Mlalahoi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2006
- 2,182
- 883
Zimepoteza mwelekeo baada ya Dkt Slaa kujibu mashambulizi?Akikaa kimya watasema mbona hajakanusha.Akijibu mashambulizi wanasema kampeni zimepoteza mwelekeo.Hao akina Makamba na CCM wenzake wameanza leo hizo personal attacks?Mbona hatukuskia kelele za kampeni kupoteza mwelekeo!Hizi kampeni zimeanza kupoteza maana au mnaonaje? Kwasababu kama Dr. Slaa kaowa au hajaowa, kafukuzwa upadri au la, au kama Makamba kafukuzwa ualimu kwa kubaka au vipi...hii itawasaidia nini hawa wapiga kura hohe hahe?
Jamani eeeh, hebu tafanyeni kampeni, hii mipasho tuwachie akina Khadija Kopa na Mzee Yussuf kwenye majukwaa yao, tupeni sera...wagombea, hatuna haja ya kusikia mambo yenu ya ujana yalikuwaje...kila mtu kapitia mambo ya ajabu kwa wakati wake, hakuna ulazima wa kuyafanya kama ajenda za kisiasa.
Mkuki mtamu kwa kitimoto (nguruwe) kwa binadamu mchungu.Na mtu anayeishi kwenye nyumba ya vioo hatakiwi kuanzisha mashambulizi ya kurushiana mawe...