Majibizano ya Rais Samia na Spika yanaweza kuleta Anarchy!

Majibizano ya Rais Samia na Spika yanaweza kuleta Anarchy!

Paul Alex

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2012
Posts
4,346
Reaction score
9,846
Kwanza kabisa walaumiwe walioliharibu Bunge...hapa list ni ndefu ila Spika Ndugai hawezi kukwepa hizi lawama, pamoja na Polepole, Bashiru, Mwendazake, n.k
Hawa wamesababisha majadiliano yaliyopaswa kufanyika bungeni yafanyike mtaania...
Na hili ni tatizo maana mijadala ya mitaani ni unguided, uninformed na endless...

Nimeligusa hilo hapo juu kidogo maana kimsingi ndio lililozalisha huu mjadala wa 'mikopo na nchi kupigwa mnada' kati ya Rais Samia na Spika - Ndugai.
Nitagusia kidogo huu mjadala kisha nitamalizia na athari zake kwa imani ya wananchi juu ya watu wanaowaongoza.

1. Deni letu la taifa lina usiri mkubwa sana. Hapa Nape aliwahi kusema kuna haja ya kulifanyia 'audit' na kutafuta thamani ya fedha kwenye miradi mikubwa ya maendeleo inayoendelea. Hoja hii ikawa chungu kuliko 'mbilimbi' na mara moja ikazalisha timu ya 'wahuni' na 'viroboto'. Kama kawaida hoja ikageuka kioja na baadae ikafa kifo cha kawaida..japo umuhimu wa hoja yenyewe utaendelea kuwa hai.

2. Mama Samia ameongelea 'concession loans' zitakazoanza kulipwa baada ya miaka 20. Ukweli ni kwamba;
● Baada ya hiyo miaka 20 mama hatakuwa madarakani na hivyo sio yeye atakayelipa hayo madeni. Najua pia na yeye analipa madeni ya nyuma...HAPA...hapa ni pakiangalia sana. Utaratibu wa kiongozi kutengeneza tatizo leo litakalokuja kuonyesha makali wakati hayupo madarakani sio utaratibu mzuri kwasababu haya matatizo yatakua juu ya wananchi na vizazi vyao.
● Rais atakayekuwepo baada ya miaka 20 atahitaji pia kufanya miradi ya maendeleo kutokana na uhitaji wa jamii wakati huo, je itakuwaje? Miradi inayotegemewa kulipa hii mikopo ni pamoja na Ule wa umeme wa bwawa la Nyerere ambao kwakweli nina mashaka nao sana.. mvua ikigoma pale tutavuna tu kambale ambao sidhani kama watalipa deni. Kuna ule mwingine wa Shirika la Ndege ulioanza kuingiza hasara kabla hata haujaanza..big doubt!

3. Kauli ya Ndugai kwamba hii nchi itapigwa mnada.. hii ni alert kubwa sana kutoka kwa kiongozi wa mhimili wa bunge. Hii ni kengele ya hatari.
Ila kama kuna viongozi wa ajabu nchi hii nadhani Ndugai amewazidi wote.. yeye binafsi ameitia nchi hasara, misimamo yake imekuwa ikitegemea hali ya hewa ya siku hiyo. Huyu ameshiriki kugeuza bunge kuwa kituko na kutengeneza msingi wa maamuzi mabovu mengi ambayo mwendazake aliyafanya. Wakati wote deni linakuwa alikuwa akiangalia na kukaa kimya... leo miradi iko katikati ya utekelezaji na uchumi ukiwa umeyumba vibaya, anataka wananchi watozwe ili kuikamilisha... sasa sijui watatozwa nini??

Yote kwa pamoja, majibizano ya 'titi for tati' kati ya rais na spika wa bunge hayana afya kwa ustawi wa taifa...
Haya majibizano yanapeleka ujumbe kwa wananchi kuwa jikoni mambo sio mazuri. Eee..na sio mazuri kweli.. kama wapishi wanasema chakula kimeungua, basi yawezekana kweli kimeungua..
Mitaani watu wanachagua upande.. kuna wale wanaomsupport mama na kuna wagalilaya walio upande wa mwenzao..
Mwisho wa haya mabishano mtaani ni kufa kwa imani ya wananchi dhidi ya viongozi wao...hence..Anarchy!!
 
FB_IMG_16386175235704325.jpg
 
Kazi ya bunge ni kutunga sheria, kuishauri serikali na kuisimamia serikali..
Sio kujibizana na serikali..

