Maiti yageuka ng'ombe Tanzania

kwa tunaotoka Kilombero hatupati tabu kuelewa jambo hili....baadhi ya koo fulani fulani tukiwa katika misiba yao basi mazishi huarakishwa ili kupesha maiti kugeuka simba, chatu nk........tena utasikia wanasema duuh ameshaanza kugeuka humo ndani anaota kwato basi mtakimbizwa makaburini haraka sana......koo hizo naomba nizihifadhi kwa sasa ila zipo Kilombero na huleta mitafaruku yenye sura hiyo misibani, ili kuepusha hayo basi madawa ya kienyeji huwa yanatumika kuchelewesha maiti kugeuka na wakati mwingine inabidi maiti izikwe na kipande cha ngozi ya mnyama fulani kwenye paji la uso ili hata akigeuka hapo baadae (baada ya mazishi) asiwe na madhara......ninachooamini mpuuzi ibilisi anaweza kufanya jambo lolote ku justify uwezo wake kwa wanaomwamini na kumtii kwani yeye ni mwongo toka mwanzo wala kweli haimo ndani mwake

mix with yours
Mfano Mofu...Kwa akina Lumbanga mmmmmh hata ukinjenga nyumba ukimaliza tu kifo ukichelewa kuzikwa unageuka mnyama.....Pia sehemu za Mahenge pia hipo hiyo mdau wa Kilombero.
 
NYAMBO NGALI,ni Mwanga ata mimi nimeamini.

Leonard,

mwanga according to Kamusi ya Kiswahili sanifu , Taasisi ya uchunguzi wa Kiswahili Oxford University Press, Dar Es Salaam,2002 means

1. mtu afanyaye mazingaombwe ya uchawi usiku
2. mtu anayetembea usiku badala ya kulala
3. mtu anayecheza ngoma ya mahepe

Mimi niko kwenye kundi gani na kwa sababu zipi unaniweka kundi hilo
 
Ushirikina Upo tuu, hata huko Lindi kuna mtu aliwahi kugeuka simba na bado yupo mpaka sasa, ni simba asiye na madhara kwa watu wema.
 
teh teh...nenda usukumani kunakijiji ukijidaunajua mvua itakuwa inanyesha kwako tu au ulipo, na ukitaka kupika chakula hakiivi au unajikuta unatandikwa fimbo na mtu ambae humuoni...acha mkuu haya mambo yapo ukikataa kuwa haya po basi wewe mbishi tu...

Bila shaka unazungumzia gamboshi, au sio?
 
kwa tunaotoka Kilombero hatupati tabu kuelewa jambo hili....baadhi ya koo fulani fulani tukiwa katika misiba yao basi mazishi huarakishwa ili kupesha maiti kugeuka simba, chatu nk........tena utasikia wanasema duuh ameshaanza kugeuka humo ndani anaota kwato basi mtakimbizwa makaburini haraka sana......koo hizo naomba nizihifadhi kwa sasa ila zipo Kilombero na huleta mitafaruku yenye sura hiyo misibani, ili kuepusha hayo basi madawa ya kienyeji huwa yanatumika kuchelewesha maiti kugeuka na wakati mwingine inabidi maiti izikwe na kipande cha ngozi ya mnyama fulani kwenye paji la uso ili hata akigeuka hapo baadae (baada ya mazishi) asiwe na madhara......ninachooamini mpuuzi ibilisi anaweza kufanya jambo lolote ku justify uwezo wake kwa wanaomwamini na kumtii kwani yeye ni mwongo toka mwanzo wala kweli haimo ndani mwake

mix with yours

nimebakia nacheka peke yangu ...
 
kunani bunda
juzi kati mama kajifungua jiwe
nkasikia mtu kazaa kitimoto
leo kuna maiti imegeuka ng'ombe whats going on there?



Ni kweli hiyo habari ipo lakini ni ngumu sana kuamini. Inachosema, kwa ufupi, ni kuwa mwiliw a Bi Jamida Lucas (27) mkazi wa kijiji cha Igundu wilayani Bunda uligeuka imbo na kuwa na sura ya ng'ombe muda mfupi baada ya kufariki.
Pia, pamoja na kugeuka sura na kuwa kama ng'ombe, mwili huo ulivimba sana jambo lililowafanya ndugu na waombolezaji wautoe ndani na kuuweka nje kwa hofu kuwa unaweza kuvimba zaidi na kushindwa kupita mlango wakatakapokwenda kuzika.

Baadaye ukiwa nje, mwili uliendelea kuvimba huku viungo vingine vikibadilika pia na kuanza kutoa kinyesi cha ngombe...

Nasema ni vigumu sana kuamini habari kama hizi
 
khaaa nyie waongo na hivyo vya sukari vinatoka wapi?
mtageuka paka kwa uongo we haya wee


sawa sawa_yaani mpaka uende dukani kununua sukari ndio upate kipande ulicofungiwa sukari then ukisome...hebu wekeni hii habari hapa wakuu
 
Babu wa Loriondo anaweza kuwa na ufafanuzi kwa vile yeye huwa anaoteshwa... hakuna member wa JF jirani huko amuulize? Maana magazeti yameshajua kuwa akili zetu zimechoka kufikiri nazinapokea na kukubari chochote basi wanaleta chochote wanachoona watafanya biashara.
 
Atakuwa aliiba ng'ombe wa mnyantuzu huyo. Hao wanyantuzu huwa hawaoni taabu kukugeuza pusi, ngo'ombe au mbusi. Ni noma sana hao jamaa lakini pia ni wema na wakarimu sana.
 
Kweli nimeamini mtu akisoma saaaaaana badae anakuwa mjinga katika makabila yenu hakuna mila na desturi? Mambo kama haya yalikuwa yanafanyika au ni adhabu alikuwa anaadhibiwa mtu kutokana na kile alichokitenda kilichokuwa kinafanyika kinyume na jamii inayomzunguka na hilo tukio hufanyika ili iwe fundisho kwa waliobaki wasirudie tabia kama hiyo alokuwa anaifanya marehemu.Tusijidai kusoooma sana tukazisahau mila zetu. Mbona mtu huwa anapigwa kipapai mnaletewa huko hospitali na hayo maPHD na sayansi zenu mnagwaya???????
 
Acha bwana,mi nilienda kijiji fulani cha kabila la wanyamwanga huko mbozi,nikapewa onyo nikimuona simba kijijini mida ya jioni nisishtuke,huyo ni marehemu Sinkala,alifufuka akawa simba,ila huwa hana madhara yoyote.Wenyewe wakimuona wanampa vikuku na bata,akisha kula wanamwambia aondoke na anaondoka.
 
kwa tunaotoka Kilombero hatupati tabu kuelewa jambo hili....baadhi ya koo fulani fulani tukiwa katika misiba yao basi mazishi huarakishwa ili kupesha maiti kugeuka simba, chatu nk........tena utasikia wanasema duuh ameshaanza kugeuka humo ndani anaota kwato basi mtakimbizwa makaburini haraka sana......koo hizo naomba nizihifadhi kwa sasa ila zipo Kilombero na huleta mitafaruku yenye sura hiyo misibani, ili kuepusha hayo basi madawa ya kienyeji huwa yanatumika kuchelewesha maiti kugeuka na wakati mwingine inabidi maiti izikwe na kipande cha ngozi ya mnyama fulani kwenye paji la uso ili hata akigeuka hapo baadae (baada ya mazishi) asiwe na madhara......ninachooamini mpuuzi ibilisi anaweza kufanya jambo lolote ku justify uwezo wake kwa wanaomwamini na kumtii kwani yeye ni mwongo toka mwanzo wala kweli haimo ndani mwake

mix with yours
Tunaficha nini mkuu,ni hawa ndugu zetu wandamba.Kama umeshawahi kukaa na wandamba,maumbo yao juu ni wapana chini wembamba hali inayowafanya wafanane na simba.
 
Mioyo isiyo na imani na Mungu na iliyokata tamaa na maisha ni uwanja mpana sana wa kupandikiza imani za ushirikina.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom