Ndugu yangu kuna siku ukweli utafahamika tuuu. Kila siku watakuja na hoja tofauti kuhalalisha kuwa wanachokisema ni kweli japo wenyewe wanajua fika kuwa ni uongo. Ni wazi kuwa hata Lissu hataki dereva ahojiwe pamoja na kumfundisha mambo ya kuongea karibu mwaka mzima. Usishangae wakasema dereva ameomba hifadhi ya kisiasa huko aliko. Na ikilazimika akaja TZ naona uwezekano wa hao hao kumwuua na kusingizia serikali. Naamini mpango ulisukwa na Lissu na wenzake ili ashambuliwe ila wenzake kama kawaida yao wakabadilisha gear angani wakawaambia wale washambuliaji wammalize kabisa. Sasa Lissu atapenda hiyo ifahamike? Na wale wenzake watapenda ifahamike? Ni wazi dereva alihusishwa na wanaona anaweza kutoa siri. Fikiria gharama inayotumika kumficha huyu dereva. Karibu mwaka mzima amekaa nje ya TZ akifundishwa ya kuzungumza pindi akihojiwa na serikali. Ikitokea wakaamini kuwa hajafuzu watamwondoa tu ili kuepuka aibu.