Majibizano ni ishara kwamba serikali haishauriki .. na hili sio jambo jema
Majibizano ya Spika (Bunge) na Serikali ndio inaonyesha Bunge linafanya kazi yake..., Kwahio majibizano haya na yaendeleee (kwa facts bila mipasho)
 
Kwanza kabisa walaumiwe walioliharibu Bunge...hapa list ni ndefu ila Spika Ndugai hawezi kukwepa hizi lawama, pamoja na Polepole, Bashiru, Mwendazake, n.k
Hawa wamesababisha majadiliano yaliyopaswa kufanyika bungeni yafanyike mtaania...
Na hili ni tatizo maana mijadala ya mitaani ni unguided, uninformed na endless...

Nimeligusa hilo hapo juu kidogo maana kimsingi ndio lililozalisha huu mjadala wa 'mikopo na nchi kupigwa mnada' kati ya Rais Samia na Spika - Ndugai.
Nitagusia kidogo huu mjadala kisha nitamalizia na athari zake kwa imani ya wananchi juu ya watu wanaowaongoza.

1. Deni letu la taifa lina usiri mkubwa sana. Hapa Nape aliwahi kusema kuna haja ya kulifanyia 'audit' na kutafuta thamani ya fedha kwenye miradi mikubwa ya maendeleo inayoendelea. Hoja hii ikawa chungu kuliko 'mbilimbi' na mara moja ikazalisha timu ya 'wahuni' na 'viroboto'. Kama kawaida hoja ikageuka kioja na baadae ikafa kifo cha kawaida..japo umuhimu wa hoja yenyewe utaendelea kuwa hai.

2. Mama Samia ameongelea 'concession loans' zitakazoanza kulipwa baada ya miaka 20. Ukweli ni kwamba;
● Baada ya hiyo miaka 20 mama hatakuwa madarakani na hivyo sio yeye atakayelipa hayo madeni. Najua pia na yeye analipa madeni ya nyuma...HAPA...hapa ni pakiangalia sana. Utaratibu wa kiongozi kutengeneza tatizo leo litakalokuja kuonyesha makali wakati hayupo madarakani sio utaratibu mzuri kwasababu haya matatizo yatakua juu ya wananchi na vizazi vyao.
● Rais atakayekuwepo baada ya miaka 20 atahitaji pia kufanya miradi ya maendeleo kutokana na uhitaji wa jamii wakati huo, je itakuwaje? Miradi inayotegemewa kulipa hii mikopo ni pamoja na Ule wa umeme wa bwawa la Nyerere ambao kwakweli nina mashaka nao sana.. mvua ikigoma pale tutavuna tu kambale ambao sidhani kama watalipa deni. Kuna ule mwingine wa Shirika la Ndege ulioanza kuingiza hasara kabla hata haujaanza..big doubt!

3. Kauli ya Ndugai kwamba hii nchi itapigwa mnada.. hii ni alert kubwa sana kutoka kwa kiongozi wa mhimili wa bunge. Hii ni kengele ya hatari.
Ila kama kuna viongozi wa ajabu nchi hii nadhani Ndugai amewazidi wote.. yeye binafsi ameitia nchi hasara, misimamo yake imekuwa ikitegemea hali ya hewa ya siku hiyo. Huyu ameshiriki kugeuza bunge kuwa kituko na kutengeneza msingi wa maamuzi mabovu mengi ambayo mwendazake aliyafanya. Wakati wote deni linakuwa alikuwa akiangalia na kukaa kimya... leo miradi iko katikati ya utekelezaji na uchumi ukiwa umeyumba vibaya, anataka wananchi watozwe ili kuikamilisha... sasa sijui watatozwa nini??

Yote kwa pamoja, majibizano ya 'titi for tati' kati ya rais na spika wa bunge hayana afya kwa ustawi wa taifa...
Haya majibizano yanapeleka ujumbe kwa wananchi kuwa jikoni mambo sio mazuri. Eee..na sio mazuri kweli.. kama wapishi wanasema chakula kimeungua, basi yawezekana kweli kimeungua..
Mitaani watu wanachagua upande.. kuna wale wanaomsupport mama na kuna wagalilaya walio upande wa mwenzao..
Mwisho wa haya mabishano mtaani ni kufa kwa imani ya wananchi dhidi ya viongozi wao...hence..Anarchy!!
Napita nitrejea, ila nimeondoka na moja kwa sasa, yupo aliyekuwa was ajabu kuliko wote Tanzania.
 
Kazi ya bunge ni kutunga sheria, kuishauri serikali na kuisimamia serikali..
Sio kujibizana na serikali..

Majibizano ni ishara kwamba serikali haishauriki .. na hili sio jambo jema
Ushauri sio lazima uchukuliwe, kujibizana ndio kushindanisha hoja na mwisho wa siku mwenye hoja anashinikiza hoja zake zikubaliwe
 
Wanaspin mijadala tu

Tuendelee na kazi jamani
 
Majibizano ya Spika (Bunge) na Serikali ndio inaonyesha Bunge linafanya kazi yake..., Kwahio majibizano haya na yaendeleee (kwa facts bila mipasho)


Yaendelee kwa facts bila mipasho

Mungu ibariki Tanzania
 
Bunge kimsingi ni mbadala wa wananchi, ushauri wake kimsingi ndio matakwa ya wananchi...ila hii ni kama wabunge wametokana na wananchi... sio hili bunge la sasa..

Sasa unadhani ni sawa wananchi kujibizana na viongozi wao??
Ushauri sio lazima uchukuliwe, kujibizana ndio kushindanisha hoja na mwisho wa siku mwenye hoja anashinikiza hoja zake zikubaliwe
 
Kwanza kabisa walaumiwe walioliharibu Bunge...hapa list ni ndefu ila Spika Ndugai hawezi kukwepa hizi lawama, pamoja na Polepole, Bashiru, Mwendazake, n.k
Hawa wamesababisha majadiliano yaliyopaswa kufanyika bungeni yafanyike mtaania...
Na hili ni tatizo maana mijadala ya mitaani ni unguided, uninformed na endless...

Nimeligusa hilo hapo juu kidogo maana kimsingi ndio lililozalisha huu mjadala wa 'mikopo na nchi kupigwa mnada' kati ya Rais Samia na Spika - Ndugai.
Nitagusia kidogo huu mjadala kisha nitamalizia na athari zake kwa imani ya wananchi juu ya watu wanaowaongoza.

1. Deni letu la taifa lina usiri mkubwa sana. Hapa Nape aliwahi kusema kuna haja ya kulifanyia 'audit' na kutafuta thamani ya fedha kwenye miradi mikubwa ya maendeleo inayoendelea. Hoja hii ikawa chungu kuliko 'mbilimbi' na mara moja ikazalisha timu ya 'wahuni' na 'viroboto'. Kama kawaida hoja ikageuka kioja na baadae ikafa kifo cha kawaida..japo umuhimu wa hoja yenyewe utaendelea kuwa hai.

2. Mama Samia ameongelea 'concession loans' zitakazoanza kulipwa baada ya miaka 20. Ukweli ni kwamba;
● Baada ya hiyo miaka 20 mama hatakuwa madarakani na hivyo sio yeye atakayelipa hayo madeni. Najua pia na yeye analipa madeni ya nyuma...HAPA...hapa ni pakiangalia sana. Utaratibu wa kiongozi kutengeneza tatizo leo litakalokuja kuonyesha makali wakati hayupo madarakani sio utaratibu mzuri kwasababu haya matatizo yatakua juu ya wananchi na vizazi vyao.
● Rais atakayekuwepo baada ya miaka 20 atahitaji pia kufanya miradi ya maendeleo kutokana na uhitaji wa jamii wakati huo, je itakuwaje? Miradi inayotegemewa kulipa hii mikopo ni pamoja na Ule wa umeme wa bwawa la Nyerere ambao kwakweli nina mashaka nao sana.. mvua ikigoma pale tutavuna tu kambale ambao sidhani kama watalipa deni. Kuna ule mwingine wa Shirika la Ndege ulioanza kuingiza hasara kabla hata haujaanza..big doubt!

3. Kauli ya Ndugai kwamba hii nchi itapigwa mnada.. hii ni alert kubwa sana kutoka kwa kiongozi wa mhimili wa bunge. Hii ni kengele ya hatari.
Ila kama kuna viongozi wa ajabu nchi hii nadhani Ndugai amewazidi wote.. yeye binafsi ameitia nchi hasara, misimamo yake imekuwa ikitegemea hali ya hewa ya siku hiyo. Huyu ameshiriki kugeuza bunge kuwa kituko na kutengeneza msingi wa maamuzi mabovu mengi ambayo mwendazake aliyafanya. Wakati wote deni linakuwa alikuwa akiangalia na kukaa kimya... leo miradi iko katikati ya utekelezaji na uchumi ukiwa umeyumba vibaya, anataka wananchi watozwe ili kuikamilisha... sasa sijui watatozwa nini??

