Majembe Auction Mart washapewa UBUNGO

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
swali tangazo la hii tenda lilitolewa lini na SUMATRA na je mbona hatujaambiwa kama sheria za PPRA zilifuatwa na mchakato uliofanywa uliwapitisha akina nani mpaka akapatikana huyu Majembe?


surely kwa issue controversial kama UBUNGO BUS stop ilitakiwa SUMATRA waonyeshe due to public interest Business plan yao nzima na malengo gani wanayo katika kufanya kile kituo kiwe user friendly


au tunakosea kuuliza?

Halafu kwa nini PINDA hataki tuone first (original ) version ya ripoti ya CAG kuhusu UBUNGO?
 
"Kuna watu zaidi ya laki moja wanatumia kituo hiki kila siku, hatuwezi kuhatarisha usalama wa taifa kwa kuweka ripoti hii hadharani"
 
Usalama wa kulinda ufisadi ofcourse.
Toa Fisadi weka Fisadi ndio mchezo wa kisasa ,nilimuona Mama Simba kama mpayukaji sasa nimeanza kumwamini kwa kumnukuu "Katika CCM hakuna asiye fisadi"nakubaliana naye kwa asilimia mia moja kabsaaa
 
Mkuu, in the name of commission everyone becomes a servants!!! i think some of decisions a better left unknown!!!
 
Mkuu wa Usalama barabarani James Kombe akizungumza leo jijini Dar kuhusu utoaji huduma ya usafiri kupitia kampuni ya Majembe Auction Mart.

SUMATRA imeanzisha utaratibu mpya wa kuleta maboresho katika usafiri wa umma na kuondoa kero kwa wakazi wa jiji wa Dar.
Yaani Kuanzia Desemba 1, 2009 Kampuni ya MAJEMBE AUCTION MART imekasimiwa kazi ya kusimamia, kufuatilia na kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa masharti ya leseni ya kusafirisha abiria katika jiji la Dar na kituo Kikuu Cha Mabasi Ubungo.

Mbali na kufanya kazi kwa karibu na Trafiki ambao ndio wanawajibu wa kusimamia sheria zote za nchi, Mamlaka itakuwa na utaratibu wake wa kufuatilia utendaji wao.

Wenye vyombo vya Usafiri, wafanyakazi wao, abiria na wananchi kwa ujumla wanaombwa kutoa ushirikiano wa hali ya juu ili kuleta maboresho yenye manufaa kwa umma.
Kama kawaida bongo mambo tambalale ukiwa mpiga deal mambo yako safi kila siku.Hawa majembe ni kampuni ya udalali na kudai madeni sugu yaliyoshindikana,sasa suala la kushughulikia usafiri wote wa Dar pamoja na mabasi yanayokwenda mikoani hapo ubungo yamekujaje?
Wamebadilisha fani, na je leseni yao haina specification kwamba mwisho wa majukumu yao ni wapi?
Na hawa SUMATRA ndio siwaelewi kabisa ubabaishaji mtupu. SUMATRA ndio Surface and Marine Transport Authority, sasa tena Majembe! Kama wananchi jamani tunatakiwa kuwahoji hawa watu,mwisho wa yote hata TRA watapewa majembe.
TUENDAKO KAMA NCHI SINA UHAKIKA!
 
Wa madhabahuni ale madhabahuni...kama aupo madhahabahuni usiulize wanakulaje...huo ni mstari kaka upo wapi check na google
 
Hivi inakuwaje watu ambao "profession" yao ni waendesha mnada/wakala wa mahakama, wanapewa kazi kubwa kama hiyo ya kusimamia utekelezaji wa masharti ya leseni za usafirishaji? Au ni kwa sababu Memorandum and Articles of Association inawaruhusu kufanya "kazi nyingine yoyote"? Jamani, tunakwenda wapi? SUMATRA inatupeleka PABAYA sana!

./Mwana wa Haki
 
Hivi inakuwaje watu ambao "profession" yao ni waendesha mnada/wakala wa mahakama, wanapewa kazi kubwa kama hiyo ya kusimamia utekelezaji wa masharti ya leseni za usafirishaji? Au ni kwa sababu Memorandum and Articles of Association inawaruhusu kufanya "kazi nyingine yoyote"? Jamani, tunakwenda wapi? SUMATRA inatupeleka PABAYA sana!

