni kila mmoja kai yao atawajibika binafsi kwa matokeo atakayoyapata.

Zitto akishindwa asiwalumu Chadema na Chadema wasipofikia malengo wasimlaumu Zitto, ni wananchi watakaokuwa wameongea.Ndio siasa.Ubishi wa kisiasa haumalizwi na viongozi bali na wananchi.
 
Kama umezungumzia shonza sina comment!! kama unawaunga mkono sina comment. Msiba ulikuwepo wewe? Acha majungu nani hukumuona! The political issue of content is ZZK is a deadly traitor!! He has not being able to dispute this!! All the evidences are crystal clear!!

Majungu teh teh teh... nchi yoyote akienda JK akaonekana watasema watanzania walikuwepo.. kama sie basi kuna mwakilishi. Akionekana lipumba twaweza sema CUF walikuwepo... pia Akiwepo Mbowe ni rahc kusema chadema walikuwepo... kati ya hao nani ulimuona wewe Mnyika,Mbowe, Slaa, au... anyway dhamira huwa ba jibu zuri zaidi katika maisha ya mwanadamu. Endeleeni na dhamira zenu zikiwa huru. Mtakuwa huru kinyume na hapo... mtahangaika sana . Coz u can fool sm pple smtym bt not all the pple all the tym.
 
Back
Top Bottom