Yote kwa pamoja, majibizano ya 'titi for tati' kati ya rais na spika wa bunge hayana afya kwa ustawi wa taifa...
Haya majibizano yanapeleka ujumbe kwa wananchi kuwa jikoni mambo sio mazuri. Eee..na sio mazuri kweli.. kama wapishi wanasema chakula kimeungua, basi yawezekana kweli kimeungua..
Mitaani watu wanachagua upande.. kuna wale wanaomsupport mama na kuna wagalilaya walio upande wa mwenzao..
Mwisho wa haya mabishano mtaani ni kufa kwa imani ya wananchi dhidi ya viongozi wao...hence..Anarchy!!
Tunachochanganya ni kuthani kuwa miradi hii ambayo inachukuliwa fresh loans na Mh Raisi Samia ilikuwa inatekelezwa na fedha za serikali. Hali hii ililetwa na seriakli ya awamu ya 5, kusema kila kitu tunafanya kwa hela zetu, akiwa na maana kwamba hata kama yunatumia mikopo eventually tutalazimika kulipa, kwa hiyo ni fedha zetu. Wanainchi wengi hawakuielewa dhana ile, Leo tuna rais ambaye hataki kuficha kitu, akichukua mkopo anataka ueleweke wazi kuwa huu ni mkopo na tutatekeleza mradi kwa mkopo ambao tutalipa. Mimi nakubaliana na mwelekeo wa raisi kuchukua mikopo ya masharti nafuu "concessional loans" tatizo ni kuwa reli ile ikikamilika tunaitumia kwa shughuli gani za kiuchumi zitakazoifanya kurudisha gharama za ujenzi? Sioni mashamba makubwa yakifunguliwa along the railway line, sioni viwanda, kilimo along the railway line bado ni subsistence ....SIJUI
 
Bunge kimsingi ni mbadala wa wananchi, ushauri wake kimsingi ndio matakwa ya wananchi...ila hii ni kama wabunge wametokana na wananchi... sio hili bunge la sasa..

Sasa unadhani ni sawa wananchi kujibizana na viongozi wao??
Hapo hakuna bunge kuna genge la wahuni tupu
 
Kuna mtu alishauri umuhimu PPP kwenye hii miradi akajibiwa kihuni sana ila setup ya hii mradi ilikuwa na mapungufu maana zilikuwa ni fikra za mtu mmoja tu!
Tunachochanganya ni kuthani kuwa miradi hii ambayo inachukuliwa fresh loans na Mh Raisi Samia ilikuwa inatekelezwa na fedha za serikali. Hali hii ililetwa na seriakli ya awamu ya 5, kusema kila kitu tunafanya kwa hela zetu, akiwa na maana kwamba hata kama yunatumia mikopo eventually tutalazimika kulipa, kwa hiyo ni fedha zetu. Wanainchi wengi hawakuielewa dhana ile, Leo tuna rais ambaye hataki kuficha kitu, akichukua mkopo anataka ueleweke wazi kuwa huu ni mkopo na tutatekeleza mradi kwa mkopo ambao tutalipa. Mimi nakubaliana na mwelekeo wa raisi kuchukua mikopo ya masharti nafuu "concessional loans" tatizo ni kuwa reli ile ikikamilika tunaitumia kwa shughuli gani za kiuchumi zitakazoifanya kurudisha gharama za ujenzi? Sioni mashamba makubwa yakifunguliwa along the railway line, sioni viwanda, kilimo along the railway line bado ni subsistence ....SIJUI
 
Bunge kimsingi ni mbadala wa wananchi, ushauri wake kimsingi ndio matakwa ya wananchi...ila hii ni kama wabunge wametokana na wananchi... sio hili bunge la sasa..

Sasa unadhani ni sawa wananchi kujibizana na viongozi wao??
Sio kujibizana tu..., bali hata kuwakaripia na ikibidi kuwaambia mmeshindwa kazi...., Kosa kubwa ni kudhani baina ya kiongozi na mwananchi (mwananchi ndio mtumishi wa kiongozi badala ya ukweli kwamba kiongozi ndio mtumishi)

Ila all in all am all for transparency na mtu kuongea kila anachoona kipo sawa bila kufungana midomo (kwa facts lakini bila mipasho wala kejeli) tena kama vipi waite hata midahalo wanyukane kwa facts.... (hio ni for the good of the country..., hizi funika kombe mwanaharamu apite ndio hayo ya kuja kushangaa nchi inapigwa mnada kunaweza kutokea)
 
Kwanza kabisa walaumiwe walioliharibu Bunge...hapa list ni ndefu ila Spika Ndugai hawezi kukwepa hizi lawama, pamoja na Polepole, Bashiru, Mwendazake, n.k
Hawa wamesababisha majadiliano yaliyopaswa kufanyika bungeni yafanyike mtaania...
Na hili ni tatizo maana mijadala ya mitaani ni unguided, uninformed na endless...

Nimeligusa hilo hapo juu kidogo maana kimsingi ndio lililozalisha huu mjadala wa 'mikopo na nchi kupigwa mnada' kati ya Rais Samia na Spika - Ndugai.
Nitagusia kidogo huu mjadala kisha nitamalizia na athari zake kwa imani ya wananchi juu ya watu wanaowaongoza.

1. Deni letu la taifa lina usiri mkubwa sana. Hapa Nape aliwahi kusema kuna haja ya kulifanyia 'audit' na kutafuta thamani ya fedha kwenye miradi mikubwa ya maendeleo inayoendelea. Hoja hii ikawa chungu kuliko 'mbilimbi' na mara moja ikazalisha timu ya 'wahuni' na 'viroboto'. Kama kawaida hoja ikageuka kioja na baadae ikafa kifo cha kawaida..japo umuhimu wa hoja yenyewe utaendelea kuwa hai.

2. Mama Samia ameongelea 'concession loans' zitakazoanza kulipwa baada ya miaka 20. Ukweli ni kwamba;
● Baada ya hiyo miaka 20 mama hatakuwa madarakani na hivyo sio yeye atakayelipa hayo madeni. Najua pia na yeye analipa madeni ya nyuma...HAPA...hapa ni pakiangalia sana. Utaratibu wa kiongozi kutengeneza tatizo leo litakalokuja kuonyesha makali wakati hayupo madarakani sio utaratibu mzuri kwasababu haya matatizo yatakua juu ya wananchi na vizazi vyao.
● Rais atakayekuwepo baada ya miaka 20 atahitaji pia kufanya miradi ya maendeleo kutokana na uhitaji wa jamii wakati huo, je itakuwaje? Miradi inayotegemewa kulipa hii mikopo ni pamoja na Ule wa umeme wa bwawa la Nyerere ambao kwakweli nina mashaka nao sana.. mvua ikigoma pale tutavuna tu kambale ambao sidhani kama watalipa deni. Kuna ule mwingine wa Shirika la Ndege ulioanza kuingiza hasara kabla hata haujaanza..big doubt!

3. Kauli ya Ndugai kwamba hii nchi itapigwa mnada.. hii ni alert kubwa sana kutoka kwa kiongozi wa mhimili wa bunge. Hii ni kengele ya hatari.
Ila kama kuna viongozi wa ajabu nchi hii nadhani Ndugai amewazidi wote.. yeye binafsi ameitia nchi hasara, misimamo yake imekuwa ikitegemea hali ya hewa ya siku hiyo. Huyu ameshiriki kugeuza bunge kuwa kituko na kutengeneza msingi wa maamuzi mabovu mengi ambayo mwendazake aliyafanya. Wakati wote deni linakuwa alikuwa akiangalia na kukaa kimya... leo miradi iko katikati ya utekelezaji na uchumi ukiwa umeyumba vibaya, anataka wananchi watozwe ili kuikamilisha... sasa sijui watatozwa nini??

Yote kwa pamoja, majibizano ya 'titi for tati' kati ya rais na spika wa bunge hayana afya kwa ustawi wa taifa...
Haya majibizano yanapeleka ujumbe kwa wananchi kuwa jikoni mambo sio mazuri. Eee..na sio mazuri kweli.. kama wapishi wanasema chakula kimeungua, basi yawezekana kweli kimeungua..
Mitaani watu wanachagua upande.. kuna wale wanaomsupport mama na kuna wagalilaya walio upande wa mwenzao..
Mwisho wa haya mabishano mtaani ni kufa kwa imani ya wananchi dhidi ya viongozi wao...hence..Anarchy!!
Wote mnaokomalia huu mjadala ni wapumbavu kwasababu mnajadili kitu ambacho Ndugai hakumaanisha.

Mjadala umejikita kwenye UPUUZI
 
Back
Top Bottom