./Mwana wa Haki

Mwanzo mgumu, labda baadaye patakuwa na makampuni mengi ya ndani yanayoweza mambo yote.
 
swali tangazo la hii tenda lilitolewa lini na SUMATRA na je mbona hatujaambiwa kama sheria za PPRA zilifuatwa na mchakato uliofanywa uliwapitisha akina nani mpaka akapatikana huyu Majembe?

Ngoja nifafanue Mkuu, ni kwamba Majembe wamepewa uwakala wa kusimamia taratibu za leseni na uratibu wa utekelezaji wa wasafirishaji kwa niaba ya SUMATRA, sio kuendesha kituo cha Ubungo. Hata hivyo SUMATRA walitakiwa kutangaza hiyo tender hilo halina ubishi kama hawakutangaza.

Mkuu wa Usalama barabarani James Kombe akizungumza leo jijini Dar kuhusu utoaji huduma ya usafiri kupitia kampuni ya Majembe Auction Mart.



SUMATRA imeanzisha utaratibu mpya wa kuleta maboresho katika usafiri wa umma na kuondoa kero kwa wakazi wa jiji wa Dar.

Yaani Kuanzia Desemba 1, 2009 Kampuni ya MAJEMBE AUCTION MART imekasimiwa kazi ya kusimamia, kufuatilia na kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa masharti ya leseni ya kusafirisha abiria katika jiji la Dar na kituo Kikuu Cha Mabasi Ubungo.



Mbali na kufanya kazi kwa karibu na Trafiki ambao ndio wanawajibu wa kusimamia sheria zote za nchi, Mamlaka itakuwa na utaratibu wake wa kufuatilia utendaji wao.




Kituo cha ubungo kiko chini ya City​
 
hapa ndipo ambapo pananitia hasira, mimi sioni sababu kwanini kazi ambazo serikali ina mamlaka maarumu za kusimamia na kuratibu zikabidhiwe third party, kama wanaona hawana uwezo basi si waongeze resources...huu ni ufisadi kwakuwa gharama wanazomlipa huyo wakara ni nyingi sana....ni mchezo mchafu tu...hawa trafiki na polisi wanafanya kazi gani, je hatuwaamini?? hatuamini ufanisi wao? hao ndio products ya system zetu na wanalipwa na serikali kwa nafasi zao, kumweka wakara afanye kazi hizo ni kuongeza gharama na kumkandamiza mhusika..demotivate...
sasa utaona watakavyotunyima raha hao jamaa, wanahistoria ya vurugu, ubabe...
kila siku sisi ni wakubebeshwa mizigo tu, kwanini shughuli kama hizi zenye maslahi ya jamii wadau wasihusishwe, leo tuna zigo la stika za fire....kule kinondoni kuna kampuni imepewa uwakara wa kukusanya kodi za matangazo, hata wakikuta umetangaza mlangoni kwako wanachaji...tena wanataka malipo ndani ya siku 7 bila hivyo wanatishia kukupeleka mbele ya sheria....hujakaa vizuri kuna wengine wanapita wanasema wanakusanya pesa za afya (takataka)...ukiangalia takataka zinakaa wiki2 hawajazoa.....
mbona maisha yanafanywa magumu hivi.....ina maana wananchi hawana mamlaka ya kuamua au hata kushauri hatima ya mazingira yao......
Tanzania wajanja ndio wanokula nchi hii....HIVI YONO NI YA NANI???
 
Suala zima naona lina utata hasa lengo kubwa likiwa ni kupunguza kero kwa wasafiri na wasafirishaji abiria.
Kuna mambo ya msingi yameelezwa kuhusu kupewa tender yenyewe lakini pia 1.Hawa majembe watalipwa namna gani? kama watalipwa kutokana na faini za
wakosaji na kwenda tofauti na leseni za usafirishaji , itakuwa vipi kama
hakuna wakosaji hasa pale wote watakapo fuata sheria,
2. je hawa majembe hawatabambikia makosa wasafiri na wasafirishaji.
3. Je hawa majembe watatumia diplomasia gani kuwatimua wapiga debe
vituoni mwetu na stand ya mkoa-dsm, nahisi kuna maafa yanakuja hapo!
4.Alikuwepo Mwaibula na timu yake walifanya kazi ilionekena japo hapakosi
mapungufu kwani wengi wao walikuwa wanafahamika, je hawa Majembe
watafahamikaje kama sio loop hole ya wezi na matepeli.Hapa naamini watu
watalia hasa kwa hii BONGO
5.kwa upande ya wakatiza ruti hapo Majembe na ubabe wao watakomesha
kabisa kama wakijipanga vizuri kama wakati askari wa FFU a.ka TIGO
walipokuwa wanaanza kazi walikuwa moto!.
 
