BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
MAJIBIZANO KATI YA ASKOFU MWAMAKULA NA PROFESA LWAITAMA!
Baada ya Askofu Mwamakula kuposti katika ukurasa wake taarifa za mwanaharakati nguli wa Haki za Binadamu, Mama Helen Kijo-Bisimba kuunga mkono kampeni za "Matembezi ya Hiyari" ya Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya, watu mbalimbali wametoa hisia zao akiwemo Prof. Azaveli Lwaitama! Yafuatayo na majibizano mafupi Kati yake na Askofu Mwamakula:
Prof. LWAITAMA: Ahaha!! Baba Askofu kweli wewe na wenzako wachache unaanza kuwa na ujasiri kama wa Askofu Desmond Tutu wa Afrika ya Kusini kipindi hiki Tanzania inapozidi kusonga mbele kwenye Harakati za Ukombozi Aaamu ya Pili. Asante sana kwa kujitoa muhanga huku Maskofu wetu na Masheikh wetu wachache!!
Askofu Mwamakula: Azaveli Lwaitama ha ha ha! Profesa! Ukweli ni kuwa Mungu hatarajii kitu kingine chochote zaidi ya kuona watu wakitenda haki katika uso wa nchi (Mika 6:8)!
Je, ni nini mtazamo wako kuona Mama huyu kuunga mkono kampeni hizi katika utu uzima wake? Unawaza nini kuhusu haki katika uso wa nchi? Unafikiri ni nguvu ya kibinadamu iliyo nyuma ya vuguvugu hili? Unafikiri wanaopambana na vuguvugu hili wanajua nguvu iliyoko nyuma yake?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Baada ya Askofu Mwamakula kuposti katika ukurasa wake taarifa za mwanaharakati nguli wa Haki za Binadamu, Mama Helen Kijo-Bisimba kuunga mkono kampeni za "Matembezi ya Hiyari" ya Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya, watu mbalimbali wametoa hisia zao akiwemo Prof. Azaveli Lwaitama! Yafuatayo na majibizano mafupi Kati yake na Askofu Mwamakula:
Prof. LWAITAMA: Ahaha!! Baba Askofu kweli wewe na wenzako wachache unaanza kuwa na ujasiri kama wa Askofu Desmond Tutu wa Afrika ya Kusini kipindi hiki Tanzania inapozidi kusonga mbele kwenye Harakati za Ukombozi Aaamu ya Pili. Asante sana kwa kujitoa muhanga huku Maskofu wetu na Masheikh wetu wachache!!
Askofu Mwamakula: Azaveli Lwaitama ha ha ha! Profesa! Ukweli ni kuwa Mungu hatarajii kitu kingine chochote zaidi ya kuona watu wakitenda haki katika uso wa nchi (Mika 6:8)!
Je, ni nini mtazamo wako kuona Mama huyu kuunga mkono kampeni hizi katika utu uzima wake? Unawaza nini kuhusu haki katika uso wa nchi? Unafikiri ni nguvu ya kibinadamu iliyo nyuma ya vuguvugu hili? Unafikiri wanaopambana na vuguvugu hili wanajua nguvu iliyoko nyuma yake?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula