Maisha ya Temeke: Uhuni, defender za polisi hadi kunusurika kuuawa kisa mwanamke

Maisha ya Temeke: Uhuni, defender za polisi hadi kunusurika kuuawa kisa mwanamke

Satoh Hirosh

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2021
Posts
7,145
Reaction score
28,845
Hii ni series ya matukio yaliyotokea miaka ya 2010-2013.

Ni mtiririko wa matukio ya ujasiri,kushangaza,kufurahisha na kusikitisha. Maisha ya watoto wa Temeke.

Miaka hii ilikuwa ndiyo mwisho mwisho wa uhuni uliokithiri wa watoto wa Temeke. Bhangi,wizi,mauaji, kukimbizana na defender za polisi na Kila aina ya uovu

Kwa mtanzamo wangu,hii miaka ya 2010 hadi 2013/14 ndiyo usela mavi wa vijana wa temeke ilikuwa unaishia ishia. Japo tabia za hovyo haziishagi lakini angalau miaka hii ya sasa viunga vya Temeke vina unafuu sana.

Hizi ni enzi za mwisho mwisho za Madogo wa Temeke kuzamia Bondeni(south Africa) kwa mafungu ambapo ilikuwa inaonekana ‘mchongo’. Walipozamia South Madogo wengine walichoafanikiwa ni kurudi na macheni ya silver shingoni na Pete kwenye vidole na kuishia kujisifu ujinga na starehe walizofanya wakiwa ‘Dizonga’ kwenye miji ya Durban, Jo'burg na Capetown. Wengine walirudishwa bongo wakiwa wamelala kwenye mabox na kupakiwa ndani ya ndege za cargo na kuishia kuleta vilio kwa familia zao..tukawazika. Wengine walirudi wakiwa mateja.

Kipindi hiko mitaa ya mwembe yanga kukiwa na matamasha yaliyoandaliwa na media maarufu kama clouds na times fme,shoo ilikuwa haifiki mwisho kwa sababu wahuni walijazana kati kupora watu wakati shoo ikiwa inaendelea. Hata uweke ulinzi vipi,wahuni walikuwa wanaharibu na show haiishi salama.

Enzi hizo kulikuwa na askari maarufu wa chang’ombe Polisi aliyefahamika kwa jina la Tyson. Watu wa viunga vya Temeke wanamjua huyu jamaa.

Mitaa ya Last(Tandika), Sheraton ,Maputo ,Devis corner,kaburi Moja,mikoroshini,mtoni kichangani,Mitaa ya pugila pugila,yombo na kote huko wahuni waliisoma namba kwa shoo za huyu Mwamba wa kuitwa Tyson.

Picha linaanza,jamaa alikuwa akiwakamata hawapakii kwenye difenda.

Anawaacha mtembee Huku Mkiimba ule wimbo maarufu “Jua lile literemke” na hakuna anayethubutu kumtoroka Wala kukimbia. wahuni wote waliufyata mkia na walifika Chang'ombe police salama chini yake. Jamaa alikuwa mbabe kiasi kwamba mkikamatwa anaweza kuwaambia “ambae anaona ameonewa kwa kukamatwa ajitokeze mbele apigane na Mimi,au kama unahisi unaniweza sogea hapa mbele tuzichape ukinishinda nakuruhusu usepe kiroho safi bila kukufikisha chango'mbe(au kwa lugha ya Aggrey "anayehisi ananiweza afanye kama anajikuna tu kichwani nimwone)”.

Wahuni walitazamana na hakuna aliyethubutu kunyanyuka ili akazinese na Tyson!!

Huyu askari alipowanyoosha sana wahuni wa Temeke. Nasikia baadae alihamishiwa Arusha Kwa Mafwele (enzi hizo Mafwele alikuwa Arusha)akaenda kuparangana na wahuni wa chuga.

Uhuni Temeke ulipokuwa sugu na hakuna dalili ya kuisha nikaona hapa napaswa kufanya jambo ili kuweza kucopy au kuji-camouflage na maisha ya Temeke. Nikasema Rule of the jungle,ili uweze kusurvive lazima nawe uwe mbabe kama wababe wengine,hivyo napaswa kuingia kwenye Sanaa ya mapigano.

Unajua kwa wasioelewa maisha ya mitaa ya Temeke wanaweza kuona naongea vitu visivyo halisi ila haya ndiyo yalikuwa maisha yetu.

Kipindi hiko mtu ilikuwa siyo rahisi kukatiza mitaa ya Sheraton au relini Maputo huku umejiachia unaongea na simu. Wahuni “wanakupokea” simu yako alafu wanakuambia “haya tembea ole wako ugeuke nyuma”. Na haikuwa usiku,ila mchana wa jua Kali.

Nishawahi kushuhudia wahuni wakimpora simu mdada mitaa ya relini alafu wakawa wanampulizia Moshi wa Bhang! Na hakuna kitu alithubutu kuwafanya Wala kupiga kelele maana alijua nini kingetokea endapo angepiga kelele.

Siku zikasonga na maisha ya Temeke ya usela wa kishamba hayana dili. Defender zilikuwa Kila saa kufanya patrol. Kuna muda mtu unashinda kitaani na washikaji lakini roho ikiwa juu. Kikiwaka tu unaamsha mbio,kama swala anamkimbia Chui.

Sasa Ndipo Nikakutana na jamaa mmoja mkufunzi wa Kung Fu,jamaa anapiga mkono kama komando madafu wa Ikulu. Nikasema Wacha nijifunze Kung Fu maana maisha ya Temeke hayahitaji unyonge.

Lakini kulikuwa na kikwazo..ili ujifunze sanaa ya mapigano kwa huyu jamaa lazima uwe muislamu,maana jamaa alikuwa ostadhi na alikuwa na darasa lake la madrassa,alafu Mimi ni mkristo na sielewi chochote kuhusu uislamu ila kung Fu nahitaji kujifunza… Sasa itakuwaje?

Wanasema Ukiishi Dar ni chuo kikuu. Sasa Ukiishi Temeke enzi hizo lazima uwe mjanja na mwenye akili zaidi yenye kufanya kazi kwa speed.

Nikabadili jina,nikajiita jina feki Abdul. Ila nitamshawishi vipi ostaz kuwa Mimi ni muislamu na siyo ‘kafiri' kama Hawa ndugu zetu wanavyotuita?

Ikanibidi nigeuke jasusi.

Kuna jamaa yangu mmoja ni muislamu,alisoma madrassa nikakomaa nae kwa muda Fulani ili anipige msasa kuhusu kusoma juzuu ili nipate gia ya kuingilia Dojo. Jamaa akanifunza vitu basic nikaiva kukariri. Lengo ikuwa nikistukiwa kuwa Mimi siyo miongoni mwao ila nimezamia nijue jinsi ya kujitetea.

Pale chuo(madrassa )asubuhi ilikuwa madrassa ya watoto,usiku kuanzia saa mbili jengo linageuka kuwa dojo ya Kung Fu/karate..Wazee wa kazi tukawa tunapiga mayoko geri,mawashigeri, na staili mbalimbali za mapigano.

Siku zikaenda, upande wa karate nikaiva ila sasa mtaani hakuna ishu,ni kukimbizana na defender za polisi tu,wakipita tunatoka mafichoni tunarudi kijiwe kupiga stori.

Nikahamia Last (Tandika sokoni) kuuza nguo ila Nako hakusomeki, Huku Nako ni uhuni na wizi tu vilitamalaki. Mteja ukizubaa umeisha.

Ajira hakuna,maisha magumu,nikasema Wacha nifanye jambo…!

*********
Pale mtaani kwetu Kuna mabroo watatu walikuwa wanafanya kazi bandarini.

Enzi hizo bandari Kuna Hela na mabroo wanatamba sana.

Ukiangalia chini bro ana kiatu cha maana,walikuwa hawavai viatu “mdosho” wala cheni “goroka”. Ni shati na suruali ya bei ghali,cheni Kali,na kiatu original ,ila vyote wamepiga bandari kwenye mabaro ya nguo kwenye meli. Tena walikuwa wanavizia mabaro ya Australia yenye nguo kali.

Mabroo Walikuwa wana Hela kwa sababu walikuwa wezi balaa,licha ya kufanya kazi bandari ila walikuwa wanaiba sana. Miaka ile bandari ilikuwa inapigwa na Kila mtu. Mabroo ilikuwa Kila wanapoingia kwenye viwanja vya starehe wanatambulika kama wazee wa bandari. Wakitajwa Majina bar wanatunza kama mapapaa-hela za wizi bandarini,hahah. wakimwita mhudumu awahudumie hawamdai chenji. Wakichenji 10k wanaita uchafu-baki nayo.

Shukrani zimwendee Hayati Magufuli mana alipoingia amefanya maboresho makubwa sana bandari. Enzi hizo mabroo wa Temeke wameiba sana,tatizo walikula Bata bila kufanya mambo ya maana. Wengine wamekufa kwa magonjwa.

Kipindi hiko bandarini Redio na power window za magari ziliwakoma watoto wa Temeke.Majamaa walikuwa wanaiba hadi magari mengine yanabaki skeletons. Mtajuana nyie na wateja wenu walioagiza magari japan.

Watoto wa Temeke na kurasini walikuwa siyo watu wazuri!!

Chumbani kwa mabroo kulikuwa Kuna nguo na viatu vya Kila aina. Vyote hivi wamepiga bandari. Mademu walikuwa wakija maghetoni walikuwa wanapagawa. Ndiyo kipindi hiko nikaanza kushuhudia mambo ya three some. Mabroo walifanya uchafu wa Kila aina kisa Wana Hela za bandari.

Leo bandari Ina VAR(camera) Kila mahali,mascanner na takataka kibao za ulinzi

Tusitoke kwenye reli!!

Mabroo wakatupeleka bandari Mimi na ‘mwanangu’ Y-lala.

Huu ndiyo ukawa mwanzo wa kuishi maisha ya ustaarabu maana nilitoka kwenye kinywa cha mamba-Mtaani.. maisha ya kuishi na masela na wahuni Kila kona.

Mimi na Ylala Tukaanza kazi bandarini.

Tukawa wazee wa bandari tukiwa Madogo kabisa!!

Nilipoanza kushika vihela nikahamia mtaa mpya mbali na kule nilikokuwa naishi zamani. Nikapanga chumba Mtoni Mtongani.

Hapa ndipo kisa cha kutaka kuuawa kisa mwanamke kinaanza…

Naunganisha part two.
 
Nilipoanza kupata Hela nikahama kutoka mitaa niliyokuwa naishi(nyumbani) kisha nikahamia mtoni mtongani,kule chini wanakuita mtaa wa ndekereko(ndengereko street).

Maisha yalikuwa yanaenda vizuri tu hakukuwa na tatizo.

Siku Moja jumapili nimeamka zangu,nilikuwa na ratiba ya kufua nguo. Nikaingia kokoni kwenda kufua mana hapakuwa mbali na nyumba niliyokuwa nakaa.

Kwa niliowaacha ninaposema “nilienda kufua kokoni” ni hivi; ukienda kigamboni ukawa unapita kwenye daraja la kigamboni “Nyerere bridge” ukiangalia upande wa kulia Kuna mkondo wa bahari unaelekea upande wa kusini. Kule mbele umegawanyika umetengeneza pacha,upande mmoja umeelekea mtoni kijichi(msende sema beach,hadi vikunai-magorofa ya nssf ukaja kuungana na mto mzinga/kongowe) na hapa na hii pacha nyingine kabla ya ile pacha ya mtoni kijichi ndiyo imekuja kutokea kurasini,kule nyuma ya makao ya Kanisa katoriki-TEC,Kijiji cha wavuvi na kutokea mtoni mtongani kisha huu mkondo ukaja kuungana na mto kizinga(ule wa kongowe unaitwa mto mzinga na huu wa mtongani karibu na daraja la treni pale chini unaitwa mto kizinga).

Sasa basi, kwenye hii mikondo bahari miwili(huu wa kijichi na huu unakuja mtongani Kuna misitu mikubwa ya mikoko na chini yake Huwa yanapita maji ya bahari kipindi cha bamvua(maji kupwa/maji kujaa in English “tides”) na Kuna siku za bamvua kule chini mtongani Kuna kiwanja cha mpira kunakuwa hakuchezeki maana maji ya bahari yanajaa kuanzia saa Tisa jioni uwanja wote.

Kwenye hii mikondo bahari (hasa mtongani Kuna chemchemi za maji ambazo zinatitirisha maji kuelekea baharini. Wenyeji wa maeneo haya wamechimba visima vidogo vidogo wanachota kwa ajili ya shughuli za bustani na kufulia nguo. Sasa haya maeneo ndiyo wenyeji huyaita “KOKONI”. Hapa nilikuwa natoa elimu ya geography kidogo ya jinsi haya maneno kuanzia daraja la kigamboni hadi kijichi/mtongani.

Let's stick into our lane...

Hiyo jumapili nikaweka nguo zangu kwenye ndoo na kusogeoa KOKONI kwenda kufua. Nilipomaliza nikarudi home kuanika nguo kisha kuzisubiri ili zikauke kisha niendele na misele mingine.

Maeneo ya uswahilini huwezi kufua nguo alafu ukasepa zako,ukirudi utakuta kamba tu,wahuni wameshapita nazo.

Wakati nasubiri nguo zikauke Huku nafanya maandalizi ya chai,ghafla simu ikaingia meseji nikaangalia nani ametuma meseji muda huo nikakuta text imeandikwa “oii Satoh Hirosh jioni twenzetu mitaa ya Temeke-Kichangani nataka tukamcheki shemeji yako”. Alikuwa Mwanangu Mzee wa bandari Y-lala. Nikamjibu “poa nimekusoma”.

Jioni ikafika,Y-lala akaja home akanikuta Bado sijajiandaa.

Y-lala: Mzee baba,saa 11 hii jioni hadi muda huu haujajiandaa wakati nilishakupanga kitambo?

Mimi: Mapema yote hii tunawahi nini,Mzee? Subiri jua lipoe poe. Kwanza kichangani hapo tu siyo mbali.

Y-lala: sema jiandae kabisa,ili saa12 itukute kule,tuwahi kurudi. Tukichelewa kwenda tutachelewa pia kurudi.

Mimi: poa nimekusoma,Wacha nikaoge kabisa maana mzee ukitaka jambo lako!!? Ila kama una genye si umwite tu kwako badala ya kwenda kwao?

Y-lala: Hapana,Leo kasema hawezi Kuja,alafu we huchoki kushida home wakati ni weekend? Si tunafanya kama tunanyoosha viungo?

Mimi: poa umeshinda,Wacha nikamwage maji fasta.

Nikaingia ndani na kuzama bafuni kuoga.

Dakika kadhaa…sauti.

Oya mwanangu unaogesha scania pulling huko bafuni? Au unapiga nyet*? Fasta basi Mzee tusepe. Mbona unaoga muda mrefu sana? Ilikuwa sauti ya Y-lala.

Y-lala alikuwa anapenda kunizingua sana ile kishkaji. Alafu yeye mwongeaji,ila Mimi siyo mwongeaji. Tulikutana introvert na extrovert.

Nilipotoka bafuni(lilikuwa bafu la nje,na yeye hakuwa mbali na hilo eneo) akaniangalia usoni wakati nataka kuingia ndani Huku anatabasamu akasema “sema mwanangu huko bafuni ulikuwa una kazi mbili,mbona macho mekundu?

Mimi: Sabuni iliingia machoni bana. Mbona umenikalia kooni,kaka? Mimi siyo kama wewe,Mimi mtoto wa Mungu. Nilimjibu Huku nazama ndani nacheka. Naye akacheka Huku anaongea ila sikumzingatia.

Baada ya dakika kadhaa nikatoka nje nikiwa tayari mimejiandaa kwa safari ya kwenda kichangani.

Y-lala : sema SH unapenda sana kutupia. Mbona umepania sana kuvaa?

Mimi: sasa unataka twende kutembea tukiwa kama tunaenda kuomba kazi viwandani kwa wachina,kaka? Alafu umesahau sisi ni wazee wa bandari. Mbona unapenda unyonge?

Y-lala: Poa twenzetu,sema tupitie home nikabadili viatu.

Wakati huo jamaa ananisifia nilikuwa nimevaa black jeans plain na fulana nyeupe plain pia(manga white),shingoni nimevaa rozari na kuuweka msalaba kwa ndani. Chini nilikuwa nimevaa buyu(American boot 🥾) Rangi nyeusi. Hili boot lipo hadi Leo hii naandika. Nimelihifadhi katika archive. Huwa nagawa viatu na nguo mara kibao ila hii American boot Huwa siigawi mana Ina historia ndefu na Mimi.

Na kiukweli tangu nipo kachalii sana Mimi ni mtu ninayependa kuvaa. Na siyo kuvaa tu,Huwa napenda kuvaa vizuri. Ni muumini mkubwa wa ule msemo wa “dress well no matter what the occasion” na ile “never underestimate the power of dressing well”.

Nakumbuka miaka hiyo kwenye graduation ya darasa la Saba,sister alikuja kunitunza. Muda wa kufungua gift 🎁 nikakuta ameniwekea suruali na t-shirt. Nilipoziangalia tu nikasema kamwe siwezi kuvaa hii midosho. Si Bora sister angenipa Hela ninaenda mwenyewe kununua nguo kisha nimkabidhi aweke kwenye hii gift box!!? Ilipita kama mwezi hivi akaniuliza “mbona sijawahi kukuona umevaa hata siku Moja zawadi nilizokutunza?” Nikamjibu zile hazinitoshi kubwa,kumbe niligawa kwa mtoto wa mama mkubwa,ahahah.

Safari ya kuelekea kwa Y-lala kwenda kubadilisha viatu ikaanza…

Kisha tukaingia mtongani juu,tukavuka barabara ya kilwa na kuhamia upande wa pili kuanza kuitafuta kichangani karibu na kanisa la Roma kwa mrembo wake.

Baada ya dakika kadhaa tukafika kichangani.

Tukaonana na huyu bibie,akanichangamkia sana ile Shem mambo vipi,mara umependeza,unapenda kuwa kama mtu wa mbele Shem!! Huku anacheka.

Tuliposalimiana nikawapa nafasi ya kuongea wawili,kama unavyojua tena wapendanao.

Pale mtaani Huwa Kuna sehemu walikuwa wanakaa ambako hakuna watu wengi Wala wapita Njia,hapo wanaweza kukaa hata masaa mawili na Kuna muda wanafanya mambo yao ya ajabu mara wanyonyane mate kama unavyojua tena wapenzi wawili wakikaa pamoja ni utoto tu unaendelea.

Mimi nikasogea mbali kidogo Kuna kijiwe kimoja maarufu Huwa nawasubiri hapo. Hapa kwenye hiki kijiwe ni kijiwe cha wacheza pool table. Na boda boda Huwa wanashinda karibu na hapo kama kijiwe chao. Kwa kiasi Fulani washikaji wa hapa wananifahamu kwa sura na Mimi nawafahamu kwa sura maana karibia Kila mwezi Huwa tunakuja na Ylala kutembea hii mitaa ya kichangani na Mimi huweka hukaa hapa kijiweni kucheki pool table japo siyo mchezaji mzuri.

Sasa baada ya kama nusu saa kupita,GHAFLA nikasikia makelele kutoka upande ule alipo Y-lala na mwanamke wake. Sikujali maana hivi ni vitu vya kawaida uswahilini. Mara kelele zikazidi kiasi Kila mmoja pale kwenye pool table kupay attention nini kinaendelea upande ule.

Baada ya muda mtu mmoja mmoja akaanza kusogea upande ule. Na Mimi nikasema hapa hapaeleweki wazee wa kazi(polisi) wanaweza kuja wakati wowote,ngoja nikamcheki Y-lala tusepe zetu.

Ile nakaribia alipo Y-lala….lahaulaaa!!!

Mara nasikia “Tena ms*ng* mwenzie si huyu hapa sharo”. Nilipoangalia kwa umakini nikaona Y-lala yupo chini na demu wale akiwa amesimama lakini analia. Nikiangalia zaidi ni kama jamaangu alikuwa amepigwa na Hawa wahuni hadi kupelekea kukaa chini. Kwa ufupi jamaa alikuwa ameshataitiwa na Hawa wahuni kama wanne hivi kwa hesabu za haraka haraka.

Wakati jamaa wananitolea matusi wahuni watatu wakawa wanakuja upande wangu Huku wamefura kwa hasira. Kwa kifupi walikuwa katika mkao wa kunifanya kitu chochote kibaya. Moyo ukaanza kwenda mbio kwa woga na mshangao maana nilikuwa sijui nini Y-lala amaefanya alafu mbaya zaidi jamaa wanakuja upande wangu Huku wamekunja ngumi na mmoja anakuja Huku anavua mkanda. Lengo aje kunichapa nao ule upande wa kifungashio.

Nikasikia mwingine anasema “nyie maboya mnajikuta masharukh-khan siyo? Yani mnatoka huko mnakotoka mnakuja kutamba mtaani kwetu na kutuchukulia mademu zetu au siyo? Sasa leo ndiyo mtajua hapa mmekojoloea transformer. Unajua kwa walio kaa hood/mtaani wanaelewa maneno ya mtaani wahuni wanavyoongea. Huwa wanaongea kibabe kiasi kwamba mikwara yao hata angekuwa shetani asingethubutu kukaa..angekimbia.

Mpaka hapa nikasema hapa nipo katika hatari. Napaswa kujiokoa na napaswa kumuokoa mwanangu Y-lala.

NIKAVUTA FOCUS..!!

Jamaa hawakujua enzi hizo nilikuwa mtu wa medani. Kung Fu nilikuwa naipiga vibaya mno. Wakataka kuniingia kichwa kichwa na jamaa aliyekuwa anachomoa mkanda alikuwa wa tatu kutoka nyuma ya Hawa wawili walio mbele ambao walishanikaribia…!

Nilichofanya nilikaa kwenye stance ya pigo kwa yule mtu wa nyuma ambaye nilimwona hatari zaidi. Niliwazunguka Hawa jamaa wa mbele kwa Kasi ya mwanga na kumfikia yule wa tatu ambaye tayari alikuwa ameshasokota ule mkanda wake na kubakiza eneo dogo na kile kipande cha bizm sijui mnaita(kile chuma cha kufungua mkanda,sina uhakika na jina lake). Katika ile speed kwa kutumia mguu wa kulia nilipiga mtama mzito(back low kick) jamaa akaanguka kama mfuko alafu nikashindilia na teke karibu na jicho(nitaeleza mbele kwa nini nimeelezea kwa ufasaha kiasi hiki). Jamaa akakata moto palepale. Alafu kumbuka chini nilikuwa nimevaa American boot…alooo!!!

Jamaa wawili kabla hawajajua nilichofanya na hawajapata muda wa kutafakari nikaruka flying kick Moja,mmoja akaenda chini na huyu mwingine chap nikamtembezea yoko geri.

Wale jamaa wengine kule kwa Y-lala Bado hawakusanuka mbele yao nimesimama mtu hatari Sana. Wanasema “aagh unajifanya mtata siyo” wakamwacha Y-lala wote sasa wakawa wanakuja kwangu. Nadhani kupitia hii chance ndiyo Y-lala alichomoka na kunitoroka maana kuanzia hapo sikumwona tena. Msala wote ukabaki kwangu. Y-lala hayupo,mwanamke wake hayupo,nipo Mimi tu najitetea peke yangu.. Balaa zito!!

Jamaa baada ya kuona wenzao watatu hawainuki wakagwaya kunijia kindezi. Wakawa kama wananizunguka,alafu mmoja nikamwona kama ameshika kitu mkononi. Nikawaza Hawa wahuni hawakosi visu au vitu vyenye ncha Kali. Nisipoongeza focus na kumaliza mchezo ndani ya dakika 3 naweza kukutwa na jambo baya. Na nisipoangalia hapa nakufa…!

Nikakumbuka enzi zile najifunza kung Fu,sensei alinifundisha mambo kadhaa kuhusu kung Fu ambayo ni FOCUS, FLEXIBILITY,POWER na CONTROL. Nikasema hapa ndiyo nimeingia rasmi kwenye real battlefield.

Wale jamaa niliwapiga vibaya mno. Na kwa kuwa walikuwa wengi nilikuwa nawapiga zaidi mateke ya chini kwenye ugoko(shin kick &low kicks),wengine niliwapiga pigo la mawash geri ili wasiweze kuamka.

Jamaa walipoona wamezidiwa kwa vipigo na hali zao kuwa mbaya sana wakaanza kupiga kelele za “mwiziiiii” huyu jamaa na mwezie ni wezi”. Wakati huo tayari watu walikuwa wameshajaa. Si unajua uswhilini. Watu kibao wametuzunguka.

Alafu naitwa mwizi...!!

Watu walipojaa Kuna ambao walikuwa wanataka kuingilia ile kwa kuanza kuvunja miti iliyo karibu kama mihogo,mawe nk ila Kuna sauti zingine miongoni mwao zilikuwa zinasema “huyu dogo siyo mwizi,acheni kwanza”.

Wakati huo nilikuwa nimeshahama kutoka kuwa mtu wa kawaida na kuwa kiumbe wa ajabu. Yeyote anayeonekana mbele yangu na kunikaribia kwa namna yeyote,Hana bahati. Nilikuwa nawapiga mapigo ya either uzimike au ukae chini usiinuke kabisa.


Wakati huo pale chini Kuna watu kadhaa wameshalala hawawezi kuamka na watu walikuwa wanazidi kujaa kutoka maeneo tofauti kiasi kwamba nikazidi kuogopa.

Kuna jamaa nikasikia sauti yake kutoka mbele yangu ambako nilikuwa nimeweka stance ya pigo akiniita “white tulia kwanza,imekuwaje mbona tulikuwa pale kwenye pool table? Nini kimetokea?” Hapo ndiyo fahamu zikanijia na kuanza kurudi kuwa mtu wa kawaida. Isivyo bahati Mimi sijui kuongea. Hasa kwa speed au katika majibizano ya ana kwa ana ndiyo kabisa lazima nizidiwe kuongea.

Mimi: Nilikuwa na mshikaji wangu hapa kumcheki demu wake anaitwa Habiba(code). Sasa ghafla nikasikia sauti za kama mtu anapigwa wakati huo Mimi nipo kwenye pool table pale. Nilipokuja hapa na baadhi ya washikaji wa pale kwenye pool table kuangalia nini kinaendelea ndiyo nikaona Hawa jamaa wanakuja upande wangu na kuanza kuishambulia pasipo Mimi kujua sababu.

Jamaa aliyeniuliza swali: Ni kweli jamaa tulikuwa nae pale pool table,Oya nyie wa**** huyu dogo amewakosea nini hadi muanze kutaka kumpiga.

Jamaa mmoja pale chini: (Huku anaongea kwa maumivu makali Huku amejishika tumbo) Hawa madogo wezi **** zao.

Mwingine aliyesimama: wamewaibia nini?

Mdada: Nyie waongo,sema mmeona wivu Habiba kutembea na yule mkaka mwingine. We jumanne si umeshaachwa? Sasa mbona unazidi kumfata fata mwenzio?


Ghafla…! Watu wakaanzs kutawanyika Kila mmoja anakimbia kusikojulikana.

Kufumba na kufumbua…! Polisi Hawa hapa.

Wakatuweka chini ya ulinzi wote waliotukuta pale,wale jamaa wote hawakuweza kuinuka wakasombwa kama kuku na tukaingizwa kwenye defender kisha safari ya kuelekea ‘chang’ombe police post’ ikaanza.

Wakati huo tayari ilikuwa usiku kama saa mbili. Tukashuka police nakuingia ndani.

Afande: vua mkanda na kabidhi Kila kitu kwenye dawati kisha andikisha jina.


Mimi: Fasta nikatoa mkanda,kisha simu na wallet na kuunyonga mkanda ukawa kama jongoo aliyejisokota kisha nikaweka kwenye buyu(American boot niliyovaa) na wallet na simu nikaweka kwa kiatu kingine.

Afande; Dogo una viatu vikali hivyo,hahahah. Ngoja wenzio kesho asubuhi wakiwa wanaenda mahakamani wakitoka wapite navyo. Hapo kubali umeshapoteza hivyo viatu(akacheka Tena kwa dharau)

Mimi: Afande naomba unihifadhie basi huko kwako.

Afande: Dogo unajaribu kunitumikisha? Yani nikuhifandhie matakataka yako Huku kwenye dawati langu? (Akanitukana)

Mimi: (nikachomoa 10k kwenye wallet na kuirudisha wallet ndani ya kiatu). Afande nakuomba. Akaona nimeshika elfu Kumi akaichukua na kuvishika viatu akavihifandhi upande wao kwa chini Huku namwangalia kwa makini anapoweka.

Unajua American boot ni kiatu kikubwa sana(kina nafasi) kiasi kwamba ukihifadhi wallet na vitu vidogo vidogo vinakaa bila shida ndiyo maana nilipoweka vitu vyangu vilikaa vyote bila mtu kujua kama ndani Kuna vitu zaidi ya hivyo viatu vyenyewe. Afande akadhani ameweka viatu tu kumbe Kuna wallet yenye Hela kama 40k,simu na mkanda niliokukunja. Kumbuka nilipotoka na Ylala kwenda kutembea,kwenye wallet niliweka elfu 50. Kwa hiyo nikatoa elfu Kumi kumpa afande ili anihifadhie viatu vyangu sehemu salama maana pale kwenye viatu vingi ni kweli kesho nisingevikuta. Mtu akiruhusiwa tu kutoka korokoroni anapita na viatu vyovyote anavyoviona vinamfaa.

Tukazama ndani.

Ilikuwa kama naota maana sikuwahi kudhani siku Moja ningekuja kulala sello. Kweli kwenye maisha hatuijui kesho yetu.

Upande wa pili Y-lala baada ya kukimbia alienda Moja kwa Moja Temeke mitaa ya home kutoa taarifa ya nini kimetokea. Fasta bro na yeye wakaja hadi kichangani kuniangalia,wakapata taarifa nimepelekwa polisi. Wakaja wakakuta jina langu limeandikishwa wakapumua maana walidhani nimekufa,ahahaha.

Unajua kuitiwa mwizi mtaani na ukapona siyo mchezo. Mtaani ukiitiwa mwizi hasa hii mitaa niliyokulia hawakupi nafasi ya kujitetea,ni mawe na vipigo tu vinafuata..Hadi unakufa.

Ila Mimi kwa sababu pengine kuonekana pale kwenye pool table au niseme Mungu hakutaka kuruhusu nife ile siku,basi nilipona.

Usiku mule ndani sikulala. Aisee cello siyo pazuri hata kidogo.

Kadili muda ulivyozidi kwenda walikuwa wanaingizwa watu wa ajabu ajabu. Huyu kaja anavuja damu,huyu mwingine anatembelea mikono,kachezea kipondo mtaani akaokolewa na polisi,anaburuza miguu Huku anaacha alama za damu chini.

Yani hadi chooni Kuna watu wametulia hawana habari.

Jamaa mmoja akaniuliza “we sharo umekuja kufanya nini humu? Mbona hufananii na haya mazingira?”

Nikawa Sina jibu nimekausha tu maana walionifanya nimeingia ndani nipo nao hapo hapo wamelala wengi wao hawawezi kutembea.

Yule jamaa niliyempa teke la jicho ndiyo nikamwona vizuri mle ndani asee!! kumbe nilimuumiza sana na lile boot,alikuwa anavuja damu alafu analia chini chini.

Huruma ikaniingia.

Asubuhi ndugu wakaja kuniletea chakula na kuniona.Ghafla nikasikia jina langu linaitwa nikaamka ghafla.

Nikatoka nje nikamkuta Brother pale kwenye dawati. Afande wa kike akaniuliza “wewe ndiye Satoh Hirosh?” Nikamjibu ndiyo?

Afande: mbona unakuwa muhuni alafu hufanani na uhuni?

Mimi: Kimya,nikavuta tu pumzi.

Bro alikuwa ananitazama kwa hasira sana.

Sikumbuki hata nililetewa nini maana sikutaka kula chochote,nikarudi ndani.

Bro na wengine waliokuja kunicheki wakakaa kule nje kabisa kungojea muda. Nadhani walikuwa wanafanya process za kunitoa.

Baadae muda wa saa nane mchana nikaitwa Tena nikaambiwa umetolewa ila kesho unatakiwa uje kituoni. Kesho mnapaswa muende mahakamani. Moyo ukafanya paaa! Nikajiuliza kwamba kesi imekuwa kubwa kiasi hiki kweli? Sasa si nitafungwa!! Maana jamaa kule ndani walikuwa hawawezi kutembea.

Afande: umeacha viatu,mkanda,wallet na simu. Kagua vitu vyako kama vipo na vimetimia kisha upotee. Alafu dogo acha uhuni utapotea.

Mimi: afande vitu vyangu vipo huko kwenu.

Afande: Huku vimefikaje?

Mimi: nilimwomba afande wa Jana usiku anihifadhie huko.

Afande: (Huku maafande wengine pia wakinikazia macho) dogo unaonekana unajiamini sana eeh? Hii ni mara ya ngapi kufika hapa?

Afande Alikuwa ananiuliza Huku ameinama chini anaangalia Huku na kule.

Mimi: (Bila kumjibu swali lake Huku nikiwa nimefocuss kuangalia kule chini upande wao) eeeh hivyo hivyo ndiyo viatu vyangu!!

Afande: (wakishirikiana na wenzie kutabasamu) dogo mjanja mjanja sana. Kumbe uliweka viatu vya bei mbaya Huku chini?

Mimi: (Huku nikiingiza mkono na kutoa kitu kimoja baada ya kingine kwenye viatu) afande vitu vyangu vimetimia.

Jamaa hawakunijibu,nikaanza safari ya kutoka nje Mimi na bro.

Njiani brother alinisema sana.

Bro: SH umeanza kujitegemea juzi tu umeshaanza uhuni. Inakuwaje unapigana na watu karibia muuane? Alafu nasikia walikuwa wanakuita mwizi,hujui kama ulibaki kidogo ufe? Unajua hii kesi ni ngumu sana maana unaweza kuozea jela hivi hivi. Nasikia wale jamaa umewaumiza sana.

Mimi: (Huku nikiwa nimezidiwa na woga baada ya kusikia naweza kuozea jela maana ni kweli jamaa wameumia sana hasa yule wa jichoni ambaye kule mwanzo nilisema nitaelezea kwa nini nilikuwa naelezea kwa ufasaha. Kule kituoni ndani ndiyo nilimshuhudia live). Kaka Mimi Sijafanya chochote kibaya,jamaa walikuwa wamenivamia.

Uzuri ndugu zangu wananijua Mimi siyo mtata Wala mkorofi na hata bro alipokuja kunitoa alikuwa ananisoma jinsi Gani najuta na kuumia kwa kilichotokea.

Kesho yake asubuhi nilifika kituoni Chang'ombe na bro. Nikapakiwa kwenye Ashok Mimi na watuhumiwa wenzangu safari ianze kwenda mahakamani.

Lakini gari ilichelewa sana kuondoka. Kumbe kule ndani brother alikuwa anajaribu kuongea na ndugu wa wale jamaa ili kesi imalizwe tu mtaani. Hata hivyo kesi ilikosa nguvu maana hakukuwa na ushahidi wowote kuwa Mimi nilikuwa mwizi na wale ndiyo watu ambao nilitaka kuwaibia. Kinyume chake wao ndiyo walionekana wezi.

Kesi iliisha mtaani na nikawa huru.

Mwanangu Y-lala aliponiona alikuwa analia tu Hana cha kuongea. Alijua mwanae ndiyo basi Tena hataniona. Samahani zilikuwa nyingi sana maana yeye na mwanamke wake walinikimbia na kuniachia msala niumalize mwenyewe.

Siku zikakatika.

Siku Moja Tena tukapanga kwenda kichangani kwa Habiba Mimi na mshikaji wangu Y-lala. Penzi kitovu cha uzembe!!

Siku hiyo nafika mitaa ile ile kwenye pool japo siku hii ilikuwa mapema zaidi nikakuta stori ya “dogo kuwapiga watu kama 15 kwa mpigo”.

Jamaa wa kwanza: Aaah mwanangu dogo alikuwa anapiga kareti vibaya mno. Alinipigia watu kama 15 ndani ya dakika kadhaa tu.

Jamaa wa pili: Kuna teke hilo alinipigia dah!! Kama nilikuwa naangalia movie asee!! Dogo yuko vizuri. Alafu huwezi kumdhania maana bonge la sharo ukimwona.

Jamaa mwingine: Sema Jamal ameumia vibaya karibu na jicho,bila kumuwahi hospitali wangetoa jicho maana lilikuwa limevimba alafu limevilia damu balaa.

Wakati huo bila wao kujua wanayemwongelea alikuwa mitaa ile ile, Mimi nilikuwa mpole tu nawasilikiliza Hawa jamaa lakini nikasema kweli mbongo mpe kichwa cha habari,stori ataitunga mwenyewe. Wale watu mbona hawakufika hata 10 alafu jamaa anasema nimewapiga kama watu 15. Yani stori Ina chai nyingi balaa.

Kwa kifupi hii stori ilikuja kuwa maarufu mitaa ile yote maana ilitembea kama moto wa msituni. Nilikuwa nasikia sehemu mbali mbali wanamsimulia huyo “dogo” pasi wao kujua mtu mwenyewe ni Mimi.

Baadae nikaachana na mambo ya kung Fu,hadi Leo Huwa napasha push up tu na mazoezi madogo madogo mara Moja moja.

Nikakomaa na Bandari..nikaitwa Mzee wa bandari.

Thank you for your time.

The End.
 
Nyongeza.

KAMA HUJASOMA HUKO JUU USISITE KUSOMA HII CHINI UTAPATA KITU.👇

Baada ya kukua nimejifunza kuwa,maisha yetu tukiwa wadogo yanatushape na kuwa hivi tulivyo sasa.

Maeneo tunapotokea Yana mchango mkubwa sana hivi tulivyo Leo. Ukimwona mtu ni mwizi, mtu wa matusi, muhuni,mtu wa dini,mstaarabu sana na tabia zote anazodisplay kwa jamii, sababu inayomfanya kuwa hivyo alivyo ni malezi ya nyumbani na makuzi ya mtaa/mitaa aliyokulia pindi akiwa mdogo.

Yes,

Kuna maeneo hayafai kwa malezi ya watoto kabisa!!

Kama haujajenga,umepanga basi unayo option ya kuchagua sehemu nzuri kwa ajili ya kuishi wewe na familia yako hasa watoto. Ila kama umeshajenga huna jinsi maana huwezi kuiamisha nyumba upeleke unapotaka wewe

Temeke ya enzi hizo uhuni umeharibu maisha ya vijana wengi sana.

Hata vijana Rika langu Kuna mambo mengi yametokea katika safari.

Wengine leo wako jela,wengine wamelamba mchanga,wapo futi Sita chini ya ardhi(wamekufa). Wengine walienda kuiba ushuani kama mbezi, kigamboni na Goba wakapigwa Shaba huko kwa washua,tukaenda kutambua miili yao hospital,tukazika na hadithi zao kuishia hapo.

Wapo wengine walioenda mbali zaidi enzi zile. Kuna ambaowalikuwa mchana wanashinda kinondoni wakijifanya kuwa wasanii na wengine kuwa dancers. Ila kumbe walikuwa na missions zao za kulia rada ‘wanene’ kisha wanawapiga.

Nakumbuka Kuna madogo waliojifanya wasanii na kuonekana kwenye video za nyimbo Fulani Fulani kipindi kile ila wameshakufa maana walipigwa Shaba maeneo ya kinondoni.

Madogo wa Temeke ilikuwa usiombe waingie ndani mwako kukuibia,hawakuwa na huruma!! Wanafaulisha Kila kitu kilicho ndani wanakuachia nyumba peke yake. Alafu ukikutana na machimbo wanayowauzia “madon” wa hizo mali za wizi ilikuwa wanauza bei ya hasara kabisa…! Ila kupata Mali ilikuwa hadi ujue code maana hakuna kuaminiana. Vichomi walikuwa wengi sana,muda wowote unauzwa.

Vijana,Kati ya vitu vya kuepuka ni tamaa na maisha ya kuflex Huku asilimia kubwa tukiwa tunafake.

Vijana tuepuke maisha ya video hasa zama hizi za digitali,washikaji wanapost wanakula Bata na maisha ya kuflex ila kiuhalisia Wana maisha magumu kukuzidi. Ila wewe kwa ujinga unadhani wewe ndiye una maisha magumu na umechelewa. Matokeo unaanza kujiingiza kwenye mambo ya hovyo ili mradi nawe uishi kidon/ kishua.

Naongea haya kwa sababu Leo maeneo kama magomeni,kinondoni na Sinza si sehemu salama kwa kulea mtoto kwa sababu ya ushoga uliotamalaki maeneo hayo.

Tunapoamua kuchagua maeneo ya kuishi tuangalie na future za watoto wetu,wakuu.

Binafsi Nimewahi kukosa mtoto mkali maeneo ya bahari beach kisa tu nilijitambulisha natokea Temeke akaniambia “mkaka mzuri sana ila unapotokea hapana kwa kweli,nyie ni wahuni sana,sitawezana na wewe”

Yote kwa yote Nashukuru sana Mungu ,pamoja na maisha mabaya niliyoishi na kushuhudia mambo mengi ya hovyo lakini sijaishia kuwa na tabia mbovu.

Ila ukweli utabaki kuwa ukweli.

…Watoto wa Temeke hatukupenda kuishi maisha mabovu kiasi kile. Ilikuwa ni Survival of the fittest, struggle for existence!!

Wengine Mungu alituokoa tu.

wengine haikuwa bahati,tulizika na wengine wameishia jela. kamanda Jisu na Cyborg wanahesabu mvua ndani ya Cello miaka sasa. Kuna walioishia kuwa mateja. Kuna waliochomwa sindano za sumu wakafa.

REST IN PEACE DULLAH NA WASHKAJI ZAKO WATATU.

Baada ya kuchokwa na mtaa kwa wizi uliokithiri mkapelekwa mto kizinga,mkafungwa kamba mikono nyuma kisha mkapigishwa magoti sura zinaangalia maji. Mlikufa kifo kibaya sana cha KUSUJUDU ndani ya maji ya mto kizinga.

Wenzenu walikuwa wanaenda kuiba ushuani kama Masaki,kigamboni na kinondoni,ila nyie mkawa mnaiba mtaani. Mtaa ukawachoka,mkachukuliwa usiku na kupelekwa Mto kizinga na hadithi yenu ikaishia hapo. Ilikuwa ni Kifo cha kikatili sana. Dah!!

All in all what I've learnt so far is,Life is a series of events.

Kumbukumbu ya Temeke inaishia hapo.

Thank you for your time.
 
Hii ni series ya matukio yaliyotokea miaka ya 2010-2013.

Ni mtiririko wa matukio ya ujasiri,kushangaza,kufurahisha na kusikitisha. Maisha ya watoto wa Temeke.

Miaka hii ilikuwa ndiyo mwisho mwisho wa uhuni uliokithiri wa watoto wa Temeke. Bhangi,wizi, kukimbizana na defender za polisi na Kila aina ya uovu

Kwa mtanzamo wangu,hii miaka ya 2010 hadi 2013/14 ndiyo usela mavi wa vijana wa temeke ilikuwa unaishia ishia. Japo tabia za hovyo haziishagi lakini angalau miaka hii ya sasa viunga vya Temeke vina unafuu sana.

Hizi ni enzi za mwisho mwisho za Madogo wa Temeke kuzamia Bondeni(south Africa) kwa mafungu ambapo ilikuwa inaonekana ‘mchongo’. Walipozamia South Madogo wengine walichoafanikiwa ni kurudi na macheni ya silver shingoni na Pete kwenye vidole na kuishia kujisifu ujinga na starehe walizofanya wakiwa ‘Dizonga’ kwenye miji ya Durban, Jo'burg na Capetown. Wengine walirudishwa bongo wakiwa wamelala kwenye mabox na kupakiwa ndani ya ndege za cargo na kuishia kuleta vilio kwa familia zao..tukawazika. Wengine walirudi wakiwa mateja.

Kipindi hiko mitaa ya mwembe yanga kukiwa na matamasha yaliyoandaliwa na media maarufu kama clouds na times fm,shoo ilikuwa haifiki mwisho kwa sababu wahuni walijazana kati kupora watu wakati shoo ikiwa inaendelea. Hata uweke ulinzi vipi,wahuni walikuwa wanaharibu na show haiishi salama.

Enzi hizo kulikuwa na askari maarufu wa chang’ombe Polisi aliyefahamika kwa jina la Tyson. Watu wa viunga vya Temeke wanamjua huyu jamaa.

Mitaa ya Last(Tandika), Sheraton ,Maputo ,Devis corner,kaburi Moja,mikoroshini,mtoni kichangani,Mitaa ya pugila pugila,yombo na kote huko wahuni waliisoma namba kwa shoo za huyu Mwamba wa kuitwa Tyson.

Picha linaanza,jamaa alikuwa akiwakamata hawapakii kwenye difenda.

Anawaacha mtembee Huku Mkiimba ule wimbo maarufu “Jua lile literemke” na hakuna anayethubutu kumtoroka Wala kukimbia. wahuni wote waliufyata mkia na walifika Chang'ombe police. Jamaa alikuwa mbabe kiasi kwamba mkikamatwa anaweza kuwaambia “ambae anaona ameonewa kwa kukamatwa ajitokeze mbele apigane na Mimi,au kama unahisi unaniweza sogea hapa mbele tuzichape ukinishinda nakuruhusu usepe kiroho safi bila kukufikisha chango'mbe”. Wahuni walitazamana na hakuna aliyethubutu kunyanyuka ili akazinese na Tyson!!

Huyu askari alipowanyoosha sana wahuni wa Temeke. Nasikia baadae alihamishiwa Arusha Kwa Mafwele (enzi hizo Mafwele alikuwa Arusha)akaparangane na wahuni wa chuga.

Uhuni Temeke ulipokuwa sugu na hakuna dalili ya kuisha nikaona hapa napaswa kufanya jambo ili kuweza kucopy maisha ya Temeke. Nikasema Rule of the jungle,ili uweze kusurvive lazima nawe uwe mbabe kama wababe wengine,hivyo napaswa kuingia kwenye Sanaa ya mapigano.

Unajua kwa wasioelewa maisha ya mitaa ya Temeke wanaweza kuona naongea vitu bisivyo halisi ila haya ndiyo yalikuwa maisha yetu. Kipindi hiko mtu ilikuwa siyo rahisi kukatiza mitaa ya Sheraton au relini Maputo huku umejiachia unaongea na simu. Wahuni “wanakupokea” simu yako alafu wanakuambia “haya tembea ole wako ugeuke nyuma”. Na haikuwa usiku,ila mchana wa jua Kali.

Nishawahi kushuhudia wahuni wakimpora simu mdada mitaa ya relini alafu wakawa wanampulizia Moshi wa Bhang! Na hakuna kitu alithubutu kuwafanya Wala kupiga kelele maana alijua nini kingetokea endapo angepiga kelele.

Siku zikasonga na maisha ya Temeke ya usela wa kishamba nikayachoka. Defender zilikuwa Kila saa kufanya patrol. Kuna muda mtu unashinda kitaani na washikaji lakini roho ukiwa juu. Kikiwaka tu unaamsha mbio,kama swala anamkimbia Chui.

Sasa Ndipo Nikakutana na jamaa mmoja mkufunzi wa Kung Fu,jamaa anapiga mkono kama komando madafu wa Ikulu. Nikasema Wacha nijifunze Kung Fu maana maisha ya Temeke hayahitaji unyonge.

Lakini kulikuwa na kikwazo..ili ujifunze sanaa ya mapigano kwa huyu jamaa lazima uwe muislamu,maana jamaa alikuwa Shehe na alikuwa na darasa lake la madrassa,alafu Mimi ni mkristo na sielewi chochote kuhusu uislamu ila kung Fu nahitaji kujifunza… Sasa itakuwaje?

Wanasema Ukiishi Dar ni chuo kikuu. Sasa Ukiishi Temeke enzi hizo lazima uwe mjanja na mwenye akili zaidi.

Nikabadili jina,nikajiita jina feki Abdul. Ila nitamshawishi vipi ostaz kuwa Mimi ni ni muislamu na siyo ‘kafiri' kama Hawa ndugu zetu wanavyotuita? Ikanibidi nigeuke jasusi.Kuna yangu mmoja muislamu,alisoma madrassa nikakomaa nae kwa muda Fulani i anipige msasa kuhusu kusoma juzuu ili nipate gia ya kuingilia Dojo. Jamaa akanifunza vitu basic nikaiva kukariri. Lengo ikuwa nikistukiwa kuwa Mimi siyo miongoni mwao ila nimezamia nijue jinsi ya kujitetea.

Pale chuo(madrassa )asubuhi ilikuwa madrassa ya watoto,usiku kuanzia saa mbili ni dojo ya Kung Fu/karate..Wazee wa kazi tukawa tunapiga mayoko geri,mawashigeri, na staili mbalimbali za mapigano.

Siku zikaenda, upande wa karate nikaiva ila sasa mtaani hakuna ishu,ni kukimbizana na defender za polisi tu,wakipita tunatoka mafichoni tunarudi kijiwe kupiga stori.

Nikahamia Last (Tandika sokoni) kuuza nguo ila Nako hakusomeki, Huku Nako ni uhuni na wizi tu vilitamalaki. Mteja ukizubaa umeisha.

Ajira hakuna,maisha magumu,nikasema Wacha nifanye jambo…!

*********
Pale mtaani kwetu Kuna mabroo watatu walikuwa wanafanya kazi bandarini.

Enzi hizo bandari Kuna Hela na mabroo wanatamba sana,ukiangalia chini bro ana kiatu cha maana,walikuwa hawavai viatu “mdosho” wala cheni “goroka”. Ni shati na suruali ya bei ghali,cheni Kali,na kiatu original ,ila vyote wamepiga bandari kwenye meli. mabroo Walikuwa wana Hela kwa sababu walikuwa wezi balaa,licha ya kufanya kazi bandari ila walikuwa wanaiba sana. Miaka ile bandari ilikuwa inapigwa na Kila mtu. Mabroo ilikuwa Kila wanapoingia wanatambulika kama wazee wa bandari. Wakitajwa Majina bar wanatunza kama mapapaa-hela za wizi bandari,hahah. wakimwita mhudumu awahudumie hawamdai chenji. Wakichenji 10k wanaita uchafu kama nayo.

Shukrani zimwendee Hayati Magufuli mana alipoingia amefanya maboresho makubwa sana bandari. Enzi hizo mabroo wa Temeke wameiba sana,tatizo walikula Bata bila kufanya mambo ya maana. Wengine wamekufa kwa magonjwa.

Kipindi hiko bandarini Redio na power window za magari ziliwakoma watoto wa Temeke.Majamaa walikuwa wanaiba hadi magari mengine yanabaki skeletons. Watoto wa Temeke na kurasini walikuwa siyo watu wazuri!!

Chumbani kwa mabroo kulikuwa Kuna nguo na viatu vya Kila aina. Vyote hivi wamepiga bandari. Mademu walikuwa wakija maghetoni walikuwa wanapagawa. Ndiyo kipindi hiko nikaanza kushuhudia mambo ya three some. Mabroo walifanya uchafu wa Kila aina kisa Wana Hela za bandari.

Leo bandari Ina VAR(camera) Kila mahali,mascanner na takataka kibao za ulinzi

Tusitoke kwenye reli!!

Mabroo wakatupeleka bandari Mimi na ‘mwanangu’ Y-lala.

Huu ndiyo ukawa mwanzo wa kuishi maisha ya ustaarabu maana nilitoka kwenye kinywa cha mamba-Mtaani.. maisha ya kuishi na masela na wahuni Kila kona. Mimi na Ylala Tukaanza kazi, tukawa wazee wa bandari tukiwa Madogo kabisa!!

Nilipoanza kushika vihela nikahamia mtaa mpya mbali na kule nilikokuwa naishi zamani. Nikapanga chumba Mtoni Mtongani.

Hapa ndipo kisa cha kutaka kuuawa kisa mwanamke kinaanza…

Naunganisha part two.
Aisee
 
Heko kwa huyo Ustadhi mkufunzi wa judo. Huku kitaa kuna jamaa ni Ustadhi fulani nadhani alipitia madrasa za namna hii, maana anapiga mkono si haba.
 
Heko kwa huyo Ustadhi mkufunzi wa judo. Huku kitaa kuna jamaa ni Ustadhi fulani nadhani alipitia madrasa za namna hii, maana anapiga mkono si haba.
Jamaa yuko vizuri sana kwenye Kung Fu,ila tulipotezana muda sana,sijui amepotelea wapi maana hata nikipata muda nikaenda ile mitaa kusalimia na kumuulizia majibu hayaeleweki.

Tatizo lake kubwa ilikuwa ni misimamo yake mikali ya kidini(extremist). Sasa kwa yaliyotokea miaka ya katikati inshu ya MKIRU(Mkuranga,kibiti na Rufiji) sijui kama alitoboa. Kwa sababu Kuna maostadhi wengi tu walifinywa kimya kimya kutokea mitaa ya sterio Temeke sokoni. Na yeye alikuwa mfanya biashara mdogo mdogo.

Huwa najaribu tu kuwaza kwa sauti kuhusu hili,Sina uhakika.
 
Jamaa yuko vizuri sana kwenye Kung Fu,ila tulipotezana muda sana,sijui amepotelea wapi maana hata nikipata muda nikaenda ile mitaa kusalimia na kumuulizia majibu hayaeleweki.

Tatizo lake kubwa ilikuwa ni misimamo yake mikali ya kidini(extremist). Sasa kwa yaliyotokea miaka ya katikati inshu ya MKIRU(Mkuranga,kibiti na Rufiji) sijui kama alitoboa. Kwa sababu Kuna maostadhi wengi tu walifinywa kimya kimya kutokea mitaa ya sterio Temeke sokoni. Na yeye alikuwa mfanya biashara mdogo mdogo.

Huwa najaribu tu kuwaza kwa sauti kuhusu hili,Sina uhakika.
Lengo la kuwa vile wale jamaa sijui ni lipi. Na vipi hakuwahi kupasha kwa Tyson?.
 
Hii ni series ya matukio yaliyotokea miaka ya 2010-2013.

Ni mtiririko wa matukio ya ujasiri,kushangaza,kufurahisha na kusikitisha. Maisha ya watoto wa Temeke.

Miaka hii ilikuwa ndiyo mwisho mwisho wa uhuni uliokithiri wa watoto wa Temeke. Bhangi,wizi, kukimbizana na defender za polisi na Kila aina ya uovu

Kwa mtanzamo wangu,hii miaka ya 2010 hadi 2013/14 ndiyo usela mavi wa vijana wa temeke ilikuwa unaishia ishia. Japo tabia za hovyo haziishagi lakini angalau miaka hii ya sasa viunga vya Temeke vina unafuu sana.

Hizi ni enzi za mwisho mwisho za Madogo wa Temeke kuzamia Bondeni(south Africa) kwa mafungu ambapo ilikuwa inaonekana ‘mchongo’. Walipozamia South Madogo wengine walichoafanikiwa ni kurudi na macheni ya silver shingoni na Pete kwenye vidole na kuishia kujisifu ujinga na starehe walizofanya wakiwa ‘Dizonga’ kwenye miji ya Durban, Jo'burg na Capetown. Wengine walirudishwa bongo wakiwa wamelala kwenye mabox na kupakiwa ndani ya ndege za cargo na kuishia kuleta vilio kwa familia zao..tukawazika. Wengine walirudi wakiwa mateja.

Kipindi hiko mitaa ya mwembe yanga kukiwa na matamasha yaliyoandaliwa na media maarufu kama clouds na times fm,shoo ilikuwa haifiki mwisho kwa sababu wahuni walijazana kati kupora watu wakati shoo ikiwa inaendelea. Hata uweke ulinzi vipi,wahuni walikuwa wanaharibu na show haiishi salama.

Enzi hizo kulikuwa na askari maarufu wa chang’ombe Polisi aliyefahamika kwa jina la Tyson. Watu wa viunga vya Temeke wanamjua huyu jamaa.

Mitaa ya Last(Tandika), Sheraton ,Maputo ,Devis corner,kaburi Moja,mikoroshini,mtoni kichangani,Mitaa ya pugila pugila,yombo na kote huko wahuni waliisoma namba kwa shoo za huyu Mwamba wa kuitwa Tyson.

Picha linaanza,jamaa alikuwa akiwakamata hawapakii kwenye difenda.

Anawaacha mtembee Huku Mkiimba ule wimbo maarufu “Jua lile literemke” na hakuna anayethubutu kumtoroka Wala kukimbia. wahuni wote waliufyata mkia na walifika Chang'ombe police. Jamaa alikuwa mbabe kiasi kwamba mkikamatwa anaweza kuwaambia “ambae anaona ameonewa kwa kukamatwa ajitokeze mbele apigane na Mimi,au kama unahisi unaniweza sogea hapa mbele tuzichape ukinishinda nakuruhusu usepe kiroho safi bila kukufikisha chango'mbe”. Wahuni walitazamana na hakuna aliyethubutu kunyanyuka ili akazinese na Tyson!!

Huyu askari alipowanyoosha sana wahuni wa Temeke. Nasikia baadae alihamishiwa Arusha Kwa Mafwele (enzi hizo Mafwele alikuwa Arusha)akaparangane na wahuni wa chuga.

Uhuni Temeke ulipokuwa sugu na hakuna dalili ya kuisha nikaona hapa napaswa kufanya jambo ili kuweza kucopy maisha ya Temeke. Nikasema Rule of the jungle,ili uweze kusurvive lazima nawe uwe mbabe kama wababe wengine,hivyo napaswa kuingia kwenye Sanaa ya mapigano.

Unajua kwa wasioelewa maisha ya mitaa ya Temeke wanaweza kuona naongea vitu bisivyo halisi ila haya ndiyo yalikuwa maisha yetu. Kipindi hiko mtu ilikuwa siyo rahisi kukatiza mitaa ya Sheraton au relini Maputo huku umejiachia unaongea na simu. Wahuni “wanakupokea” simu yako alafu wanakuambia “haya tembea ole wako ugeuke nyuma”. Na haikuwa usiku,ila mchana wa jua Kali.

Nishawahi kushuhudia wahuni wakimpora simu mdada mitaa ya relini alafu wakawa wanampulizia Moshi wa Bhang! Na hakuna kitu alithubutu kuwafanya Wala kupiga kelele maana alijua nini kingetokea endapo angepiga kelele.

Siku zikasonga na maisha ya Temeke ya usela wa kishamba nikayachoka. Defender zilikuwa Kila saa kufanya patrol. Kuna muda mtu unashinda kitaani na washikaji lakini roho ukiwa juu. Kikiwaka tu unaamsha mbio,kama swala anamkimbia Chui.

Sasa Ndipo Nikakutana na jamaa mmoja mkufunzi wa Kung Fu,jamaa anapiga mkono kama komando madafu wa Ikulu. Nikasema Wacha nijifunze Kung Fu maana maisha ya Temeke hayahitaji unyonge.

Lakini kulikuwa na kikwazo..ili ujifunze sanaa ya mapigano kwa huyu jamaa lazima uwe muislamu,maana jamaa alikuwa Shehe na alikuwa na darasa lake la madrassa,alafu Mimi ni mkristo na sielewi chochote kuhusu uislamu ila kung Fu nahitaji kujifunza… Sasa itakuwaje?

Wanasema Ukiishi Dar ni chuo kikuu. Sasa Ukiishi Temeke enzi hizo lazima uwe mjanja na mwenye akili zaidi.

Nikabadili jina,nikajiita jina feki Abdul. Ila nitamshawishi vipi ostaz kuwa Mimi ni ni muislamu na siyo ‘kafiri' kama Hawa ndugu zetu wanavyotuita? Ikanibidi nigeuke jasusi.Kuna yangu mmoja muislamu,alisoma madrassa nikakomaa nae kwa muda Fulani i anipige msasa kuhusu kusoma juzuu ili nipate gia ya kuingilia Dojo. Jamaa akanifunza vitu basic nikaiva kukariri. Lengo ikuwa nikistukiwa kuwa Mimi siyo miongoni mwao ila nimezamia nijue jinsi ya kujitetea.

Pale chuo(madrassa )asubuhi ilikuwa madrassa ya watoto,usiku kuanzia saa mbili ni dojo ya Kung Fu/karate..Wazee wa kazi tukawa tunapiga mayoko geri,mawashigeri, na staili mbalimbali za mapigano.

Siku zikaenda, upande wa karate nikaiva ila sasa mtaani hakuna ishu,ni kukimbizana na defender za polisi tu,wakipita tunatoka mafichoni tunarudi kijiwe kupiga stori.

Nikahamia Last (Tandika sokoni) kuuza nguo ila Nako hakusomeki, Huku Nako ni uhuni na wizi tu vilitamalaki. Mteja ukizubaa umeisha.

Ajira hakuna,maisha magumu,nikasema Wacha nifanye jambo…!

*********
Pale mtaani kwetu Kuna mabroo watatu walikuwa wanafanya kazi bandarini.

Enzi hizo bandari Kuna Hela na mabroo wanatamba sana,ukiangalia chini bro ana kiatu cha maana,walikuwa hawavai viatu “mdosho” wala cheni “goroka”. Ni shati na suruali ya bei ghali,cheni Kali,na kiatu original ,ila vyote wamepiga bandari kwenye meli. mabroo Walikuwa wana Hela kwa sababu walikuwa wezi balaa,licha ya kufanya kazi bandari ila walikuwa wanaiba sana. Miaka ile bandari ilikuwa inapigwa na Kila mtu. Mabroo ilikuwa Kila wanapoingia wanatambulika kama wazee wa bandari. Wakitajwa Majina bar wanatunza kama mapapaa-hela za wizi bandari,hahah. wakimwita mhudumu awahudumie hawamdai chenji. Wakichenji 10k wanaita uchafu kama nayo.

Shukrani zimwendee Hayati Magufuli mana alipoingia amefanya maboresho makubwa sana bandari. Enzi hizo mabroo wa Temeke wameiba sana,tatizo walikula Bata bila kufanya mambo ya maana. Wengine wamekufa kwa magonjwa.

Kipindi hiko bandarini Redio na power window za magari ziliwakoma watoto wa Temeke.Majamaa walikuwa wanaiba hadi magari mengine yanabaki skeletons. Watoto wa Temeke na kurasini walikuwa siyo watu wazuri!!

Chumbani kwa mabroo kulikuwa Kuna nguo na viatu vya Kila aina. Vyote hivi wamepiga bandari. Mademu walikuwa wakija maghetoni walikuwa wanapagawa. Ndiyo kipindi hiko nikaanza kushuhudia mambo ya three some. Mabroo walifanya uchafu wa Kila aina kisa Wana Hela za bandari.

Leo bandari Ina VAR(camera) Kila mahali,mascanner na takataka kibao za ulinzi

Tusitoke kwenye reli!!

Mabroo wakatupeleka bandari Mimi na ‘mwanangu’ Y-lala.

Huu ndiyo ukawa mwanzo wa kuishi maisha ya ustaarabu maana nilitoka kwenye kinywa cha mamba-Mtaani.. maisha ya kuishi na masela na wahuni Kila kona. Mimi na Ylala Tukaanza kazi, tukawa wazee wa bandari tukiwa Madogo kabisa!!

Nilipoanza kushika vihela nikahamia mtaa mpya mbali na kule nilikokuwa naishi zamani. Nikapanga chumba Mtoni Mtongani.

Hapa ndipo kisa cha kutaka kuuawa kisa mwanamke kinaanza…

Naunganisha part two.
Temeke sio watu mkuu

Nilipanga chumba enzihizo

Nkawa nagededa binti mmoja

Saa nane jamaa wakachana nyavu wanataguta simuzetu

Nilipowashtukia nkauchuna wewe kumbe wameniona wakangalia hawaoni simu

M nkajiamini wanaondoka basi ile fimbo ilikuwa ndefu nkasikia wamenipiga makalio chwaa nkiwa naingiza bushels kwa bibie dah nkalia mamamaaa ukweli tuliendelea asbh

Yaan waliosoma tambaza enzihizo mwl Julius ndie alikuwa anapiga hivyo yaan

Sinahamu nao
 
Back
Top Bottom