surely kwa issue controversial kama UBUNGO BUS stop ilitakiwa SUMATRA waonyeshe due to public interest Business plan yao nzima na malengo gani wanayo katika kufanya kile kituo kiwe user friendly

Tenda waliyopewa niya kukusanya mapato kituo cha mabasi Ubungo au ni kudhibiti madereva wasiofuata sheria??


headline_bullet.jpg
Sumatra yaipa rungu rasmi kuanzia leo


Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra).

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), umeipa rungu kampuni ya mnada ya Majembe Auction Mart kusimamia shughuli zote za usafiri wa daladala jijini Dar es Salaam.
Kampuni hiyo imepewa jukumu la kuhakikisha kuwa inawashughulikia madereva wachafu, wanaokatisha ruti, wanaopandisha nauli wakati wa usiku pamoja na kupita kwenye hifadhi ya barabara.
Aidha, makosa mengine ambayo kampuni hiyo itayashughulikia ni pamoja kukamata magari yaliyotoboka chini, wanayotoa moshi na mambo mengine yote yanayovunja sheria za barabarani.
Uamuzi huo ulitangazwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Israeli Sekilasa, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Sekilasa alisema kampuni hiyo itafanya kazi sambamba na jeshi la polisi ili kuhakikisha kuwa usafiri katika jiji la Dar es Salaam unaboreka.
Alisema ubabaishaji katika shughuli za kuendesha biashara ya daladala umefikia mwisho na kwamba kampuni hiyo imepewa jukumu la kusimamia utendaji wa kila siku wa magari hayo jijini.
Alifafanua kuwa kampuni hiyo itaanza kazi yake leo ambapo wafanyakazi wake watakaa katika maeneo mbalimbali kwenye barabara ili kusimamia mabasi hayo ili yaweze kufanya kazi vizuri.
Sekilasa alisema dereva yeyote ambaye atakutwa na kosa ama gari lake, Majembe Action Mart itamwandikia faini na atatakiwa kuilipa ili aruhusiwe kuingia barabarani tena.
Aliongeza kuwa usafiri katika Jiji la Dar es Salaam umekuwa na matatizo mengi hasa wakati wa usiku.
Alisema polisi wa usalama barabarani hawatoshi kuwadhibiti madereva wakorofi pamoja na wamiliki wanaokataa kutengeneza magari yao hivyo kuwepo kwa kampuni hiyo kutakomesha matatizo yote.
Sekilasa aliwaambia waandishi wa habari kuwa wasaidie kufichua utendaji wa kampuni hiyo ambayo mamlaka yake imeingia nayo mkataba wa mwaka mmoja.
Kuhusu malipo kwa kampuni hiyo, alisema itajilipa yenyewe kupitia fedha itakazotoza daladala zenye makosa.
Hata hivyo, alisema kama kampuni hiyo itashindwa kutatua matatizo ya usafiri jijini Dar es Salaam, Sumatra itavunja mkataba huo baada ya mwaka mmoja kumalizika.
Kwa muda mrefu, usafiri katika Jiji la Dar es Salaam umekuwa na matatizo hasa wakati wa usiku ambapo magari mengi hukataa kufika mwisho wa safari ama kupita njia ambazo haziruhusiwi.
Aidha, wafanyakazi katika magari hayo wamekuwa na lugha za matusi na kuwanyanyasa abiria, mambo ambayo Sekilasa alisema Kampuni ya Majembe itayadhibiti.

CHANZO: NIPASHE
 
Ngoja nifafanue Mkuu, ni kwamba Majembe wamepewa uwakala wa kusimamia taratibu za leseni na uratibu wa utekelezaji wa wasafirishaji kwa niaba ya SUMATRA, sio kuendesha kituo cha Ubungo. Hata hivyo SUMATRA walitakiwa kutangaza hiyo tender hilo halina ubishi kama hawakutangaza.




Kituo cha ubungo kiko chini ya City​

Huu ndiyo ukweli, msichanganye mambo
 
Ufalme wa dunia hutekwa na wenye nguvu na wenye nguvu ni "MAFISADI" wimbo namba moja TANZANIA
 
Tenda waliyopewa niya kukusanya mapato kituo cha mabasi Ubungo au ni kudhibiti madereva wasiofuata sheria??


headline_bullet.jpg
Sumatra yaipa rungu rasmi kuanzia leo


Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra).

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), umeipa rungu kampuni ya mnada ya Majembe Auction Mart kusimamia shughuli zote za usafiri wa daladala jijini Dar es Salaam.
Kampuni hiyo imepewa jukumu la kuhakikisha kuwa inawashughulikia madereva wachafu, wanaokatisha ruti, wanaopandisha nauli wakati wa usiku pamoja na kupita kwenye hifadhi ya barabara.
Aidha, makosa mengine ambayo kampuni hiyo itayashughulikia ni pamoja kukamata magari yaliyotoboka chini, wanayotoa moshi na mambo mengine yote yanayovunja sheria za barabarani.
Uamuzi huo ulitangazwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Israeli Sekilasa, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Sekilasa alisema kampuni hiyo itafanya kazi sambamba na jeshi la polisi ili kuhakikisha kuwa usafiri katika jiji la Dar es Salaam unaboreka.
Alisema ubabaishaji katika shughuli za kuendesha biashara ya daladala umefikia mwisho na kwamba kampuni hiyo imepewa jukumu la kusimamia utendaji wa kila siku wa magari hayo jijini.
Alifafanua kuwa kampuni hiyo itaanza kazi yake leo ambapo wafanyakazi wake watakaa katika maeneo mbalimbali kwenye barabara ili kusimamia mabasi hayo ili yaweze kufanya kazi vizuri.
Sekilasa alisema dereva yeyote ambaye atakutwa na kosa ama gari lake, Majembe Action Mart itamwandikia faini na atatakiwa kuilipa ili aruhusiwe kuingia barabarani tena.
Aliongeza kuwa usafiri katika Jiji la Dar es Salaam umekuwa na matatizo mengi hasa wakati wa usiku.
Alisema polisi wa usalama barabarani hawatoshi kuwadhibiti madereva wakorofi pamoja na wamiliki wanaokataa kutengeneza magari yao hivyo kuwepo kwa kampuni hiyo kutakomesha matatizo yote.
Sekilasa aliwaambia waandishi wa habari kuwa wasaidie kufichua utendaji wa kampuni hiyo ambayo mamlaka yake imeingia nayo mkataba wa mwaka mmoja.
Kuhusu malipo kwa kampuni hiyo, alisema itajilipa yenyewe kupitia fedha itakazotoza daladala zenye makosa.
Hata hivyo, alisema kama kampuni hiyo itashindwa kutatua matatizo ya usafiri jijini Dar es Salaam, Sumatra itavunja mkataba huo baada ya mwaka mmoja kumalizika.
Kwa muda mrefu, usafiri katika Jiji la Dar es Salaam umekuwa na matatizo hasa wakati wa usiku ambapo magari mengi hukataa kufika mwisho wa safari ama kupita njia ambazo haziruhusiwi.
Aidha, wafanyakazi katika magari hayo wamekuwa na lugha za matusi na kuwanyanyasa abiria, mambo ambayo Sekilasa alisema Kampuni ya Majembe itayadhibiti.

CHANZO: NIPASHE

I like the idea......brilliant!

Operation za Usafiri zinatakiwa ziwe na control, kwenye mambo ya health and Safety, use of the facility/ies for the intended purposes, revenue collection mpaka ratiba za usafiri

How the procurement exercise was conducted remained to be desired.....
 
labda SUMATRA watuambie valuation team yao imefanya kazi vipi mpaka ikafikia hapo iilipofikia
 
Kila tenda majembe,majembe.......tutacha lini kupeana shavu? hivi hakuna auction mart nyingine hapa Tanzania zaidi ya hawa Majembe? Tafadhali naomba mtu anieleze perfomance ya hawa jamaa na credibility yao.
 
Hii Majembe Auction Mart ni ya Mh Nani? Ama Nachanganya Madawa hapa na Mh Yono Kevela, MP Njombe Magharibi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom